< Luka 16 >

1 Yesu aliwaambia tena wanafunzi wake, “Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyekuwa na meneja, na alitaarifiwa ya kwamba meneja huyu anatapanya mali zake.
Jesus told his disciples this story. “There was once a rich man whose manager was accused of wasting what belonged to his master.
2 Hivyo tajiri akamwita, akamwambia, “Ni nini hii ninayo isikia juu yako? Toa hesabu ya umeneja wako, kwa kuwa huwezi kuwa meneja tena.'
So the rich man called in his manager, and asked him, ‘What's this I hear about you? Bring in your accounts, because you won't be continuing as manager.’
3 Yule meneja akasema moyoni mwake, Nifanye nini, maana bwana wangu ananiondolea kazi yangu ya umeneja? Sina nguvu za kulima, na kuomba naona haya.
The manager said to himself, ‘Now what will I do since my master is going to fire me from my job? I'm not strong enough to dig, and I'm ashamed to beg.
4 Najua nitakalotenda ili nitakapotolewa katika kazi yangu ya uwakili watu wanikaribishe nyumbani mwao.
Oh, I know what I'm going to do so that when I'm sacked as manager people will make me welcome in their homes.’
5 Hivyo wakili akawaita wadeni wa bwana wake kila mmoja akamwambia wa kwanza, 'unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?'
So he invited all those who were in debt to his master to come and see him. He asked the first one, ‘How much do you owe my master?’
6 Akasema vipimo mia moja vya mafuta akamwambia 'chukua hati yako keti upesi andika hamsini.'
The man replied, ‘A hundred units of oil.’ He said to him, ‘Sit down quickly. Take your bill, and change it to fifty.’
7 kisha akamwambia mwingine na wewe unadaiwa kiasi gani?' akasema 'vipimo mia moja vya unga vya ngano.' Akamwambia 'twaa hati yako andika themanini.'
Then he said to another, ‘How much do you owe?’ The man replied, ‘A hundred units of wheat.’ He said to him, ‘Take your bill and change it to eighty.’
8 Yule bwana akamsifu meneja dhalimu kwa vile alivyotenda kwa wereu. Kwakua watoto wa ulimwengu huu ni werevu nyingi na hushughulika kwa ujanja na watu wa upande wao kuliko walivyo watoto wa nuru. (aiōn g165)
The rich man commended his dishonest manager for his cunning idea. The children of this world are more cunning towards one another than are the children of light. (aiōn g165)
9 Nami nawaambia jifanyieni marafiki kwa mali ya udhalimu ili itakapokosekana wawakaribishe katika makao ya milele. (aiōnios g166)
I tell you, use the wealth of this world to make friends for yourselves so that when it's gone, you'll be welcomed into an eternal home. (aiōnios g166)
10 Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia. na aliye dhalimu katika lililo dogo huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.
If you can be trusted with very little you can also be trusted with much; if you are dishonest with very little you will also be dishonest with much.
11 Kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu ni nani atakayewaamini katika mali ya kweli?
So if you can't be trusted when it comes to worldly wealth, who will trust you with true riches?
12 Na kama hamkuwa waaminifu katika kutumia mali ya mtu mwingine ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
And if you can't be trusted with what belongs to someone else, who will trust you with what is yours?
13 Hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili, kwamaana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, ama atashikamana na huyu na kumdharau huyu. Hamuwezi kumtumikia Mungu na mali.”
No servant can obey two masters. Either he will hate one and love the other, or he will be devoted to one and despise the other. You can't serve both God and Money.”
14 Basi Mafarisayo, ambao walikuwa wanapenda fedha waliyasikia haya yote na wakamdhihaki.
The Pharisees, who loved money, heard what Jesus said and laughed at him.
15 Na akawaambia, “Ninyi ndiyo mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu.
But Jesus told them, “You appear pious to people, but God knows what you're thinking. What people value highly is detested by God.
16 Sheria na manabii vilikuwapo mpaka Yohana alivyokuja. Tangu wakati huo, habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujaribu kujiingiza kwa nguvu.
What was written in the law and the prophets lasted until John. From then on the good news of the kingdom of God is being spread, and everyone is forcing their way in.
17 Lakini ni rahisi kwa mbingu na nchi vitoweke kuliko hata herufi moja ya sheria ikosekane.
However, it's easier for heaven and earth to pass away than for the smallest point of the Law to disappear.
18 Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini, naye amwooaye yeye aliyeachwa na mumewe azini.
Any man who divorces his wife and marries someone else commits adultery, and a man who marries a divorced woman commits adultery.
19 Palikua na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi na alikua akifurahia kila siku utajiri wake mkubwa.
Once there was a man who was rich. He wore purple clothes and fine linen, and enjoyed a luxurious life.
20 Na maskini mmoja jina lake Lazaro aliwekwa getini pake, na ana vidonda.
A beggar named Lazarus used to sit at his gate, covered in sores,
21 Naye alikua akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri hata mbwa wakaja wakamlamba vidonda vyake.
longing to eat the leftovers from the rich man's table. Even the dogs came and licked his sores.
22 Ikawa yule maskini alikufa na akachukuliwa na Malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa akazikwa.
Then the beggar died, and angels carried him away to be with Abraham. The rich man also died and was buried.
23 Na kule kuzimu alipokua katika mateso aliyainua macho yake akamuona Ibrahimu kwa mbali na Lazaro kifuani mwake. (Hadēs g86)
In Hades, where he was in torment, he looked up and saw Abraham in the far distance, with Lazarus beside him. (Hadēs g86)
24 Akalia akasema, 'Baba Ibrahimu, nihurumue umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
‘Father Abraham,’ he called out, ‘Have mercy on me and send Lazarus to dip the tip of his finger in water and cool my tongue, because I'm burning in agony.’
25 Lakini Ibrahimu akasema, 'Mwanangu kumbuka ya kwamba katika maisha yako uliyapokea mambo yako mema, na Lazaro vivyo alipata mabaya. Ila sasa yupo hapa anafarijiwa na wewe unaumizwa.
But Abraham replied, ‘My son, remember that you enjoyed the good things of life, while Lazarus had a very poor life. Now he is here being comforted, while you suffer in torment.
26 Na zaidi ya hayo, kumewekwa shimo kubwa na refu kati yetu, ili wale wanaotaka kutoka huku kwenda kwenu wasiweze wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.'
Apart from that, there's a great gulf that stretches between us and you. Nobody who wants to cross from here to you can do so, and nobody can cross from there over to us.’
27 Yule tajiri akasema, 'Nakuomba Baba Ibrahimu, kwamba umtume nyumbani kwa baba yangu
The rich man said, ‘Then Father, I beg you, please send him to my father's house.
28 kwa kuwa ninao ndugu watano ili awaonye, kwa hofu kwamba wao pia watkuja mahali hapa pa mateso. '
For I have five brothers and he can warn them so that they don't end up here in this place of torment.’
29 Lakini Ibrahimu akasema, 'Wanao Musa na manabii. Waache wawasikilize wao.
But Abraham replied, ‘They have Moses and the prophets. They should listen to them.’
30 Yule tajiri akasema, 'hapana, Baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu watatubu.'
‘No, father Abraham,’ said the man. ‘But they would repent if someone went to them from the dead!’
31 Lakini Ibrahimu akamwambia, 'wasipowasikia Musa na manabii hawatashawishiwa hata mtu akifufuka katika wafu.
Abraham said to him, ‘If they won't listen to Moses and the prophets, they won't be convinced even if someone returns from the dead.’”

< Luka 16 >