< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
And, looking up, he saw the, rich, who were casting their gifts into the treasury, —
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
and he saw a certain poor widow, casting in thither two mites;
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
and he said—Of a truth, I say unto you—This destitute widow, more than they all, hath cast in;
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For, all these, out of their superfluity, have cast in among the gifts, but, she, out of her deficiency, all the living that she had, hath cast in.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
And, certain saying, of the temple—With beautiful stones and offerings, hath it been adorned! he said—
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
As to these things, which ye are looking upon, There will come days, in which there will not be left here, stone upon stone, which will not be taken down.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
And they questioned him, saying—Teacher! when, therefore, will these things be? And, what the sign, when these things shall be about to come to pass?
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And, he, said—Be taking heed ye be not deceived; for, many, will come upon my name, saying—I, am he, —and—The season, hath drawn near! Do not go after them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
But, whensoever ye shall hear of wars and revolutions, be not terrified, —for these things, must needs, come to pass first, but, not immediately, is the end.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then, said he unto them—There will rise up, nation against nation, and kingdom against kingdom;
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
As well great earthquakes, as also, in places, pestilences and famines, will there be, as well objects of terror, as also, from heaven, great signs, will there be.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
And before, all these things, they will thrust upon you their hands, and persecute you, delivering you up into the synagogues and prisons, —when ye have been led away before kings and governors, for the sake of my name;
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
But it shall turn out to you for a witness.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Settle, then, in your hearts, not to be studying beforehand, how to make defense;
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
For, I, will give you a mouth and wisdom, which one-and-all who are setting themselves against, you shall be unable to withstand or gainsay.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
But ye will be delivered up, even by parents, and brethren, and kinsfolk, and friends, and they will put to death some from among you;
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
And ye will be hated by all, because of my name:
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
And, a hair of your head, in nowise shall perish, —
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
By your endurance, shall ye gain your lives for a possession.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
But whensoever ye shall see Jerusalem, encompassed by armies, then, know, that her desolation hath drawn near.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then they who are in Judaea, let them flee into the mountains, and they who are in her midst, let them go forth, —and they who are in the fields, let them not enter into her;
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
For, days of avenging, are, these, for all the things written to be fulfilled.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
Alas! for the women with child, and for them who are giving suck, in those days; for there will be great distress upon the land, and anger against this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
And they will fall by the edge of the sword, and be carried away captive into all the nations, and, Jerusalem, shall be trodden down by the nations, until the seasons of the nations shall be fulfilled [and shall be].
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
And there will he signs in sun, and moon, and stars, and, on the earth, anguish of nations in embarrassment—sea and surge resounding, —
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
Men fainting, from fear and expectation of the things overtaking the inhabited earth. For, the powers of the heavens, will be shaken.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
And, then, will they see the Son of Man—coming in a cloud, with great power and glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
And, when these things are beginning to come to pass, unbend and lift up your heads, because that, your redemption, is drawing near.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And he spake a parable unto them: See the fig-tree, and all the trees, —
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
Whensoever they have already budded, seeing it, of yourselves, ye observe that, already near, is, the summer:
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
Thus, ye also, whensoever ye shall see, these, things coming to pass, observe ye, that, near, is the kingdom of God!
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Verily, I say unto you—In nowise shall this generation pass away, until, all things, shall happen:
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Heaven and earth, will pass away, but, my word, in nowise will pass away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
But be taking heed unto yourselves, lest once your hearts be made heavy—with debauch and drunkenness and anxieties about livelihood, and that day come upon you suddenly,
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
as a snare, —For it will come in by surprise, upon all them that are dwelling on the face of all the earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
But be watching in every season, making supplication, that ye may gain full vigour, to escape all these things that are about to be coming to pass, and to stand before the Son of Man.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
And he was, by day, in the temple, teaching; but, by night, going forth, he was lodging in the mount which is called the Mount of Olives.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And, all the people, were coming at day-break unto him, in the temple, to be hearkening unto him.

< Luka 21 >