< Luka 18 >

1 Kisha akawaambia mfano wa namna wanavyopaswa kuomba daima, na wasikate tamaa.
And he spoke also a parable to them to the purport that they should always pray and not faint,
2 akaisema, 'Kulikuwa na hakimu katika mji fulani, ambaye hakuwa anamwogopa Mungu na hakuwaheshimu watu.
saying, There was a judge in a city, not fearing God and not respecting man:
3 Kulikuwa na mjane katika jiji hilo, naye alimwendea mara nyingi, akisema, 'Nisaidie kupata haki dhidi ya mpinzani wangu.'
and there was a widow in that city, and she came to him, saying, Avenge me of mine adverse party.
4 Kwa muda mrefu hakuwa tayari kumsaidia, lakini baada ya muda akasema moyoni mwake, `Ingawa mimi simwogopi Mungu au kuheshimu mtu,
And he would not for a time; but afterwards he said within himself, If even I fear not God and respect not man,
5 lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua nitamsaidia kupata haki yake, ili asije akanichosha kwa kunijia mara kwa mara. ''
at any rate because this widow annoys me I will avenge her, that she may not by perpetually coming completely harass me.
6 Kisha Bwana akasema, 'Sikiliza alivyosema huyo hakimu dhalimu.
And the Lord said, Hear what the unjust judge says.
7 Je Mungu pia hataleta haki kwa wateule wake ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, yeye hatakuwa mvumilivu kwao?
And shall not God at all avenge his elect, who cry to him day and night, and he bears long as to them?
8 Nawaambia kwamba ataleta haki kwao upesi. Lakini wakati Mwana wa Adamu atakapokuja, je, atakuta imani duniani? '
I say unto you that he will avenge them speedily. But when the Son of man comes, shall he indeed find faith on the earth?
9 Ndipo akawaambia mfano huu kwa baadhi ya watu ambao wanajiona wenyewe kuwa wenye haki na kuwadharau watu wengine,
And he spoke also to some, who trusted in themselves that they were righteous and made nothing of all the rest [of men], this parable:
10 'Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo mwingine mtoza ushuru.
Two men went up into the temple to pray; the one a Pharisee, and the other a tax-gatherer.
11 Farisayo akasimama akaomba mambo haya juu yake mwenyewe, 'Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine ambao ni wanyang'anyi, watu wasio waadilifu, wazinzi, au kama huyu mtoza ushuru.
The Pharisee, standing, prayed thus to himself: God, I thank thee that I am not as the rest of men, rapacious, unjust, adulterers, or even as this tax-gatherer.
12 Nafunga mara mbili kila wiki. Natoa zaka katika mapato yote ninayopata. '
I fast twice in the week, I tithe everything I gain.
13 Lakini yule mtoza ushuru, alisimama mbali, bila hakuweza hata kuinua macho yake mbinguni, akagonga kifua chake akisema, 'Mungu, nirehemu mimi mwenye dhambi.'
And the tax-gatherer, standing afar off, would not lift up even his eyes to heaven, but smote upon his breast, saying, O God, have compassion on me, the sinner.
14 Nawaambia, mtu huyu alirudi nyumbani akiwa amehesabiwa haki kuliko yule mwingine, kwa sababu kila ajikwezaye atashushwa, lakini kila mtu anayejinyenyekeza atainuliwa. '
I say unto you, This [man] went down to his house justified rather than that [other]. For every one who exalts himself shall be humbled, and he that humbles himself shall be exalted.
15 Watu walimletea watoto wao wachanga, ili aweze kuwagusa, lakini wanafunzi wake walipoona hayo, wakawazuia.
And they brought to him also infants that he might touch them, but the disciples when they saw [it] rebuked them.
16 Lakini Yesu akawaita kwake akisema, 'Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie. Maana ufalme wa Mungu ni wa watu kama hao.
But Jesus calling them to [him] said, Suffer little children to come to me, and do not forbid them, for of such is the kingdom of God.
17 Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto ni dhahiri hatauingia. '
Verily I say to you, Whosoever shall not receive the kingdom of God as a little child shall in no wise enter therein.
18 Mtawala mmoja akamwuliza, akisema, 'Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?' (aiōnios g166)
And a certain ruler asked him saying, Good teacher, having done what, shall I inherit eternal life? (aiōnios g166)
19 Yesu akamwambia, 'Kwa nini unaniita mwema? Hakuna mtu aliye mwema, ila Mungu peke yake.
But Jesus said to him, Why callest thou me good? There is none good but one, God.
20 Unazijua amri- usizini, usiue, Usiibe, usishuhudie uongo, waheshimu baba yako na mama yako.
Thou knowest the commandments: Do not commit adultery, Do not kill, Do not steal, Do not bear false witness, Honour thy father and thy mother.
