< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
And He looked up and saw the rich people bringing their gifts to the treasury:
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
and He saw also a poor widow throwing in two mites.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
And He said, Verily I tell you, this poor widow hath put in more than they all.
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For all these have out of their abundance contributed to the offerings of God: but she out of her penury hath given all she had.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
And as some were speaking of the temple; how it was adorned with beautiful stones and gifts, He said, As for these things which ye see,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
the days will come, in which there shall not be left one stone upon another, that shall not be demolished.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
And they asked Him, saying, Master, when shall these things be? And what will be the sign when these things shall come to pass?
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And He said, Take heed that ye be not deceived; for many shall come in my name, saying, I am the Christ; and the time is near: but do not therefore go after them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
And when ye shall hear of wars and commotions, be not terrified: for these must first happen; but the end will not be directly.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then said He unto them, Nation shall rise against nation, and kingdom against kingdom;
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
and there will be great earthquakes in several places, and famines, and pestilences, and fearful sights and great prodigies from heaven.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
But before all these things they will lay hands on you, and persecute you, delivering you up to synagogues, and prisons, being brought before kings and rulers for my name's sake:
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
but it shall be for a testimony to you.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Fix it therefore in your hearts not to premeditate a defence: for I will give you a mouth and wisdom,
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
which all your adversaries shall not be able to contradict nor withstand.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
But ye shall be betrayed even by parents, and brethren, and kindred and friends; and some of you shall they cause to be put to death:
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
and ye will be hated by all men for my sake.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
But not an hair of your head shall perish.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
In your patience therefore possess your souls.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
And when ye shall see Jerusalem surrounded with armies, then know that the desolation thereof is nigh: then let them that are in Judea flee to the mountains,
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
and those that are in the midst of it, depart; and let not them that are in the countries enter into it.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
For these are days of vengeance, that all things which are written may be fulfilled.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
But wo to them that are with child, and to them that give suck in those days; for there shall be great distress in the land, and wrath upon this people,
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
and they shall fall by the edge of the sword, and be led captive into all nations: and Jerusalem shall be trampled down by the Gentiles, till the times of the Gentiles too shall be fulfilled.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
And there shall be signs in the sun, and in the moon, and in the stars; and on the earth distress of nations in perplexity, the sea and the waves roring:
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
and men ready to die for fear and apprehension of the things that are coming upon the land; for the powers of heaven shall be shaken.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
And then shall they see the Son of man coming, as on a cloud, with power and great glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
But when these things begin to come to pass, look upwards and lift up your heads, for your redemption draweth nigh.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And He spake a parable to them, Behold the fig-tree,
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
and all the trees, when they shoot out, ye see and know of yourselves that summer is now near:
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
so likewise know ye, when ye see these things coming to pass, that the kingdom of God is at hand.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Verily I tell you, this generation shall not pass away till all be accomplished.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Heaven and earth shall pass away, but my words shall not pass away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
Take heed to yourselves, least at any time your hearts be overcharged with surfeiting and drunkenness, and the cares of life, and so that day should come upon you unawares:
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
for as a snare shall it come upon all that dwell on the face of the whole earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Watch therefore and be constant in prayer, that ye may be counted worthy to escape all these things, which shall come to pass, and to stand before the Son of man.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
Thus He was by day teaching in the temple; and at night He retired to the mount called the mount of Olives.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people came early in the morning to Him in the temple to hear Him.

< Luka 21 >