< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
And looking up, He saw the rich casting their gifts into the treasury.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
And He also saw a certain poor widow, casting in thither two mites.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
And He said; Truly I say unto you, That this poor widow cast in more than all.
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For they all of that which abounds unto them cast into the gifts of God: but she out of her scarcity cast in all her living which she had.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
And certain ones speaking concerning the temple, that it was ornamented with beautiful stones and offerings, He said,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
These things which you see, the days will come, in which stone will not be left upon stone, which shall not be thrown down.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
And they asked Him, saying, Teacher, when then shall these things be? and what shall be the sign when these things may be about to come to pass?
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And He said, See that you are not deceived. For many will come in my name, saying, I am He; and The time is at hand: go ye not after them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
And when ye may hear of wars and commotions, be not affrighted: for it behooveth these things first to take place; but the end is not immediately.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then He said to them, Nation shall rise up against nation, and kingdom against kingdom:
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
and there shall be great earthquakes, famines and pestilences in divers places; and there shall be great terrors and signs from heaven.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
And before all of these things, they will lay their hands on you, and persecute you, delivering you into their synagogues and prisons, led before kings and governors on account of my name.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
And it shall come to pass to you for a testimony.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Place it in your hearts, not to premeditate your defense:
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
for I will give to you mouth and wisdom, which all who are opposed to you will not be able to gainsay nor resist.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
And you shall be delivered up also by your parents, and brothers, and relatives, and friends; and they will kill some of you.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
And you shall be hated by all, on account of my name:
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
and not a hair from your head shall perish.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
In your patience gain your souls.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
And when you may see Jerusalem shut up by the armies, then know that her desolation is nigh.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then let those in Judea fly to the mountains; and let those in the midst of it depart out; and let not those in the country come into it.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
Because these are the days of vengeance, to fill up all things which have been written.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
But alas to those in gestation and nursing in those days! For there shall be great distress upon the earth, and wrath to this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
And they shall fall by the edge of the sword, and be led captive into all nations: and Jerusalem shall be trodden down by the Gentiles, until the times of the Gentiles may be fulfilled.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
And there will be signs in the sun and in the moon and in the stars; and commotion of the nations of the earth in their perplexity, the sea and the wave roaring;
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
the souls of men failing from fear, and expectation of those things coming upon the world: for the powers of the heavens will be shaken.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
And then they will see the Son of man coming in a cloud with power and great glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
And these things beginning to take place, straighten up, and lift up your heads; because your redemption is nigh.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And He spoke a parable to them: Behold the fig-tree, and all the trees:
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
when they may already put forth, seeing, know for yourselves that summer is nigh.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
So you also, when you see these things take place, know that the kingdom of God is nigh.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Truly I say unto you, that this race may not pass away, until all these things shall be fulfilled.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
But heaven and earth shall pass away, but my word can not pass away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
But take heed to yourselves, lest your hearts may be burdened with luxury, and drunkenness, and worldly cares, and that day may come on you unanticipated.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
For as a lasso it will come upon all the people who are sitting down upon the face of the whole earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Therefore watch, praying all the time, that you may be counted worthy to escape all these things which are about to come to pass, and to stand before the Son of man.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
And He was teaching in the temple during the days; and during the nights going out, He was lodging in the mountain called Mount of Olives.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people gathered in the temple to hear Him.

< Luka 21 >