< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
[Jesus] looked up [from where he was sitting] and saw rich people putting their gifts into the [offering] boxes [in the Temple courtyard].
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
He also saw a poor widow putting in two [small] copper coins.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
He said [to his disciples], “The truth is that these rich people have a lot of money, [but] they gave [only a small part of it]. But this woman, who is very poor, has put in all the money that she had to pay for the things she needs! So [God considers that] [HYP] this poor widow has put more money into the box than all the others.”
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
Some [of Jesus’ disciples] talked about the Temple. [They commented about] the beautiful stones [used in building the Temple] and the other decorations that [people] had given, decorations [that were on the walls]. But he said,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
“[I want to tell you something about] these things that you are looking at. [They will be destroyed] {[Foreign invaders will] destroy [these buildings]} [completely]. Every stone [in these buildings] will be thrown down {They will throw down every stone in these buildings}. Not one stone will be left {They will not leave one stone} on top of another.”
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
[Later] his disciples asked him, “Teacher, when will that happen? What will happen [to the temple] to indicate that the things [you(sg) just told us] are about to happen?”
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
He said, “[All that I will say is], be sure that you are not deceived {that they do not deceive [you]} [about these things]! Many [people] will come and say (that I [sent them]/that they have my authority) [MTY]. They will say, ‘I am [the Messiah]!’ They will also [say] ‘It is now the time [when God will begin to rule]!’ Do not follow them [to become their disciples]
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
Also, whenever you hear about wars and riots, do not be terrified. Keep in mind that [God has said that] those things must happen. But [when they happen], it will not mean that [the world] will end right away!”
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then he said to them, “[Groups in various] countries will fight each other, and [various] governments [will also fight] against each other.
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
There will be [big] earthquakes, and in various places there will be famines and plagues. [People will see] things that will terrify them. There will also be unusual things happening in the sky.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
But before all these things happen, [some of] you will be persecuted and arrested {people will persecute some of you and arrest you} [MTY]. [Some of] you will be put {They will put [some of] you} [on trial] in the places where you gather to worship, and [you will be thrown] into prison. You will be put on trial {[They] will put you on trial} in front of high government authorities because you are my [MTY] [disciples].
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
That will be a time for you to tell [them about me].
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
So determine within yourselves not to be worrying before that happens what you will say to defend yourselves,
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
because I will make you wise [HEN] so that you will [know] what to say. As a result, none of your enemies will be able to oppose what you say or (refute you/show that you are wrong).
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
[And there will also be other evil things that will happen]: Even your parents and brothers and [other] relatives and friends [who do not believe in me] will (betray you/help your enemies to seize you). They will kill some of you.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
[In general], most people will [HYP] hate you because [you believe in] me [MTY].
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
But your souls will be absolutely safe [IDM].
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
By enduring [all these things people will do to you], you will preserve your [eternal] life [SYN].”
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
“But when you see that Jerusalem has been surrounded by the armies of [your enemies], you will know that it is time for [this city] to be completely destroyed {[them] to completely destroy [this city]}.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
At that time those [of you] who are in Judea [district] must flee to the [higher] hills. Those who are in this city must leave [quickly]. Those who are in the nearby countryside must not go back into the city [to get any of their possessions before they flee].
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
[You must obey what I tell you] because, in order that all the things that are written [in the Scriptures] will be fulfilled, [God] will very severely punish [the people who stay in this city].
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
[I feel] very sorry for women [in this city] who will be pregnant, and women who will be nursing [their babies] in those days, [because it will be very difficult for them to run away! I] feel sorry [because] the people in this [land] will suffer greatly [MTY] [when God punishes them].
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
Many of them will be killed {Their enemies will kill many of them} with swords. [Others will be captured] and taken {They will capture [others] and take them} to [HYP] [other] countries. Non-Jewish people will trample over Jerusalem until the time [that God has determined for them to rule the city] is ended.”
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
“There will also be strange things that will [happen to] the sun, the moon, and the stars. In [many] nations, [people] will be very frightened, and they will be anxious [when they hear] the ocean roaring and [see huge] waves.
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
People will faint because they will be afraid as they wait for what will happen. [They will be afraid] because the powerful [objects] in the sky will be shaken {shake}.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
Then they will see [me], the one who came from heaven, coming in a cloud powerfully and very gloriously.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
So when these things that [I have just now described] begin to happen, stand up [straight and] be brave, because it will be close to the time when [God] will free you [from all suffering].”
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
[Then] Jesus told his disciples this parable: “Think about the fig tree, and all the [other] trees.
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
As soon as you see their leaves beginning to sprout, you know that summer is near.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
Similarly, when you see these things that [I have just described] happening, you will know that it is almost time for God to [truly] rule as king.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Keep this in mind: All the things that [I have just now described] will happen before all the people who have observed the things that I have done have died.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
[You can be certain that these things] that I have told [you] about will happen. That they will happen is more [certain] than that the earth and sky will continue to exist.”
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
“But be on guard. Do not be getting drunk with carousing or let yourselves be distracted by worries [concerning] your lives [SYN] {or let worries [concerning] your lives [SYN] distract you}. [If you do wrong things like those, you may be suddenly surprised by my return] [MTY], like a trap [suddenly catches an animal in it].
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
[You need to know that my return will surprise] everyone all over the earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
So be ready at all times. Pray that you will be able to endure without being afraid of all these [difficult] things that will happen, so that you will then stand [confidently] before me, the one who came from heaven.”
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
Each day [during that week Jesus] taught the people in the Temple [courtyard in Jerusalem]. But at night he [and his disciples] left [the city] and stayed on Olive [Tree] Hill.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
Early [each] morning many people came to the Temple [courtyard] to listen to him.

< Luka 21 >