< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
耶稣走进耶利哥城,穿城而过。
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
有一个名叫撒该的税吏长,非常富有。
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
他想看看耶稣到底是谁,但在人群中,身材矮小的他无法看见。
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
于是他跑到前面,爬上一棵无花果树,想在耶稣经过的时候看看他的样子。
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
耶稣走到这里后往上一看,对他说:“撒该,快下来,今天我要住在你家中。”
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
撒该马上爬下来,高兴地迎接耶稣到他家去。
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
众人见状议论纷纷:“他竟要住在这样的罪人家中!”
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
撒该站着对主说:“主啊,你看,我正在把一半的家财分给穷人,如果我曾欺骗谁,就会四倍奉还!”
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
耶稣说:“今天这栋房子迎来了救赎,他也是亚伯拉罕的子孙。
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
因为人子来寻找和拯救的就是迷失之人。”
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
众人专心听着耶稣的话。由于这里接近耶路撒冷,加上民众都认为上帝之国即将出现,于是耶稣就讲了一个故事。
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
他说:“从前有一个贵族,他离开家去远方接受王位加冕,然后再回到家。
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
他叫了自己的十个仆人来,将钱平分给他们,然后说:‘你们用这钱去做投资,一直到我回来。’
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
但这国家的人都憎恨他,于是派一个代表跟过去,说:‘我们不想这个人做王统治我们。’
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
贵族获得王位后返回,然后将那些拿钱投资的仆人召来,询问他们做投资的收益情况。
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
第一个仆人上前说:‘主人,你的钱已经赚了十倍。’
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
国王说:‘做得好,你是个好仆人,因为你证明了在小事上很忠心,我现在派你去管理十座城。’
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
第二个过来说:‘主人,你的钱已经赚了五倍。’
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
国王说:‘我派你去管理五座城。’
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
另一个仆人走进来说:‘主啊,你看,这是你的钱,现在还给你。我用布包着它,确保安全。
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
你是个严厉的人,我很害怕你。我怕你会拿走不属于你的东西,会收走你没有种下的作物。’
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
国王回答:‘我要根据你这番话来审判你。你知道我很严厉,会拿走不属于我的东西,会收走我没有种下的作物。
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
那你为什么不把我的钱存入银行,等我回来的时候,就可以连本带息取回来?’
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
国王对身边站着的仆人说:‘把他的钱拿走,交给那赚了十倍的人。’
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
侍卫说:‘但主人,他已经有了十倍的钱了。’
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
国王说:‘告诉你们吧,那些已经有的,还会有更多。没有的,现在有的也会被拿走。
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
至于那些不愿意我做国王统治他们的敌人,现在把他们拉到这里来,当着我的面杀掉!’”
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
耶稣讲完这个故事,就继续向前朝着耶路撒冷走去。
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
快到伯法其和伯大尼时,他来到了橄榄山,在那里叫来两名门徒,对他们说:
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
“你们到前面的村子去,进去后会看见有一个地方拴着一头从未有人骑过的小驴,解开它的绳子,把它牵来。
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
如果有人问为什么解开它,你们就说:‘主需要它。’”
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
两名门徒出发了,后来发生的一切与耶稣所说如出一辙。
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
他们解开小驴的时候,驴主人问:“你们为什么解开它?”
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
他们说:“主需要它。”
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
门徒把小驴牵到耶稣那里,把自己的衣服搭在驴背上,耶稣坐在上面。
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
耶稣骑驴前行,众人把自己的衣服铺在路上。
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
当他走近耶路撒冷,这里也是橄榄山的下山路,门徒们因为看见了所有神迹,开始充满喜悦地大声赞美上帝。
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
他们大声喊:“奉主之名前来的王,赞颂你!愿和平降临天堂,愿荣耀降临至高天堂!”
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
民众中有几个法利赛人对他说:“老师,不要让你的门徒说这些!”
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
耶稣说:“我告诉你们,他们若保持沉默,石头就要呼喊了!”
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
耶路撒冷越来越近了,耶稣看见这座城,开始为之哭泣,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
他说:“我真希望你们——就是你们啊,在今天能知道通往平安的路,但都隐藏起来了,你们看不到。
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
时间一到,你们的仇敌就会包围过来,搭建斜坡攻击你们,把你们团团围住,困住你们,
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
他们会彻底摧毁你们,还有你们的孩子。所有的石头建筑都会轰然倒塌,因为你们在救赎到来之刻拒绝接受。”
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
耶稣走进神庙,赶走做买卖之人,
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
他对他们说:“经文上记着:‘我的殿将用于祷告’。你们却把它变成贼窝了。”
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
然后他每天都在神庙里教导众人。祭司长、宗教老师和首领都想杀害他,
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
但又不知道如何下手,因为众人都围着他并聆听。

< Luka 19 >