< Luka 24 >

1 Mapema sana siku ya kwanza ya juma, walikuja kaburini, wakileta manukato ambayo walikuwa wameyaandaa.
The however on [the] first [day] of the week dawn very early to the tomb they came bringing that they had prepared spices (and certain with them. *K)
2 Wakakuta jiwe limevingirishwa mbali na kaburi.
They found then the stone rolled away from the tomb.
3 Wakaingia ndani, lakini hawakuukuta mwili wa Bwana Yesu.
(and *k) Having entered (however *no) not they found the body of the Lord Jesus.
4 Ilitokea kwamba, wakati wamechanganyikiwa kuhusu hili, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi ya kung'aa.
And it came to pass while (perplexing *N+kO) they about this that behold men two stood by them in (garment dazzling. *N+kO)
5 Wanawake wakiwa wamejaa hofu na wakiinamisha nyuso zao chini, wakawaambia wanawake, “Kwanini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?
Terrified then were becoming they and bowing (their faces *N+kO) to the ground they said to them; Why seek you the living among the dead?
6 Hayupo hapa, ila amefufuka! Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa angali Galilaya,
Not He is here but He is risen! do remember how He spoke to you yet being in Galilee
7 akisema kwamba Mwana wa Adamu lazima atolewe kwenye mikono ya watu wenye dhambi na asulubishwe, na siku ya tatu, afufuke tena.”
saying The Son of Man that it behooves to be delivered into hands of men sinful and to be crucified and on the third day to arise.
8 Wale wanawake wakakumbuka maneno yake,
And they remembered the declarations of Him,
9 na wakarudi kutoka kaburini na wakawaambia mambo haya yote wale kumi na moja na wengine wote.
And having returned from the tomb they related these things all to the eleven and to all the rest.
10 Basi Maria Magdalena, Joana, Maria mama wa Yakobo, na wanawake wengine pamoja nao wakatoa taarifa hizi kwa mitume.
It was now Magdalene Mary and Joanna and Mary the [mother] of James and the other women with them; (who *k) were telling to the apostles these things,
11 Lakini ujumbe huu ukaonekana kama mzaha tu kwa mitume, na hawakuwaamini wale wanawake.
And appeared before them like folly the declarations (of them *N+kO) and they were not believing in them.
12 Hata hivyo Petro aliamka, na akakimbia kuelekea kaburini, na akichungulia na kuangalia ndani, aliona sanda peke yake. Petro kisha akaondoka akaenda nyumbani kwake, akistaajabu nini ambacho kimetokea.
But Peter having risen up he ran to the tomb, and having stooped down he sees the linen strips (lying *k) alone and he went away in (himself *NK+o) wondering at that having come to pass.
13 Na tazama, wawili miongoni mwao walikuwa wakienda siku hiyo hiyo katika kijiji kimoja kiitwacho Emmau, ambacho kilikuwa maili sitini kutoka Yerusalemu.
And behold two of them on same the day were going to a village being distant stadia sixty from Jerusalem whose name [is] Emmaus.
14 Wakajadiliana wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotokea.
and they themselves were talking with one another about all which having taken place these things.
15 Ikatokea kwamba, wakati walipokuwa wakijadiliana na kuulizana maswali, Yesu akasogea karibu akaambatana nao.
And it came to pass during the talking by them and reasoning that Himself Jesus having drawn near He was walking along with them.
16 Lakini macho yao yalizuiliwa katika kumtambua yeye.
but the eyes of them were held not to know Him.
17 Yesu akawaambia, “Nini ambacho ninyi wawili mnakiongelea wakati mnatembea?” Wakasimama pale wakionekana na huzuni.
He said then to them; What words [are] these that you exchange with one another walking? And (they stood still *N+KO) looking sad.
18 Mmoja wao, jina lake Cleopa, akamjibu, “Je wewe ni mtu pekee hapa Yerusalemu ambaye hajui mambo yaliyotokea huko siku hizi?”
Answering now (the *k) one (from of them *O) (whose *k) (name *NK+o) Cleopas said to Him; You yourself alone visit (in *k) Jerusalem and not have known the [things] having come to pass in it in days these?
