< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
Jésus, levant les yeux, vit les riches qui mettaient leurs offrandes dans le tronc.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
Il vit aussi une pauvre veuve qui y mettait deux pites.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
Et il dit: En vérité, je vous le déclare, cette pauvre veuve a mis plus que tous les autres.
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
Car tous ceux-là, pour leurs offrandes, ont donné de leur superflu; mais celle-ci a donné de son indigence, tout ce qu'elle avait pour vivre.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
Quelques-uns parlaient du temple, des belles pierres et des dons qui l'ornaient. Jésus dit:
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
Les jours viendront où, de ce que vous regardez, il ne restera pas ici une pierre sur une autre pierre qui ne soit renversée.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
Alors ils lui demandèrent: Maître, quand donc ces choses arriveront-elles, et à quel signe connaîtra-t-on qu'elles sont sur le point d'arriver?
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
Il répondit: Prenez garde de ne pas vous laisser séduire; car plusieurs viendront en mon nom, disant: C'est moi qui suis le Christ. Le moment approche! Ne les suivez pas!
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
Et quand vous entendrez parler de guerres et de séditions, ne vous effrayez pas, car il faut que ces choses arrivent d'abord; mais ce ne sera pas de sitôt la fin.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Il leur dit aussi: Une nation s'élèvera contre une autre nation, et un royaume contre un autre royaume.
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
Il y aura de grands tremblements de terre, des famines et des pestes en divers lieux, des phénomènes effrayants et de grands signes dans le ciel.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
Mais avant tout cela, on mettra la main sur vous, on vous persécutera, on vous livrera aux synagogues, on vous mettra en prison; et vous serez traînés devant les rois et devant les gouverneurs, à cause de mon nom.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
Cela vous arrivera pour que vous rendiez témoignage.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Mettez-vous donc bien dans l'esprit de ne pas vous préoccuper de votre défense.
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
En effet, je vous donnerai une parole pleine de sagesse, à laquelle tous vos adversaires ne pourront résister ni contredire.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
Vous serez livrés même par vos pères et vos mères, par vos frères, vos parents et vos amis; et ils feront mourir plusieurs d'entre vous.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
Vous serez haïs de tous, à cause de mon nom.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
Mais il ne se perdra pas un cheveu de votre tête.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
C'est par votre patience que vous sauverez vos âmes.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
Or, quand vous verrez Jérusalem investie par des armées, sachez, à ce moment-là, que sa ruine approche.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Que ceux qui seront alors dans la Judée s'enfuient dans les montagnes; que ceux qui seront dans l'intérieur de la ville en sortent, et que ceux qui seront dans les champs, ne se retirent pas dans la ville.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
Car ce sont là les jours de la vengeance, afin que s'accomplisse tout ce qui est écrit.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
Malheur aux femmes qui seront enceintes, et à celles qui allaiteront en ces jours-là! Car il y aura une grande détresse dans le pays et une grande colère contre ce peuple.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
Ils tomberont sous le tranchant de l'épée, ils seront emmenés captifs parmi toutes les nations; et Jérusalem sera foulée aux pieds par les Païens, jusqu'à ce que les temps des nations païennes soient accomplis.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
Il y aura des signes dans le soleil, dans la lune et dans les étoiles; et, sur la terre, l'angoisse s'emparera des nations troublées par le fracas de la mer et des flots.
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
Les hommes rendront l'âme de frayeur, dans l'attente des maux qui viendront sur le monde; car les puissances des cieux seront ébranlées.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
Alors on verra le Fils de l'homme venant sur une nuée, avec une grande puissance et une grande gloire.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
Lorsque ces choses commenceront à arriver, redressez-vous et levez vos têtes, parce que votre délivrance est proche.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
Puis il leur dit une parabole: Voyez le figuier et tous les autres arbres;
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
quand ils commencent à pousser, vous savez de vous-mêmes, en les voyant, que l'été est déjà proche.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
De même, lorsque vous verrez ces choses arriver, sachez que le royaume de Dieu est proche.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
En vérité, je vous le dis, cette génération ne passera pas, que toutes ces choses n'arrivent.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Le ciel et la terre passeront; mais mes paroles ne passeront point.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
Prenez donc garde à vous-mêmes, de peur que vos coeurs ne soient appesantis par les excès de la bonne chère, par l'ivresse et par les inquiétudes, de cette vie, et que ce jour-là ne vienne subitement sur vous,
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
comme un filet; car il surprendra tous ceux qui habitent la surface de la terre entière.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Veillez donc en tout temps et priez, afin que vous puissiez échapper à tous ces maux qui doivent arriver, et subsister devant le Fils de l'homme.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
Or, Jésus enseignait dans le temple pendant le jour; mais le soir, il sortait et passait les nuits sur la montagne appelée montagne des Oliviers.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
Et, dès le point du jour, tout le peuple venait à lui dans le temple pour l'écouter.

< Luka 21 >