< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
Et ayant levé les yeux, il vit les riches qui jetaient dans le trésor leurs offrandes;
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
mais il vit une certaine veuve indigente qui y jetait deux pites,
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
et il dit: « En vérité je vous déclare que cette veuve pauvre a jeté plus que personne,
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
car tous ceux-là ont jeté de leur superflu dans les offrandes, tandis que cette femme a jeté, de son dénuement, tout ce qu'elle avait pour sa subsistance. »
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
Et quelques personnes disant à propos du temple, qu'il était orné de belles pierres et d'offrandes, il dit:
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
« Ces choses que vous voyez…, des jours viendront où il ne sera laissé ici pierre sur pierre qui ne soit démolie. »
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
Mais ils l'interrogèrent, en disant: « Maître, quand donc cela aura-t-il lieu? Et quel sera le signe qui indiquera que ces choses sont sur le point d'arriver? »
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
Or il dit: « Prenez garde de ne pas vous laisser égarer; car plusieurs viendront en mon nom, disant: « C'est moi qui le suis, et le moment approche; » ne vous mettez pas à leur suite.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
Mais quand vous entendrez parler de guerres et de révolutions, ne vous en effrayez pas, car il faut que cela arrive premièrement, mais ce n'est pas tout aussitôt la fin. »
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Alors il leur disait: « Une nation s'élèvera contre une nation, et un royaume contre un royaume;
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
et il y aura de grands tremblements de terre, et place par place des pestes et des famines; et il y aura des phénomènes effrayants et de grands signes qui viendront du ciel;
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
mais avant toutes ces choses ils mettront les mains sur vous, et ils vous persécuteront, vous livrant aux synagogues et vous jetant en prison, vous traînant devant des rois et des gouverneurs à cause de mon nom.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
Cela sera pour vous l'occasion d'un témoignage;
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
mettez donc en vos cœurs de ne pas songer d'avance à votre défense,
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
car c'est moi qui vous donnerai une bouche et une sagesse, à laquelle tous vos adversaires ne pourront résister ni répliquer.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
Mais vous serez livrés même par vos parents, et par vos frères, et par des membres de votre famille, et par des amis, et ils en mettront à mort d'entre vous,
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
et vous serez haïs de tous à cause de mon nom;
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
et pas un cheveu de votre tête ne sera certainement perdu;
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
c'est par votre patience que vous vous mettrez en possession de vos âmes.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
« Mais quand vous aurez vu Jérusalem investie par les armées, alors sachez que sa dévastation est proche.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Alors que ceux qui sont en Judée s'enfuient dans les montagnes, et que ceux qui sont au milieu de la ville se retirent, et que ceux qui sont dans les campagnes n'y rentrent pas;
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
car ce sont là des jours de châtiment, afin que tout ce qui a été écrit s'accomplisse.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
Malheur à celles qui sont enceintes et à celles qui allaitent en ces jours-là! Car il y aura une grande calamité sur la terre et de la colère contre ce peuple,
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
et ils tomberont par le fil de l'épée, et ils seront emmenés captifs chez toutes les nations, et Jérusalem sera foulée aux pieds par les Gentils, tant que dureront les temps des Gentils et jusques à ce qu'ils soient accomplis.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
« Et il y aura des signes dans le soleil, la lune et les astres, et sur la terre de l'angoisse parmi les nations inquiètes du fracas de la mer et des flots,
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
les hommes expirant de frayeur à l'attente de ce qui menace la terre, car les puissances des cieux seront ébranlées.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
Et alors ils verront le fils de l'homme venant dans une nuée avec beaucoup de puissance et de gloire.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
Mais quand ces choses commenceront à se réaliser, redressez-vous et levez la tête, car votre délivrance approche. »
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
Et il leur dit une parabole: « Voyez le figuier et tous les arbres:
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
quand ils ont commencé à pousser, vous savez d'après eux en les regardant que déjà l'été est proche.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
De même, vous aussi, quand vous aurez vu ces choses se réaliser, sachez que le royaume de Dieu est proche.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
En vérité je vous déclare que cette génération-ci ne disparaîtra certainement point, jusques à ce que tout se soit réalisé.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Le ciel et la terre passeront, mais mes paroles ne passeront certainement point.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
Mais prenez garde à vous-mêmes, de peur que vos cœurs ne s'appesantissent dans les excès, dans l'ivresse, et dans les soucis de la vie, et que ce jour-là ne vous surprenne tout à coup
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
comme un filet; car il surprendra tous ceux qui habitent la surface de toute la terre;
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
mais veillez, priant en tout temps, afin que vous puissiez échapper à toutes ces choses qui doivent survenir, et vous trouver debout en présence du fils de l'homme. »
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
Or, pendant le jour, il enseignait dans le temple, mais tous les soirs il sortait pour passer la nuit sur la montagne appelée Bois d'oliviers;
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
et tout le peuple venait de bon matin vers lui dans le temple pour l'entendre.

< Luka 21 >