< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
耶稣进了耶利哥,正经过的时候,
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
有一个人名叫撒该,作税吏长,是个财主。
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
他要看看耶稣是怎样的人;只因人多,他的身量又矮,所以不得看见,
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
就跑到前头,爬上桑树,要看耶稣,因为耶稣必从那里经过。
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
耶稣到了那里,抬头一看,对他说:“撒该,快下来!今天我必住在你家里。”
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
他就急忙下来,欢欢喜喜地接待耶稣。
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
众人看见,都私下议论说:“他竟到罪人家里去住宿。”
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
撒该站着对主说:“主啊,我把所有的一半给穷人;我若讹诈了谁,就还他四倍。”
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
耶稣说:“今天救恩到了这家,因为他也是亚伯拉罕的子孙。
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
人子来,为要寻找、拯救失丧的人。”
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
众人正在听见这些话的时候,耶稣因为将近耶路撒冷,又因他们以为 神的国快要显出来,就另设一个比喻,说:
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
“有一个贵胄往远方去,要得国回来,
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
便叫了他的十个仆人来,交给他们十锭银子,说:‘你们去做生意,直等我回来。’
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
他本国的人却恨他,打发使者随后去,说:‘我们不愿意这个人作我们的王。’
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
他既得国回来,就吩咐叫那领银子的仆人来,要知道他们做生意赚了多少。
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
头一个上来,说:‘主啊,你的一锭银子已经赚了十锭。’
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
主人说:‘好!良善的仆人,你既在最小的事上有忠心,可以有权柄管十座城。’
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
第二个来,说:‘主啊,你的一锭银子已经赚了五锭。’
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
主人说:‘你也可以管五座城。’
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
又有一个来说:‘主啊,看哪,你的一锭银子在这里,我把它包在手巾里存着。
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
我原是怕你,因为你是严厉的人;没有放下的,还要去拿,没有种下的,还要去收。’
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
主人对他说:‘你这恶仆,我要凭你的口定你的罪。你既知道我是严厉的人,没有放下的,还要去拿,没有种下的,还要去收,
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
为什么不把我的银子交给银行,等我来的时候,连本带利都可以要回来呢?’
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
就对旁边站着的人说:‘夺过他这一锭来,给那有十锭的。’
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
他们说:‘主啊,他已经有十锭了。’
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
主人说:‘我告诉你们,凡有的,还要加给他;没有的,连他所有的也要夺过来。
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
至于我那些仇敌,不要我作他们王的,把他们拉来,在我面前杀了吧!’”
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
耶稣说完了这话,就在前面走,上耶路撒冷去。
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
将近伯法其和伯大尼,在一座山名叫橄榄山那里,就打发两个门徒,说:
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
“你们往对面村子里去,进去的时候,必看见一匹驴驹拴在那里,是从来没有人骑过的,可以解开牵来。
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
若有人问为什么解它,你们就说:‘主要用它。’”
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
打发的人去了,所遇见的正如耶稣所说的。
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
他们解驴驹的时候,主人问他们说:“解驴驹做什么?”
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
他们说:“主要用它。”
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
他们牵到耶稣那里,把自己的衣服搭在上面,扶着耶稣骑上。
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
走的时候,众人把衣服铺在路上。
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
将近耶路撒冷,正下橄榄山的时候,众门徒因所见过的一切异能,都欢乐起来,大声赞美 神,
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
说: 奉主名来的王是应当称颂的! 在天上有和平; 在至高之处有荣光。
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
众人中有几个法利赛人对耶稣说:“夫子,责备你的门徒吧!”
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
耶稣说:“我告诉你们,若是他们闭口不说,这些石头必要呼叫起来。”
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
耶稣快到耶路撒冷,看见城,就为它哀哭,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
说:“巴不得你在这日子知道关系你平安的事;无奈这事现在是隐藏的,叫你的眼看不出来。
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
因为日子将到,你的仇敌必筑起土垒,周围环绕你,四面困住你,
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
并要扫灭你和你里头的儿女,连一块石头也不留在石头上,因你不知道眷顾你的时候。”
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
耶稣进了殿,赶出里头做买卖的人,
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
对他们说:“经上说: 我的殿必作祷告的殿, 你们倒使它成为贼窝了。”
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
耶稣天天在殿里教训人。祭司长和文士与百姓的尊长都想要杀他,
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
但寻不出法子来,因为百姓都侧耳听他。

< Luka 19 >