< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
And he looked up, and saw the rich men casting their gifts into the treasury.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
And he saw also a certain poor widow casting in thither two mites.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
And he said, Of a truth I say to you, that this poor widow has cast in more than they all:
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For all these have of their abundance cast in to the offerings of God: but she of her penury has cast in all the living that she had.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
And as some spoke of the temple, how it was adorned with goodly stones and gifts, he said,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
As for these things which you behold, the days will come, in the which there shall not be left one stone on another, that shall not be thrown down.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
And they asked him, saying, Master, but when shall these things be? and what sign will there be when these things shall come to pass?
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And he said, Take heed that you be not deceived: for many shall come in my name, saying, I am Christ; and the time draws near: go you not therefore after them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
But when you shall hear of wars and commotions, be not terrified: for these things must first come to pass; but the end is not by and by.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then said he to them, Nation shall rise against nation, and kingdom against kingdom:
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
And great earthquakes shall be in divers places, and famines, and pestilences; and fearful sights and great signs shall there be from heaven.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
But before all these, they shall lay their hands on you, and persecute you, delivering you up to the synagogues, and into prisons, being brought before kings and rulers for my name’s sake.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
And it shall turn to you for a testimony.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Settle it therefore in your hearts, not to meditate before what you shall answer:
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
For I will give you a mouth and wisdom, which all your adversaries shall not be able to gainsay nor resist.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
And you shall be betrayed both by parents, and brothers, and kinfolks, and friends; and some of you shall they cause to be put to death.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
And you shall be hated of all men for my name’s sake.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
But there shall not an hair of your head perish.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
In your patience possess you your souls.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
And when you shall see Jerusalem compassed with armies, then know that the desolation thereof is near.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then let them which are in Judaea flee to the mountains; and let them which are in the middle of it depart out; and let not them that are in the countries enter thereinto.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
For these be the days of vengeance, that all things which are written may be fulfilled.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
But woe to them that are with child, and to them that give suck, in those days! for there shall be great distress in the land, and wrath on this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
And they shall fall by the edge of the sword, and shall be led away captive into all nations: and Jerusalem shall be trodden down of the Gentiles, until the times of the Gentiles be fulfilled.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
And there shall be signs in the sun, and in the moon, and in the stars; and on the earth distress of nations, with perplexity; the sea and the waves roaring;
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
Men’s hearts failing them for fear, and for looking after those things which are coming on the earth: for the powers of heaven shall be shaken.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
And then shall they see the Son of man coming in a cloud with power and great glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
And when these things begin to come to pass, then look up, and lift up your heads; for your redemption draws near.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And he spoke to them a parable; Behold the fig tree, and all the trees;
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
When they now shoot forth, you see and know of your own selves that summer is now near at hand.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
So likewise you, when you see these things come to pass, know you that the kingdom of God is near at hand.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Truly I say to you, This generation shall not pass away, till all be fulfilled.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Heaven and earth shall pass away: but my words shall not pass away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
And take heed to yourselves, lest at any time your hearts be overcharged with surfeiting, and drunkenness, and cares of this life, and so that day come on you unawares.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
For as a snare shall it come on all them that dwell on the face of the whole earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Watch you therefore, and pray always, that you may be accounted worthy to escape all these things that shall come to pass, and to stand before the Son of man.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
And in the day time he was teaching in the temple; and at night he went out, and stayed in the mount that is called the mount of Olives.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people came early in the morning to him in the temple, for to hear him.

< Luka 21 >