< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
And Yahushua entered and passed through Jericho.
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
And, behold, there was a man named Zacchehu, which was the chief among the publicans, and he was rich.
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
And he sought to see Yahushua who he was; and could not for the press, because he was little of stature.
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
And he ran before, and climbed up into a sycomore tree to see him: for he was to pass that way.
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
And when Yahushua came to the place, he looked up, and saw him, and said unto him, Zacchehu, make haste, and come down; for to day I must abide at thy house.
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
And he made haste, and came down, and received him joyfully.
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
And when they saw it, they all murmured, saying, That he was gone to be guest with a man that is a sinner.
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
And Zacchehu stood, and said unto Yahushua; Behold, Rabbi, the half of my goods I give to the poor; and if I have taken any thing from any man by false accusation, I restore him fourfold.
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
And Yahushua said unto him, This day is salvation come to this house, forsomuch as he also is a son of Abraham.
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
For the Son of man is come to seek and to save that which was lost.
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
And as they heard these things, he added and spake a parable, because he was nigh to Jerusalem, and because they thought that the kingdom of YHWH should immediately appear.
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
He said therefore, A certain nobleman went into a far country to receive for himself a kingdom, and to return.
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
And he called his ten servants, and delivered them ten pounds, and said unto them, Occupy till I come.
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
But his citizens hated him, and sent a message after him, saying, We will not have this man to reign over us.
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
And it came to pass, that when he was returned, having received the kingdom, then he commanded these servants to be called unto him, to whom he had given the money, that he might know how much every man had gained by trading.
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
Then came the first, saying, Master, thy pound hath gained ten pounds.
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
And he said unto him, Well, thou good servant: because thou hast been faithful in a very little, have thou authority over ten cities.
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
And the second came, saying, Master, thy pound hath gained five pounds.
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
And he said likewise to him, Be thou also over five cities.
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
And another came, saying, Master, behold, here is thy pound, which I have kept laid up in a napkin:
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
For I feared thee, because thou art an austere man: thou takest up that thou layedst not down, and reapest that thou didst not sow.
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
And he saith unto him, Out of thine own mouth will I judge thee, thou wicked servant. Thou knewest that I was an austere man, taking up that I laid not down, and reaping that I did not sow:
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
Wherefore then gavest not thou my money into the bank, that at my coming I might have required mine own with usury?
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
And he said unto them that stood by, Take from him the pound, and give it to him that hath ten pounds.
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
( And they said unto him, Master, he hath ten pounds.)
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
For I say unto you, That unto every one which hath shall be given; and from him that hath not, even that he hath shall be taken away from him.
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
But those mine enemies, which would not that I should reign over them, bring hither, and slay them before me.
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
And when he had thus spoken, he went before, ascending up to Jerusalem.
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
And it came to pass, when he was come nigh to Bethphage and Bethany, at the mount called the mount of Olives, he sent two of his disciples,
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
Saying, Go ye into the village over against you; in the which at your entering ye shall find a colt tied, whereon yet never man sat: loose him, and bring him hither.
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
And if any man ask you, Why do ye loose him? thus shall ye say unto him, Because the Rabbi hath need of him.
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
And they that were sent went their way, and found even as he had said unto them.
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
And as they were loosing the colt, the owners thereof said unto them, Why loose ye the colt?
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
And they said, the Rabbi hath need of him.
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
And they brought him to Yahushua: and they cast their garments upon the colt, and they set Yahushua thereon.
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
And as he went, they spread their clothes in the way.
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
And when he was come nigh, even now at the descent of the mount of Olives, the whole multitude of the disciples began to rejoice and praise YHWH with a loud voice for all the mighty works that they had seen;
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
Saying, Blessed be the King that cometh in the name of YHWH: peace in heaven, and glory in the highest.
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
And some of the Pharisees from among the multitude said unto him, Master, rebuke thy disciples.
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
And he answered and said unto them, I tell you that, if these should hold their peace, the stones would immediately cry out.
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
And when he was come near, he beheld the city, and wept over it,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
Saying, If thou hadst known, even thou, at least in this thy day, the things which belong unto thy peace! but now they are hid from thine eyes.
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
For the days shall come upon thee, that thine enemies shall cast a trench about thee, and compass thee round, and keep thee in on every side,
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
And shall lay thee even with the ground, and thy children within thee; and they shall not leave in thee one stone upon another; because thou knewest not the time of thy visitation.
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
And he went into the temple, and began to cast out them that sold therein, and them that bought;
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
Saying unto them, It is written, My house is the house of prayer: but ye have made it a den of thieves.
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
And he taught daily in the temple. But the chief priests and the scribes and the chief of the people sought to destroy him,
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
And could not find what they might do: for all the people were very attentive to hear him.

< Luka 19 >