21 Yule mtawala akasema, 'Mambo haya yote nimeyashika tangu nilipokuwa kijana.'
And he said, All these things have I kept from my youth.
22 Yesu alipoyasikia hayo akamwambia, '“Umepungukiwa jambo moja. Lazima uuze vyote ulivyonavyo na uwagawie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni -kisha njoo, unifuate. '
And when Jesus had heard this, he said to him, One thing is lacking to thee yet: Sell all that thou hast and distribute to the poor, and thou shalt have treasure in the heavens, and come, follow me.
23 Lakini tajiri aliposikia hayo, alihuzunika sana, kwa sababu alikuwa tajiri sana.
But when he heard this he became very sorrowful, for he was very rich.
24 Kisha Yesu, akamwona alivyohuzunika sana akasema, 'Jinsi gani itakavyokuwa vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
But when Jesus saw that he became very sorrowful, he said, How difficultly shall those who have riches enter into the kingdom of God;
25 Maana ni rahisi sana kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu. '
for it is easier for a camel to enter through a needle's eye than for a rich man to enter into the kingdom of God.
26 Wale waliosikia hayo, wakasema, 'Nani basi, atakayeweza kuokolewa?'
And those who heard it said, And who can be saved?
27 Yesu akajibu, 'Mambo yasiyowezekana kwa mwanadamu kwa Mungu yanawezekana.”
But he said, The things that are impossible with men are possible with God.
28 Petro akasema, 'Naam, sisi tumeacha kila kitu na tumekufuata wewe. '
And Peter said, Behold, we have left all things and have followed thee.
29 Kisha Yesu akawaambia, Amin, nawaambia kwamba hakuna mtu aliyeacha nyumba, au mke, au ndugu, au wazazi au watoto, kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
And he said to them, Verily I say to you, There is no one who has left home, or parents, or brethren, or wife, or children, for the kingdom of God's sake,
30 ambaye hatapokea mengi zaidi katika ulimwengu huu, na katika ulimwengu ujao, uzima wa milele. ' (aiōn g165, aiōnios g166)
who shall not receive manifold more at this time, and in the coming age life eternal. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Baada ya kuwakusanya wale kumi na wawibili, akawaambia, 'Tazama, tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote ambayo yameandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Adamu yatakamilishwa.
And he took the twelve to [him] and said to them, Behold, we go up to Jerusalem, and all things that are written of the Son of man by the prophets shall be accomplished;
32 Kwa maana atatiwa mikononi mwa watu wa Mataifa na atatendewa dhihaka na jeuri, na kutemewa mate.
for he shall be delivered up to the nations, and shall be mocked, and insulted, and spit upon.
33 Baada ya kumchapa viboko watamwua na siku ya tatu atafufuka. '
And when they have scourged [him] they will kill him; and on the third day he will rise again.
34 Hawakuelewa mambo haya, na neno hili lilikuwa limefichwa kwao, na hawakuelewa mambo yaliyosemwa.
And they understood nothing of these things. And this word was hidden from them, and they did not know what was said.
35 Ikawa Yesu ulipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi kando ya barabara akiomba msaada,
And it came to pass when he came into the neighbourhood of Jericho, a certain blind man sat by the wayside begging.
36 aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza nini kinatokea.
And when he heard the crowd passing, he inquired what this might be.
37 Wakamwambia kwamba Yesu wa Nazareti anapita.
And they told him that Jesus the Nazaraean was passing by.
38 Hivyo yule kipofu akalia kwa sauti, akisema, 'Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu.'
And he called out saying, Jesus, Son of David, have mercy on me.
39 wale waliokuwa wakitembea walimkemea huyo kipofu, wakamwambia anyamaze. Lakini yeye akazidi kulia kwa sauti, 'Mwana wa Daudi, unirehemu.
And those [who were] going before rebuked him that he might be silent; but he cried out so much the more, Son of David, have mercy on me.
40 Yesu akasimama akaamuru mtu yule aletwe kwake. Kisha yule kipofu alipomkaribia, Yesu akamwuliza,
And Jesus stood still, and commanded him to be led to him. And when he drew nigh he asked him [saying],
41 'Unataka nikufanyie nini?' Akasema, 'Bwana, nataka kuona.'
What wilt thou that I shall do to thee? And he said, Lord, that I may see.
42 Yesu akamwambia, 'Upate kuona. Imani yako imekuponya. '
And Jesus said to him, See: thy faith has healed thee.
43 Mara hiyo akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Walipoona hili, watu wote wakamsifu Mungu.
And immediately he saw, and followed him, glorifying God. And all the people when they saw [it] gave praise to God.

< Luka 18 >