< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
As he behelde he sawe the ryche men how they cast in their offeringes into the treasury.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
And he sawe also a certayne povre widdowe which cast in thyther two mites.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
And he sayde: of a trueth I saye vnto you this poore wyddowe hath put in moare then they all.
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For they all have of their superfluyte added vnto the offerynge of God: but she of her penury hath cast in all the substaunce that she had.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
As some spake of the teple how it was garnesshed with goodly stones and iewels he sayde.
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
The dayes will come whe of these thynges which ye se shall not be lefte stone apon stone that shall not be throwen doune.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
And they axed him sayinge: Master whe shall these thinges be and what signe will therbe whe suche thinges shall come to passe.
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And he sayd: take hede that ye be not deceaved. For many will come in my name saying: I am he: and the tyme draweth neare. Folowe ye not them therfore.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
But when ye heare of warre and of dissencion: be not afrayd. For these thinges must fyrst come: but the ende foloweth not by and by.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then sayd he vnto the: Nacion shall ryse agaynst nacion and kingdom agaynst kyngdome
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
and greate erthquakes shall be in all quarters and honger and pestilence: and fearfull thinges. And greate signes shall therbe from heven.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
But before all these they shall laye their hondes on you and persecute you delyueringe you vp to the sinagoges and into preson and bringe you before kynges and rulers for my names sake.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
And this shall chaunce you for a testimoniall.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Let it sticke therfore faste in youre hertes not once to stody before what ye shall answere:
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
for I will geve you a mouth and wisdome where agaynste all youre adversarys shall not be able to speake nor resist.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
Ye and ye shalbe betrayed of youre fathers and mothers and of youre brethren and kynsmen and lovers aud some of you shall they put to deeth.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
And hated shall ye be of all men for my names sake.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
Yet ther shall not one heer of youre heedes perisshe.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
With youre pacience possesse youre soules.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
And when ye se Ierusalem beseged with an hoste then vnderstonde that the desolacio of the same is nye.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then let them which are in Iewrye flye to the mountaynes. And let them which are in the middes of it departe oute. And let not them that are in other countreis enter ther in.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
For these be the dayes of vengeance to fulfill all that are writte.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
But wo be to them that be with chylde and to them that geve sucke in those dayes: for ther shalbe greate trouble in the londe and wrath over all this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
And they shall fall on the edge of the swearde and shalbe leed captive into all nacions. And Ierusalem shalbe trooden vnder fote of the gentyls vntyll the tyme of the gentyls be fulfilled.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
And ther shalbe signes in the sunne ad in the mone and in the starres: and in ye erth the people shalbe in soche perplexite yt they shall not tell which waye to turne them selves. The see and the waters shall roore
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
and menes hertes shall fayle them for feare and for lokinge after thoose thinges which shall come on the erth. For the powers of heve shall move.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
And then shall they se the sonne of ma come in a clowde with power and greate glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
When these thinges begyn to come to passe: then loke vp and lifte vp youre heddes for youre redemcion draweth neye.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And he shewed the a similitude: beholde ye fygge tree and all other trees
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
when they shute forth their buddes ye se and knowe of youre awne selves that sommer is then nye at hod.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
So lyke wyse ye (when ye se these thinges come to passe) vnderstonde that the kyngdome of God is neye.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Verely I saye vnto you: this generacion shall not passe tyll all be fulfilled.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Heaven and erth shall passe: but my wordes shall not passe.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
Take hede to youre selves lest youre hertes be overcome with surfettinge and dronkennes and cares of this worlde: and that that daye come on you vnwares.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
For as a snare shall it come on all them that sit on the face of the erthe.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Watche therfore continually and praye that ye maye obtayne grace to flye all this that shall come and that ye maye stonde before the sonne of man.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
In the daye tyme he taught in the temple and at night he went out and had abydinge in the mount olivete.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people came in the morninge to him in the temple for to heare him.

< Luka 21 >