< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
Et il entra dans Jéricho, et traversa [la ville].
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
Et voici, un homme, appelé du nom de Zachée: et il était chef de publicains, et il était riche;
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
et il cherchait à voir Jésus, quel il était; et il ne pouvait, à cause de la foule, car il était petit de taille.
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
Et, courant en avant, il monta sur un sycomore pour le voir; car il allait passer là.
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
Et quand il fut venu à cet endroit, Jésus, regardant, le vit, et lui dit: Zachée, descends vite; car il faut que je demeure aujourd’hui dans ta maison.
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
Et il descendit à la hâte, et le reçut avec joie.
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
Et voyant cela, tous murmuraient, disant qu’il était entré chez un pécheur pour y loger.
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
Et Zachée, se tenant là, dit au Seigneur: Voici, Seigneur, je donne la moitié de mes biens aux pauvres; et si j’ai fait tort à quelqu’un par une fausse accusation, je lui rends le quadruple.
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
Et Jésus lui dit: Aujourd’hui [le] salut est venu à cette maison, vu que lui aussi est fils d’Abraham;
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
car le fils de l’homme est venu chercher et sauver ce qui était perdu.
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
Et comme ils entendaient ces choses, il ajouta et [leur] dit une parabole, parce qu’il était près de Jérusalem, et qu’ils pensaient que le royaume de Dieu allait immédiatement paraître.
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
Il dit donc: Un homme noble s’en alla dans un pays éloigné, pour recevoir un royaume et revenir.
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
Et ayant appelé dix de ses propres esclaves, il leur donna dix mines, et leur dit: Trafiquez jusqu’à ce que je vienne.
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
Or ses concitoyens le haïssaient; et ils envoyèrent après lui une ambassade, disant: Nous ne voulons pas que celui-ci règne sur nous.
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
Et il arriva, à son retour, après qu’il eut reçu le royaume, qu’il commanda d’appeler auprès de lui ces esclaves auxquels il avait donné l’argent, afin de savoir combien chacun aurait gagné par son trafic.
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
Et le premier se présenta, disant: Maître, ta mine a produit dix mines.
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
Et il lui dit: Bien, bon esclave, parce que tu as été fidèle en ce qui est très peu de chose, aie autorité sur dix villes.
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
Et le second vint, disant: Maître, ta mine a produit cinq mines.
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
Et il dit aussi à celui-ci: Et toi, sois [établi] sur cinq villes.
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
Et un autre vint, disant: Maître, voici ta mine, que j’ai gardée déposée dans un linge;
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
car je t’ai craint, parce que tu es un homme sévère: tu prends ce que tu n’as pas mis, et tu moissonnes ce que tu n’as pas semé.
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
Il lui dit: Je te jugerai par ta propre parole, méchant esclave: tu savais que moi je suis un homme sévère, prenant ce que je n’ai pas mis et moissonnant ce que je n’ai pas semé;
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
et pourquoi n’as-tu pas mis mon argent à la banque, et quand je serais venu je l’aurais retiré avec l’intérêt?
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
Et il dit à ceux qui étaient présents: Ôtez-lui la mine et donnez-la à celui qui a les dix mines.
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
– Et ils lui dirent: Seigneur, il a dix mines.
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
– Car je vous dis qu’à quiconque a, il sera donné; et à celui qui n’a pas, cela même qu’il a lui sera ôté.
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
Mais ceux-là, mes ennemis, qui n’ont pas voulu que je règne sur eux, amenez-les ici et tuez-les devant moi.
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
Et ayant dit ces choses, il allait devant eux, montant à Jérusalem.
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
Et il arriva, comme il approchait de Bethphagé et de Béthanie, vers la montagne appelée des Oliviers, qu’il envoya deux de ses disciples,
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
disant: Allez au village qui est vis-à-vis; et y étant entrés, vous trouverez un ânon attaché, sur lequel jamais aucun homme ne s’assit; détachez-le, et amenez-le.
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
Et si quelqu’un vous demande pourquoi vous le détachez, vous lui direz ainsi: Le Seigneur en a besoin.
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
Et ceux qui étaient envoyés, s’en allant, trouvèrent [tout] comme il le leur avait dit.
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
Et comme ils détachaient l’ânon, les maîtres de celui-ci leur dirent: Pourquoi détachez-vous l’ânon?
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
Et ils dirent: Parce que le Seigneur en a besoin.
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
Et ils l’amenèrent à Jésus; et ayant jeté leurs vêtements sur l’ânon, ils mirent Jésus dessus.
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
Et comme il allait son chemin, ils étendaient leurs vêtements sur le chemin.
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
Et comme il approchait déjà, à la descente de la montagne des Oliviers, toute la multitude des disciples, se réjouissant, se mit à louer Dieu à haute voix pour tous les miracles qu’ils avaient vus,
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
disant: Béni soit le roi qui vient au nom du Seigneur! Paix au ciel, et gloire dans les lieux très hauts!
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
Et quelques-uns des pharisiens lui dirent du milieu de la foule: Maître, reprends tes disciples.
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
Et répondant, il leur dit: Je vous dis que si ceux-ci se taisent, les pierres crieront.
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
Et quand il fut proche, voyant la ville, il pleura sur elle,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
disant: Si tu avais connu, toi aussi, au moins en cette tienne journée, les choses qui appartiennent à ta paix! mais maintenant elles sont cachées devant tes yeux.
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
Car des jours viendront sur toi, où tes ennemis t’entoureront de tranchées, et t’environneront, et te serreront de tous côtés,
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
et te renverseront par terre, toi et tes enfants au-dedans de toi; et ils ne laisseront pas en toi pierre sur pierre, parce que tu n’as point connu le temps de ta visitation.
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
Et il entra au temple, et se mit à chasser dehors ceux qui y vendaient et qui y achetaient,
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
leur disant: Il est écrit: « Ma maison est une maison de prière »; mais vous, vous en avez fait une caverne de voleurs.
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
Et il enseignait tous les jours dans le temple; et les principaux sacrificateurs et les scribes, et les principaux du peuple, tâchaient de le faire mourir.
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
Et ils ne trouvaient rien qu’ils puissent faire; car tout le peuple se tenait suspendu à ses lèvres pour l’entendre.

< Luka 19 >