< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
And looking around, he saw the wealthy putting their donations into the offertory.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
Then he also saw a certain widow, a pauper, putting in two small brass coins.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
And he said: “Truly, I say to you, that this poor widow has put in more than all the others.
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For all these, out of their abundance, have added to the gifts for God. But she, out of what she needed, has put in all that she had to live on.”
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
And when some of them were saying, about the temple, that it was adorned with excellent stones and gifts, he said,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
“These things that you see, the days will arrive when there will not be left behind stone upon stone, which is not thrown down.”
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
Then they questioned him, saying: “Teacher, when will these things be? And what will be the sign when these things will happen?”
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And he said: “Be cautious, lest you be seduced. For many will come in my name, saying: ‘For I am he,’ and, ‘The time has drawn near.’ And so, do not choose to go after them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
And when you will have heard of battles and seditions, do not be terrified. These things must happen first. But the end is not so soon.”
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then he said to them: “People will rise up against people, and kingdom against kingdom.
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
And there will be great earthquakes in various places, and pestilences, and famines, and terrors from heaven; and there will be great signs.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
But before all these things, they will lay their hands on you and persecute you, handing you over to synagogues and into custody, dragging you before kings and governors, because of my name.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
And this will be an opportunity for you to give testimony.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Therefore, set this in your hearts: that you should not consider in advance how you might respond.
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
For I will give to you a mouth and wisdom, which all your adversaries will not be able to resist or contradict.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
And you will be handed over by your parents, and brothers, and relatives, and friends. And they will bring about the death of some of you.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
And you will be hated by all because of my name.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
And yet, not a hair of your head will perish.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
By your patience, you shall possess your souls.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
Then, when you will have seen Jerusalem encircled by an army, know then that its desolation has drawn near.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then let those who are in Judea flee to the mountains, and those who are in its midst withdraw, and those who are in the countryside not enter into it.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
For these are the days of retribution, so that all things may be fulfilled, which have been written.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
Then woe to those who are pregnant or nursing in those days. For there will be great distress upon the land and great wrath upon this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
And they will fall by the edge of the sword. And they will be led away as captives into all nations. And Jerusalem will be trampled by the Gentiles, until the times of the nations are fulfilled.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
And there will be signs in the sun and the moon and the stars. And there will be, on earth, distress among the Gentiles, out of confusion at the roaring of the sea and of the waves:
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
men withering away out of fear and out of apprehension over the things that will overwhelm the whole world. For the powers of the heavens will be moved.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
And then they will see the Son of man coming on a cloud, with great power and majesty.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
But when these things begin to happen, lift up your heads and look around you, because your redemption draws near.”
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And he told them a comparison: “Take notice of the fig tree and of all the trees.
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
When presently they produce fruit from themselves, you know that summer is near.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
So you also, when you will have seen these things happen, know that the kingdom of God is near.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Amen I say to you, this lineage shall not pass away, until all these things happen.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Heaven and earth shall pass away. But my words shall not pass away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
But be attentive to yourselves, lest perhaps your hearts may be weighed down by self-indulgence and inebriation and the cares of this life. And then that day may overwhelm you suddenly.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
For like a snare it will overwhelm all those who sit upon the face of the entire earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
And so, be vigilant, praying at all times, so that you may be held worthy to escape from all these things, which are in the future, and to stand before the Son of man.”
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
Now in the daytime, he was teaching in the temple. But truly, departing in the evening, he lodged on the mount that is called Olivet.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people arrived in the morning to listen to him in the temple.

< Luka 21 >