< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
And looking up, he saw the men of wealth putting their offerings in the money-box.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
And he saw a certain poor widow putting in a farthing.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
And he said, Truly I say to you, This poor widow has given more than all of them:
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For they gave out of their wealth, having more than enough for themselves: but she, even out of her need, has put in all her living.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
And some were talking about the Temple, how it was made fair with beautiful stones and with offerings, but he said,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
As for these things which you see, the days will come when not one stone will be resting on another, but all will be broken down.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
And they said to him, Master, when will these things be? and what sign will there be when these events are to take place?
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And he said, Take care that you are not tricked: for a number of people will come in my name, saying, I am he; and, The time is near: do not go after them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
And when news of wars and troubled times comes to your ears, have no fear; for these things have to be, but the end will not be now.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then he said to them, Nation will be moved against nation and kingdom against kingdom:
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
There will be great earth-shocks and outbursts of disease in a number of places, and men will be without food; and there will be wonders and great signs from heaven.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
But before all this, they will take you and be very cruel to you, giving you up to the Synagogues and to prisons, taking you before kings and rulers, because of my name.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
And it will be turned to a witness for you.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
So take care not to be troubled before the time comes, about what answers you will give:
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
For I will give you words and wisdom, so that not one of those who are against you will be able to get the better of you, or to put you in the wrong.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
But you will be given up even by your fathers and mothers, your brothers and relations and friends; and some of you will be put to death.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
And you will be hated by all men, because of me.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
But not a hair of your head will come to destruction.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
By going through all these things, you will keep your lives.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
But when you see armies all round about Jerusalem, then be certain that her destruction is near.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then let those who are in Judaea go in flight to the mountains; and those who are in the middle of the town go out; and let not those who are in the country come in.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
For these are the days of punishment, in which all the things in the Writings will be put into effect.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
It will be hard for women who are with child, and for her with a baby at the breast, in those days. For great trouble will come on the land, and wrath on this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
And they will be put to death with the sword, and will be taken as prisoners into all the nations; and Jerusalem will be crushed under the feet of the Gentiles, till the times of the Gentiles are complete.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
And there will be signs in the sun and moon and stars; and on the earth, fear among the nations and doubt because of the loud noise of the sea and the waves;
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
Men's strength will go from them in fear and in waiting for the things which are coming on the earth; for the powers of the heavens will be moved.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
And then they will see the Son of man coming in a cloud, with power and great glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
But when these things come about, let your heads be lifted up, because your salvation is near.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And he made a story for them: See the fig-tree, and all the trees;
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
When they put out their young leaves, you take note of it, and it is clear to you that summer is coming.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
In the same way, when you see these things taking place you may be certain that the kingdom of God is near.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Truly I say to you, This generation will not come to an end till all things are complete.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Heaven and earth will come to an end, but my words will not come to an end.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
But give attention to yourselves, for fear that your hearts become over-full of the pleasures of food and wine, and the cares of this life, and that day may come on you suddenly, and take you as in a net:
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
For so it will come on all those who are living on the face of all the earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
But keep watch at all times with prayer, that you may be strong enough to come through all these things and take your place before the Son of man.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
And every day he was teaching in the Temple and every night he went out to the mountain which is named the Mountain of Olives to take his rest.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people came early in the morning to give ear to his words in the Temple.

< Luka 21 >