< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
Looking up, Jesus saw the rich people putting their gifts into the chests for the Temple offerings.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
He saw, too, a widow in poor circumstances putting two farthings into them.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
On this he said: “I tell you that this poor widow has put in more than all the others;
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
for every one else here put in something from what he had to spare, while she, in her need, has put in all she had to live upon.”
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
When some of them spoke about the Temple being decorated with beautiful stones and offerings, Jesus said:
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
“As for these things that you are looking at, a time is coming when not one stone will be left upon another here, which will not be thrown down.”
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
So the disciples questioned Jesus: “But, Teacher, when will this be? and what sign will there be when this is near?”
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And Jesus said: “See that you are not led astray; for many will take my name, and come saying ‘I am He,’ and ‘The time is close at hand.’ Do not follow them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
And, when you hear of wars and disturbances, do not be terrified, for these things must occur first; but the end will not be at once.”
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then he said to them: “‘Nation will rise against nation and kingdom against kingdom,’
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
And there will be great earthquakes, and plagues and famines in various places, and there will be terrible appearances and signs in the heavens.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
Before all this, they will lay hands on you and persecute you, and they will betray you to Synagogues and put you in prison, when you will be brought before kings and governors for the sake of my Name.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
Then will be your opportunity of witnessing for me.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Make up your minds, therefore, not to prepare your defence;
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
for I will myself give you words, and a wisdom which all your opponents together will be unable to resist or defy.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
You will be betrayed even by your parents and brothers and sisters and relations and friends, and they will cause some of you to be put to death,
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
and you will be hated by every one on account of my Name.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
Yet not a single hair of your heads shall be lost!
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
By your endurance you shall win yourselves Life.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
As soon, however, as you see Jerusalem surrounded by armed camps, then you may know that the hour of her desecration is at hand.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then those of you who are in Judea must take refuge in the mountains, those who are in Jerusalem must leave at once, and those who are in the country places must not go into it.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
For these are to be the Days of Vengeance, when all that Scripture says will be fulfilled.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
Alas for the women that are with child, and for those that are nursing infants in those days! For there will be great suffering in the land, and anger against this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
They will fall by the edge of the sword, and will be taken prisoners to every land, and ‘Jerusalem will be under the heel of the Gentiles,’ until their day is over — as it shall be.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
There will be signs, too, in the sun and moon and stars, and on the earth despair among the nations, in their dismay at the roar of the sea and the surge.
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
Men’s hearts will fail them through dread of what is coming upon the world; for ‘the forces of the heavens will be convulsed.’
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
Then will be seen the ‘Son of Man coming in a cloud’ with power and great glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
And, when these things begin to occur, look upwards and lift your heads, for your deliverance will be at hand.”
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
Then he taught them a lesson thus — “Look at the fig tree and all the other trees.
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
As soon as they shoot, you know, as you look at them, without being told, that summer is near.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
And so may you, as soon as you see these things happening, know that the Kingdom of God is near.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
I tell you that even the present generation will not pass away till all has taken place.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
The heavens and the earth will pass away, but my words will never pass away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
Be on your guard lest your minds should ever be dulled by debauches or drunkenness or the anxieties of life, and lest ‘That Day’ should come suddenly upon you, like a snare.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
For come it will upon all who are living upon the face of the whole earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Be on the watch at all times, and pray that you may have strength to escape all that is destined to happen, and to stand in the presence of the Son of Man.”
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
During the days, Jesus continued to teach in the Temple Courts, but he went out and spent the nights on the hill called the ‘Mount of Olives.’
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people would get up early in the morning and come to listen to him in the Temple Courts.

< Luka 21 >