< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
I ARI kotilong ong nan kanim Ieriko, ap kotin daulula.
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
A kilang, ol kapwapwa men mia, ad a Sakäus, me saumas en saunopwei kan.
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
A men kilang Iesus, pwen asa, is i, ap sota kak, pweki pokon o, o a sakakair.
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
I ari tiong mo’rail, dauda nin tuka pot, pwen kak kilang i, pwe a pan kotin daulul wasa o.
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
A lao lel wasa o Iesus ap kotin masanda diar i, masani ong i: Sakäus, madang daudi, pwe I pan pedelong ong nan im om ran wet.
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
I ari madang daudi kasamo i pereperen.
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
Irail lao kilanger met, karos ap lipanedeki inda: A pedelonger, pwen kairu ren ol dipan amen.
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
A Sakäus potodo potoan ong Kaun o: Maing re kotin mangi, apali en ai kapwa i pan kisakisaki me samama kan, o ma i kotaue amen, i kin kasapal wong i pan pa pak laude sang.
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
Iesus kotin masani ong i: Maur me pwara dong nan im wet ran wet, pwe a pil nain Apraam amen.
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
Pwe Nain aramas pwara don rapaki o kamaureda me salongalar.
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
A ni ar rongadar mepukat, a pil kotin masani karaseras eu, aki koren iong Ierusalem, o re kiki ong, me wein Kot pan madang sansaleda.
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
A kotin masani: Ol lapalap amen kolang sap doo eu, pwen nine mar a, ap pan puredo.
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
I me eker pena na ladu ek, o ki ong irail paun eisok, indang irail: Komail dodokki, i lao puredo.
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
A na aramas akan kailongki i, kadarala mur i kaireki lang i: Se sota mauki, ol men et en kaun kit.
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
Kadekadeo a lao puredo, murin a aleer wei o, ap ilakelang ladu kan, me a ki ong na moni, pwen asa duen en amen amen ar kalaudelar na moni.
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
Men mas ap pwarado indada: Maing, omui paun kareda paun eisok.
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
A indang i: Meid pai ladu mau koe, aki om apapwali mau me tikitik, koe pan id kaunda kanim eisok.
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
O kariamen ap pwarado indada: Maing, omui paun me kareda paun limau.
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
A pil indang i: Koe pan kaunda kanim limau.
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
O pil amen pwarado indada: Maing, mangi, ietet sapwilim omui paun, me i nekidala nan lim en pudo.
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
Pwe i masak komui, pwe ol petik amen komui. Komui kin aleda, me kaidin komui kidier, o dolung sang, me kaidin komui padukedier.
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
A indang i: Sang nan au om i pan kadeik kin uk ada ladu sued koe. Koe asaer, me ol petik amen ngai, me kin ale, me kaidin ngai kidier o dolung sang, me kaidin ngai padukidier.
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
Menda koe sota wala nai moni wasan kanaitik, o i lao puredo, i pan ale me udan ai iangaki moni naitik.
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
A indai ong irail me u impa: Ale sang i paun o, ki ong ren me a paun eisok!
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
Irail indai ong i: Maing, nan a nainekier paun eisok.
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
Pwe I indai ong komail, meamen, me a mia, ekis pan ko ong, a me sota a mia, nan a pwitikatik pil pan katia sang.
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
A ir, ai imwintiti, me kang, i en kakaun ir, wa ir do, o kame ir ala mo i!
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
A lao kotin kaimwisokala a masan pukat, ap kotiwei kotidala Ierusalem.
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
Kadekadeo a lao koti dong Petpake o Petanien impan dol me ad a Oliwe, ap kotin poronela sapwilim a tounpadak riamen,
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
Masani: Koma ko ong nan kanim monen, koma lao pedelong, koma pan diarada esel pul amen salidi, me aramas amen saik mondi poa. Lapwada i, ap karedo!
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
A ma meamen pan idok re oma: Da me koma lapwa kida i? Koma ap pan inda: Kaun o men dake.
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
A ira me pakadara wei, ap kola o diarada, duen a kotin masani ong ira.
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
A ni ara lawada esel pul o, ol oko, me naineki, ap indang ira: Da me koma lawa kida esel pul en?
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
Ira ap indada: Kaun o men dake.
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
Ira ari wado ren Iesus, ap irepadi pon esel pul arail likau kan ap potoan dang Iesus poa.
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
Ni a kotikot kokowei, irail ap irepakidi arail likau kan nani al.
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
A lao kotin korendor kotidila dol Oliwe tounpadak kan karos ap wiaki eu ngil laudeda kapinga Kot, pweki manaman akan karos, me re kilanger,
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
Indada: Kapinga ong Nanmarki, me kotido ni mar en Kaun! Nanlang en popol o lingan wasa ileile!
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
A Parisär kai kisan pokon o indai ong i: Saunpadak, kotin kidaue sapwilim omui tounpadak kan.
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
I ari kotin sapeng masani ong irail: I indai ong komail, ma mepukat pan nenenla, takai pan id kadededa.
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
A lao kotin korendor, ap masani kanim o, ap tontonireki,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
Masani: O i men, koe en dedeki om ran mau wet, me pan kare ong uk popol: Ari, a rir sanger mon mas om.
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
Pwe ran apwal ko pan lel ong uk, me om imwintiti pan kele kin uk pena o it pena sang ni pali karos;
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
O irail pan kase uk ala iangaki noum seri kan, o re pan karongk uk ala; sota eu takai pan mimieta pon eu, pweki om sota dedeki ansaun om kasosong.
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
I ari kotilong ong nan im en kaudok, ap sikon sang me netinet lole,
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
Masani ong ir: Nan a intingidier: Im ai im en kapakap, a komail wiaki deun lolap akan.
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
I ari kotin kaukawewe nan im en kaudok ran karos. A samero lapalap, o saunkawewe, o me lapalap akan ren aramas raparapaki, en kamatala i.
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
A re sota kak diar, me ren wiada, pwe aramas karos apwali i kaualap o men rong i.

< Luka 19 >