19 Yesu akawaambia, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo kuhusu Yesu Mnazareti, ambaye alikuwa nabii, muweza katika matendo na maneno mbele za Mungu na watu wote.
And He said to them; What things? And they said to Him; The [things] concerning Jesus (of Nazareth, *N+kO) who was a man a prophet mighty in deed and word before God and all the people,
20 Na kwa jinsi ambayo wakuu wa makuhani na viongozi wetu walivyomtoa kuhukumiwa kifo na kumsulubisha.
that then delivered up him the chief priests and the rulers of us to [the] judgment of death and crucified Him.
21 Lakini tulitumaini kwamba yeye ndiye atakaye waweka huru Israeli. Ndiyo, mbali na haya yote, sasa ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.
We ourselves however were hoping that He himself it is who is about to redeem Israel. But indeed (also *no) with all these things [the] third this day brings (today *ko) away from which these things came to pass.
22 Lakini pia, baadhi ya wanawake kutoka katika kundi letu walitushangaza, baada ya kuwapo kaburini asubuhi na mapema.
However also women certain out from us amazed us Having been (at dawn *N+kO) to the tomb
23 Walipoukosa mwili wake, wakaja, wakisema kwamba waliona pia maono ya malaika waliosema kwamba yu hai.
and not having found the body of Him they came declaring also a vision of angels to have seen who say He [is] living.
24 Baadhi ya wanaume ambao walikuwa pamoja nasi walienda kaburini, na kukuta ni kama vile wanawake walivyosema. Lakini hawakumuona yeye.”
And went some of those with us to the tomb and found [it] so even as also the women said, Him however not they saw.
25 Yesu akawaambia, “Ninyi watu wajinga na wenye mioyo mizito ya kuamini yote ambayo manabii wamesema!
And He himself said to them; O foolish and slow of heart to believe in all that spoke the prophets;
26 Je haikuwa lazima Yesu kuteseka kwa mambo haya, na kuingia katika utukufu wake?”
Surely these things it was necessary for to suffer the Christ and to enter into the glory of Him?
27 Kisha kuanzia kutoka kwa Musa na manabii wote, Yesu akawatafsiria mambo yanayomuhusu yeye katika maandiko yote.
And having begun from Moses and from all the Prophets (He interpreted *N+kO) to them in all the Scriptures the [things] concerning (of Himself. *NK+o)
28 Walipokaribia kile kijiji, huko walikokuwa wakienda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea mbele.
And they drew near to the village where they were going, and He himself (appeared *N+kO) farther to be going.
29 Lakini walimlazimisha, wakisema, “Kaa pamoja nasi, maana inaelekea jioni na siku ni kama imeisha.” Hivyo Yesu akaingia kwenda kukaa nao.
And they constrained Him saying; do abide with us, for toward evening it is and has declined (now *no) the day. And He entered in to abide with them.
30 Ilitokea kwamba, wakati amekaa nao kula, alichukua mkate, akaubariki, na kuuvunja, akawapa.
And it came to pass during the reclining of Him with them having taken the bread He blessed [it] and having broken [it] He was giving [it] to them.
31 Kisha macho yao yakafunguliwa, wakamjua, na akatoweka ghafla mbele ya macho yao.
Of them then were opened the eyes and they knew Him; And He himself vanished being seen from them.
32 Wakasemezana wao kwa wao, “Hivi mioyo yetu haikuwaka ndani yetu, wakati alipoongea nasi njiani, wakati alipotufungulia maandiko?”
And they said to one another; Surely the heart of us burning it was within us as He was speaking with us on the road (and *k) as He was opening to us the Scriptures?
33 Wakanyanyuka saa hiyo hiyo, na kurudi Yerusalemu. Wakawakuta wale kumi na mmoja wamekusanyika pamoja, na wale waliokuwa pamoja nao,
And having risen up on [that] same hour they returned to Jerusalem and they found (gathered *N+kO) the eleven and those with them
34 wakisema, “Bwana amefufuka kwelikweli, na amemtokea Simoni.”
saying that Indeed has risen the Lord and He has appeared to Simon.
