< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
耶穌進了耶利哥,正經過的時候,
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
有一個人名叫撒該,作稅吏長,是個財主。
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
他要看看耶穌是怎樣的人;只因人多,他的身量又矮,所以不得看見,
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
就跑到前頭,爬上桑樹,要看耶穌,因為耶穌必從那裏經過。
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
耶穌到了那裏,抬頭一看,對他說:「撒該,快下來!今天我必住在你家裏。」
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
他就急忙下來,歡歡喜喜地接待耶穌。
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
眾人看見,都私下議論說:「他竟到罪人家裏去住宿。」
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
撒該站着對主說:「主啊,我把所有的一半給窮人;我若訛詐了誰,就還他四倍。」
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
耶穌說:「今天救恩到了這家,因為他也是亞伯拉罕的子孫。
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
人子來,為要尋找、拯救失喪的人。」
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
眾人正在聽見這些話的時候,耶穌因為將近耶路撒冷,又因他們以為上帝的國快要顯出來,就另設一個比喻,說:
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
「有一個貴冑往遠方去,要得國回來,
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
便叫了他的十個僕人來,交給他們十錠銀子,說:『你們去做生意,直等我回來。』
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
他本國的人卻恨他,打發使者隨後去,說:『我們不願意這個人作我們的王。』
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
他既得國回來,就吩咐叫那領銀子的僕人來,要知道他們做生意賺了多少。
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
頭一個上來,說:『主啊,你的一錠銀子已經賺了十錠。』
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
主人說:『好!良善的僕人,你既在最小的事上有忠心,可以有權柄管十座城。』
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
第二個來,說:『主啊, 你的一錠銀子已經賺了五錠。』
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
主人說:『你也可以管五座城。』
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
又有一個來說:『主啊,看哪,你的一錠銀子在這裏,我把它包在手巾裏存着。
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
我原是怕你,因為你是嚴厲的人;沒有放下的,還要去拿, 沒有種下的,還要去收。』
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
主人對他說:『你這惡僕,我要憑你的口定你的罪。你既知道我是嚴厲的人,沒有放下的,還要去拿,沒有種下的,還要去收,
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
為甚麼不把我的銀子交給銀行,等我來的時候,連本帶利都可以要回來呢?』
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
就對旁邊站着的人說:『奪過他這一錠來,給那有十錠的。』
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
他們說:『主啊,他已經有十錠了。』
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
主人說:『我告訴你們,凡有的,還要加給他;沒有的,連他所有的也要奪過來。
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
至於我那些仇敵,不要我作他們王的,把他們拉來,在我面前殺了吧!』」
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
耶穌說完了這話,就在前面走,上耶路撒冷去。
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
將近伯法其和伯大尼,在一座山名叫橄欖山那裏,就打發兩個門徒,說:
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
「你們往對面村子裏去,進去的時候,必看見一匹驢駒拴在那裏,是從來沒有人騎過的,可以解開牽來。
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
若有人問為甚麼解牠,你們就說:『主要用牠。』」
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
打發的人去了,所遇見的正如耶穌所說的。
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
他們解驢駒的時候,主人問他們說:「解驢駒做甚麼?」
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
他們說:「主要用牠。」
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
他們牽到耶穌那裏,把自己的衣服搭在上面,扶着耶穌騎上。
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
走的時候,眾人把衣服鋪在路上。
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
將近耶路撒冷,正下橄欖山的時候,眾門徒因所見過的一切異能,都歡樂起來,大聲讚美上帝,
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
說: 奉主名來的王是應當稱頌的! 在天上有和平; 在至高之處有榮光。
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
眾人中有幾個法利賽人對耶穌說:「夫子,責備你的門徒吧!」
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
耶穌說:「我告訴你們,若是他們閉口不說,這些石頭必要呼叫起來。」
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
耶穌快到耶路撒冷,看見城,就為它哀哭,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
說:「巴不得你在這日子知道關係你平安的事;無奈這事現在是隱藏的,叫你的眼看不出來。
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
因為日子將到,你的仇敵必築起土壘,周圍環繞你,四面困住你,
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
並要掃滅你和你裏頭的兒女,連一塊石頭也不留在石頭上,因你不知道眷顧你的時候。」
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
耶穌進了殿,趕出裏頭做買賣的人,
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
對他們說:「經上說: 我的殿必作禱告的殿, 你們倒使它成為賊窩了。」
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
耶穌天天在殿裏教訓人。祭司長和文士與百姓的尊長都想要殺他,
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
但尋不出法子來,因為百姓都側耳聽他。

< Luka 19 >