< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
And he looked up and saw people casting their offerings into the treasury, and they were rich.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
And he saw a certain poor widow casting in two mites
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
And he said. "Of truth I tell you that this poor widow has put in more than than they all;
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
"for these men have all contributed to the offering out of their surplus, but she, out of her want, contributed all she had to live on."
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
And to some who were about the Temple, how it was adorned with beautiful stones votive offerings, he said,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
"As for what you are looking at, the time is coming when not one stone will be left upon another, that shall not be thrown down."
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
"Teacher, when will this be?" they asked him, "and what shall be the sign that these things are about to happen?"
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
"Take heed," he answered, "that you are not led astray, for many will come in my name, saying, ‘I am he,’ and ‘The time is close at hand.’ Do not go and follow them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
"And when you shall hear of wars and tumults, do not be frightened; for these things must happen first, but the end does not come immediately."
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then he said to them. "Nation shall rise against nation, kingdom against kingdom.
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
"and there shall be great earthquakes, and, in many places, famines and pestilences; and there shall be terror and great portents from heaven.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
"But before all these things happen, they will apprehend you and persecute you and deliver you to the synagogues and to prisons, and bring you before kings and governors for the sake of my name.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
"It shall turn out for a testimony to you.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
"So settle it in your hearts not to prepare a defense beforehand,
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
"for I will give you utterance and a wisdom which none of your adversaries will be able to answer or withstand.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
"You will be betrayed even by parents or brothers and kinsfolk, and friends.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
"Some of you they will put to death. And you shall be hated by all men for the sake of my name.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
"And not a hair on your head shall perish.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
"In your patience you shall purchase your souls.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
"But when you see Jerusalem encompassed with armies, then know that her desolation is at hand.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
"Then let those who are in Judea flee to the mountains; and let those who are in the country enter not in.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
"For these are the days of vengeance and of fulfilment of all that is written.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
"Woe to women with child and to those who are nursing infants in those days! For sore anguish will come upon the land, and wrath upon all his people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
"They shall fall by the edge of the sword, and shall be led captive among the Gentiles, and Jerusalem shall be trampled under foot by the Gentiles, until the appointed times of the Gentiles be fulfilled.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
"And there will be signs in the sun and the moon and the stars; and on the earth distress of nations in perplexity at the roar of the sea and the billows;
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
"men lifeless through fear, and foreboding of that which is about to come upon the habitable earth. For the powers of the heavens shall be shaken,
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
"and then shall they see the Son of man coming in a cloud, with power and great glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
"But when these things begin to come to pass, look up, lift your heads! for your redemption is drawing near."
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And he told them a parable.
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
"Look at the fig tree and all the trees! When they put out their leaves you can see for yourselves that summer is coming.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
"So whenever you see all these things comings to pass, you know that the kingdom of God is near.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
"In solemn truth I tell you that this generation shall not pass away until all this happens.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
"Heaven and earth will pass away, but my words shall never pass away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
"But take heed to yourselves lest your hearts be surcharged with self-indulgence and drunkenness and worldly cares, and that day catches you suddenly like a trap.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
"For it will come upon all the dwellers on the face of the earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
"So be on your guard at all times, praying that you may be worthy to escape these things that shall come to pass, and to take your stand in the presence of the Son of man."
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
And each day he was habitually in the Temple teaching, and at night he used to go out and lodge on the mount called the Olives Orchards.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people used to come him early in the morning in the Temple, to listen to him.

< Luka 21 >