< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
Jesus entered Jericho and made his way through the town.
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
There was a man there, known by the name of Zacchaeus, who was a senior tax collector and a rich man.
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
He tried to see what Jesus was like; but, being short, he was unable to do so because of the crowd.
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
So he ran on ahead and climbed into a mulberry tree to see Jesus, for he knew that he must pass that way.
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
When Jesus came to the place, he looked up and said to him, ‘Zacchaeus, be quick and come down, for I must stop at your house today.’
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
So Zacchaeus got down quickly, and joyfully welcomed him.
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
On seeing this, everyone began to complain, ‘He has gone to stay with a man who is an outcast.’
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
But Zacchaeus stood forward and said to the Master, ‘Listen, Master! I will give half my property to the poor, and, if I have defrauded anyone of anything, I will give him back four times as much.’
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
‘Salvation has come to this house today,’ answered Jesus, ‘for even this man is a son of Abraham.
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
The Son of Man has come to search for those who are lost and to save them.’
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
As the people were listening to this, Jesus went on to tell them a parable. He did so because he was near Jerusalem, and because they thought that the kingdom of God was going to be proclaimed at once.
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
He said, ‘A nobleman once went to a distant country to receive his appointment to a kingdom and then return.
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
He called ten of his servants and gave them ten pounds of silver each, and told them to trade with them during his absence.
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
But his subjects hated him and sent envoys after him to say “We will not have this man as our king.”
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
On his return, after having been appointed king, he directed that the servants to whom he had given his money should be summoned, so that he might learn what amount of trade they had done.
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
The first came up, and said “Sir, your ten pounds have made a hundred.”
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
“Well done, good servant!” exclaimed the master. “As you have proved trustworthy in a very small matter, I appoint you governor over ten towns.”
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
When the second came, he said “Your ten pounds, Sir, have produced fifty.”
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
So the master said to him “And you I appoint over five towns.”
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
Another servant also came and said “Sir, here are your ten pounds; I have kept them put away in a handkerchief.
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
For I was afraid of you, because you are a stern man. You take what you have not planted, and reap what you have not sown.”
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
The master answered “Out of your own mouth I judge you, you worthless servant. You knew that I am a stern man, that I take what I have not planted, and reap what I have not sown?
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
Then why didn’t you put my money into a bank? And I, on my return, could have claimed it with interest.
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
Take away from him the ten pounds,” he said to those standing by, “and give them to the one who has the hundred.”
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
“But, Sir,” they said, “he has a hundred pounds already!”
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
“I tell you,” he answered, “that, to him who has, more will be given, but, from him who has nothing, even what he has will be taken away.
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
But as for my enemies, these men who would not have me as their king, bring them here and put them to death in my presence.”’
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
After saying this, Jesus went on in front, going up to Jerusalem.
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
It was when Jesus had almost reached Bethphage and Bethany, near the Mount of Olives, that he sent on two of the disciples.
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
‘Go to the village facing us,’ he said, ‘and, when you get there, you will find a foal tethered, which no one has yet ridden; untie it and lead it here.
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
And, if anybody asks you “Why are you untying it?”, you are to say this – “The Master wants it.”’
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
So the two who were sent went and found it as Jesus had told them.
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
While they were untying the foal, the owners asked them – ‘Why are you untying the foal?’
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
And the two disciples answered – ‘The Master wants it.’
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
Then they led it back to Jesus, and threw their cloaks on the foal and put Jesus on it.
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
As he went along, the people kept spreading their cloaks in the road.
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
When he had almost reached the place where the road led down the Mount of Olives, everyone of the many disciples began in their joy to praise God loudly for all the miracles that they had seen:
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
‘Blessed is He who comes – our king – in the name of the Lord! Peace in heaven, and glory on high.’
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
Some of the Pharisees in the crowd said to him, ‘Teacher, restrain your disciples.’
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
But Jesus answered, ‘I tell you that if they are silent, the stones will call out.’
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
When he drew near, on seeing the city, he wept over it, and said,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
‘If only you had known, while yet there was time – even you – the things that make for peace! But now they have been hidden from your sight.
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
For a time is coming when your enemies will surround you with earthworks, and encircle you, and hem you in on all sides;
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
they will trample you down and your children within you, and they will not leave in you one stone on another, because you did not know the time of your visitation.’
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
Jesus went into the Temple Courts and began to drive out those who were selling,
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
saying as he did so, ‘Scripture says – “My house will be a house of prayer”; but you have made it a den of robbers.’
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
Jesus continued to teach each day in the Temple Courts; but the chief priests and teachers of the Law were eager to take his life, and so also were the leaders of the people.
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
Yet they could not see what to do, for the people all hung on his words.

< Luka 19 >