< Luka 16 >

1 Yesu aliwaambia tena wanafunzi wake, “Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyekuwa na meneja, na alitaarifiwa ya kwamba meneja huyu anatapanya mali zake.
And he sayde also vnto his disciples, There was a certaine riche man, which had a stewarde, and he was accused vnto him, that he wasted his goods.
2 Hivyo tajiri akamwita, akamwambia, “Ni nini hii ninayo isikia juu yako? Toa hesabu ya umeneja wako, kwa kuwa huwezi kuwa meneja tena.'
And hee called him, and saide vnto him, Howe is it that I heare this of thee? Giue an accounts of thy stewardship: for thou maiest be no longer steward.
3 Yule meneja akasema moyoni mwake, Nifanye nini, maana bwana wangu ananiondolea kazi yangu ya umeneja? Sina nguvu za kulima, na kuomba naona haya.
Then the stewarde saide within himselfe, What shall I doe? for my master taketh away from me the stewardship. I cannot digge, and to begge I am ashamed.
4 Najua nitakalotenda ili nitakapotolewa katika kazi yangu ya uwakili watu wanikaribishe nyumbani mwao.
I knowe what I will doe, that when I am put out of the stewardship, they may receiue mee into their houses.
5 Hivyo wakili akawaita wadeni wa bwana wake kila mmoja akamwambia wa kwanza, 'unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?'
Then called he vnto him euery one of his masters detters, and said vnto the first, Howe much owest thou vnto my master?
6 Akasema vipimo mia moja vya mafuta akamwambia 'chukua hati yako keti upesi andika hamsini.'
And he said, An hudreth measures of oyle. And he saide to him, Take thy writing, and sitte downe quickely, and write fiftie.
7 kisha akamwambia mwingine na wewe unadaiwa kiasi gani?' akasema 'vipimo mia moja vya unga vya ngano.' Akamwambia 'twaa hati yako andika themanini.'
Then said he to another, How much owest thou? And hee sayde, An hundreth measures of wheate. Then he saide to him, Take thy writing, and write foure score.
8 Yule bwana akamsifu meneja dhalimu kwa vile alivyotenda kwa wereu. Kwakua watoto wa ulimwengu huu ni werevu nyingi na hushughulika kwa ujanja na watu wa upande wao kuliko walivyo watoto wa nuru. (aiōn g165)
And the Lord commended the vniust stewarde, because he had done wisely. Wherefore the children of this worlde are in their generation wiser then the children of light. (aiōn g165)
9 Nami nawaambia jifanyieni marafiki kwa mali ya udhalimu ili itakapokosekana wawakaribishe katika makao ya milele. (aiōnios g166)
And I say vnto you, Make you friends with the riches of iniquitie, that when ye shall want, they may receiue you into euerlasting habitations. (aiōnios g166)
10 Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia. na aliye dhalimu katika lililo dogo huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.
He that is faithfull in the least, hee is also faithful in much: and he that is vniust in the least, is vniust also in much.
11 Kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu ni nani atakayewaamini katika mali ya kweli?
If then ye haue not ben faithful in the wicked riches, who wil trust you in the true treasure?
12 Na kama hamkuwa waaminifu katika kutumia mali ya mtu mwingine ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
And if ye haue not bene faithfull in another mans goods, who shall giue you that which is yours?
13 Hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili, kwamaana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, ama atashikamana na huyu na kumdharau huyu. Hamuwezi kumtumikia Mungu na mali.”
No seruaunt can serue two masters: for either he shall hate the one, and loue the other: or els he shall leane to the one, and despise the other. Yee can not serue God and riches.
14 Basi Mafarisayo, ambao walikuwa wanapenda fedha waliyasikia haya yote na wakamdhihaki.
All these thinges heard the Pharises also which were couetous, and they scoffed at him.
15 Na akawaambia, “Ninyi ndiyo mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu.
Then he sayde vnto them, Yee are they, which iustifie your selues before men: but God knoweth your heartes: for that which is highly esteemed among men, is abomination in the sight of God.