35 Hivyo wakawaambia mambo yaliyotokea njiani, na namna Yesu alivyodhihirishwa kwao katika kuumega mkate.
And they themselves were relating the [things] on the road and how He was known to them in the breaking of the bread.
36 Wakati wakiongea mambo hayo, Yesu mwenyewe alisimama katikati yao, na akawaambia, “Amani iwe kwenu.”
These things now when they are telling He Himself (Jesus *K) stood in midst of them and says to them; Peace to you.
37 Lakini waliogopa na kujawa na hofu, na wakafikiri kwamba waliona roho.
Having been terrified however and filled with fear having been they were thinking [themselves] a spirit to see.
38 Yesu akawaambia, Kwanini mnafadhaika? Kwanini maswali yanainuka mioyoni mwenu?
And He said to them; Why troubled are you and through why doubts do come up in (the heart *N+kO) of you?
39 Angalieni mikono yangu na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe. Niguseni na muone. Kwa maana roho haina nyama na mifupa, kama mnionavyo mimi kuwa navyo.”
do see the hands of Me and the feet of Me that I myself am He himself; do touch Me and do see for a spirit flesh and bones not has even as Me myself you see having.
40 Alipokwisha kusema hivi, akawaonyesha mikono yake na miguu yake.
And this having said (He showed *N+kO) to them the hands and the feet.
41 Walipokuwa bado na furaha iliyochanganyikana na kutokuamini, na kustaajabu, Yesu akawaambia, “Je mna kitu chochote cha kula?”
Still now while are disbelieving they for the joy and amazement He said to them; Have you anything to eat here?
42 Wakampa kipande cha samaki aliyechomwa.
And they gave to Him of a fish broiled part (and from honeycomb tablet. *KO)
43 Yesu akakichukua, na kukila mbele yao.
And having taken [it] before them He ate [it].
44 Akawaambia, “Nilipokuwa nanyi, niliwaambia kwamba yote yalioandikwa kwenye sheria ya Musa na manabii na Zaburi lazima yatimilike.”
He said now (unto *no) (to them; *N+kO) These [are] the words (of mine *NO) which I spoke to you still being with you that it behooves to be fulfilled all things which written in the law of Moses and (in the *no) Prophets and in [the] Psalms concerning Me.
45 Kisha akafungua akili zao, kwamba waweze kuyaelewa maandiko.
Then He opened their mind to understand the Scriptures
46 Akawaambia, “Kwamba imeandikwa, Kristo lazima ateseke, na kufufuka tena kutoka katika wafu siku ya tatu.
And He said to them that Thus it has been written (and thus it was necessary for *K) Was to suffer the Christ and to rise out from [the] dead on the third day
47 Na toba na msamaha wa dhambi lazima ihubiriwe kwa jina lake kwa mataifa yote, kuanzia kutokea Yerusalemu.
and to be proclaimed in the name of Him repentance (to *N+KO) forgiveness of sins to all nations (having begun *N+kO) from Jerusalem.
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
You yourselves (now *k) (are *ko) witnesses of these things,
49 Angalia, nawapelekea ahadi ya Baba yangu juu yenu. Lakini subirini hapa jijini, mpaka mtakapovishwa nguvu kutoka juu.
And behold (I myself am sending *NK+o) the promise of the Father of Mine upon you. you yourselves however do remain in the city (Jerusalem *k) until that you may be clothed with from on high power.
50 Kisha Yesu akawaongoza nje mpaka walipokaribia Bethania. Akainua mikono yake juu, na akawabariki.
He led now them out until (to *N+kO) Bethany, and having lifted up the hands of Him He blessed them.
51 Ikatokea kwamba, wakati alipokuwa akiwabariki, aliwaacha na akabebwa juu kuelekea mbinguni.
And it came to pass during the blessing by Him them He was separated from them and was carried up into heaven.
52 Basi wakamwabudu, na kurudi Yerusalemu na furaha kuu.
And they themselves having worshiped Him returned to Jerusalem with joy great
53 Waliendelea kuwepo hekaluni, wakimbariki Mungu.
and were (through *N+KO) (all [times] *N+kO) in the temple (praising and *KO) blessing God. (Amen *K)

< Luka 24 >