16 Sheria na manabii vilikuwapo mpaka Yohana alivyokuja. Tangu wakati huo, habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujaribu kujiingiza kwa nguvu.
The Lawe and the Prophets endured vntill Iohn: and since that time the kingdome of God is preached, and euery man preasseth into it.
17 Lakini ni rahisi kwa mbingu na nchi vitoweke kuliko hata herufi moja ya sheria ikosekane.
Nowe it is more easie that heauen and earth shoulde passe away, then that one title of the Lawe should fall.
18 Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini, naye amwooaye yeye aliyeachwa na mumewe azini.
Whosoeuer putteth away his wife, and marieth another, committeth adulterie: and whosoeuer marieth her that is put away from her husband, committeth adulterie.
19 Palikua na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi na alikua akifurahia kila siku utajiri wake mkubwa.
There was a certaine riche man, which was clothed in purple and fine linnen, and fared well and delicately euery day.
20 Na maskini mmoja jina lake Lazaro aliwekwa getini pake, na ana vidonda.
Also there was a certaine begger named Lazarus, which was laide at his gate full of sores,
21 Naye alikua akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri hata mbwa wakaja wakamlamba vidonda vyake.
And desired to bee refreshed with the crommes that fell from the riche mans table: yea, and the dogges came and licked his sores.
22 Ikawa yule maskini alikufa na akachukuliwa na Malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa akazikwa.
And it was so that the begger died, and was caried by the Angels into Abrahams bosome. The rich man also died, and was buried.
23 Na kule kuzimu alipokua katika mateso aliyainua macho yake akamuona Ibrahimu kwa mbali na Lazaro kifuani mwake. (Hadēs g86)
And being in hell in torments, he lift vp his eyes, and sawe Abraham a farre off, and Lazarus in his bosome. (Hadēs g86)
24 Akalia akasema, 'Baba Ibrahimu, nihurumue umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
Then he cried, and saide, Father Abraham, haue mercie on mee, and sende Lazarus that hee may dippe the tip of his finger in water, and coole my tongue: for I am tormented in this flame.
25 Lakini Ibrahimu akasema, 'Mwanangu kumbuka ya kwamba katika maisha yako uliyapokea mambo yako mema, na Lazaro vivyo alipata mabaya. Ila sasa yupo hapa anafarijiwa na wewe unaumizwa.
But Abraham saide, Sonne, remember that thou in thy life time receiuedst thy pleasures, and likewise Lazarus paines: now therefore is he comforted, and thou art tormented.
26 Na zaidi ya hayo, kumewekwa shimo kubwa na refu kati yetu, ili wale wanaotaka kutoka huku kwenda kwenu wasiweze wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.'
Besides all this, betweene you and vs there is a great gulfe set, so that they which would goe from hence to you, can not: neither can they come from thence to vs.
27 Yule tajiri akasema, 'Nakuomba Baba Ibrahimu, kwamba umtume nyumbani kwa baba yangu
Then he said, I pray thee therfore, father, that thou wouldest sende him to my fathers house,
28 kwa kuwa ninao ndugu watano ili awaonye, kwa hofu kwamba wao pia watkuja mahali hapa pa mateso. '
(For I haue fiue brethren) that he may testifie vnto them, least they also come into this place of torment.
29 Lakini Ibrahimu akasema, 'Wanao Musa na manabii. Waache wawasikilize wao.
Abraham said vnto him, They haue Moses and the Prophets: let them heare them.
30 Yule tajiri akasema, 'hapana, Baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu watatubu.'
And he sayde, Nay, father Abraham: but if one came vnto them from the dead, they will amend their liues.
31 Lakini Ibrahimu akamwambia, 'wasipowasikia Musa na manabii hawatashawishiwa hata mtu akifufuka katika wafu.
Then he saide vnto him, If they heare not Moses and the Prophets, neither will they be persuaded, though one rise from the dead againe.

< Luka 16 >