< Luka 14 >

1 Iltokea siku ya Sabato, alipokua akienda nyumbani kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo kula mkate, nao walikuwa wakimchunguza kwa karibu.
When he went into the house of one of the rulers of the Pharisees on a Sabbath to eat bread, they were watching him.
2 Tazama, pale mbele yake alikuwa mtu ambaye anasumbuliwa na uvimbe.
Behold, a certain man who had dropsy was in front of him.
3 Yesu aliuliza wataalam katika sheria ya Wayahudi na Mafarisayo, “Je, ni halali kumponya siku ya Sabato, au sivyo?”
Jesus, answering, spoke to the lawyers and Pharisees, saying, “Is it lawful to heal on the Sabbath?”
4 Lakini wao walikuwa kimya, kwahiyo Yesu akamshika, akamponya na kumruhusu aende zake.
But they were silent. He took him, and healed him, and let him go.
5 Naye akawaambia, “Ni nani kati yenu ambaye ana mtoto au ng'ombe anatumbukia kisimani siku ya Sabato hata mvuta nje mara moja?”
He answered them, “Which of you, if your son or an ox fell into a well, would not immediately pull him out on a Sabbath day?”
6 Wao hawakuwa na uwezo wa kutoa jibu kwa mambo haya.
They could not answer him regarding these things.
7 Wakati Yesu alipogundua jinsi wale walioalikwa kwamba wamechagua viti vya heshima, akawaambia mfano, akiwaambia,
He spoke a parable to those who were invited, when he noticed how they chose the best seats, and said to them,
8 “Wakati mnapoalikwa na mtu harusini, usiketi katika nafasi za heshima, kwa sababu inawezekana amealikwa mtu ambaye ni wakuheshimiwa zaidi kuliko wewe.
“When you are invited by anyone to a wedding feast, do not sit in the best seat, since perhaps someone more honorable than you might be invited by him,
9 Wakati mtu aliyewaalika ninyi wawili akifika, atakuambia wewe, “mpishe mtu huyu nafasi yako,” na kisha kwa aibu utaanza kuchukua nafasi ya mwisho.
and he who invited both of you would come and tell you, ‘Make room for this person.’ Then you would begin, with shame, to take the lowest place.
10 Lakini wewe ukialikwa, nenda ukakae mahali pa mwisho, ili wakati yule aliyekualika akija, aweze kukuambia wewe, `Rafiki, nenda mbele zaidi.” ndipo utakuwa umeheshimika mbele ya wote walioketi pamoja nawe mezani.
But when you are invited, go and sit in the lowest place, so that when he who invited you comes, he may tell you, ‘Friend, move up higher.’ Then you will be honored in the presence of all who sit at the table with you.
11 Kwa maana kila ajikwezaye atashushwa, na yeye ajishushae atakwezwa. '
For everyone who exalts himself will be humbled, and whoever humbles himself will be exalted.”
12 Yesu pia alimwambia mtu aliyemwalika, 'Unapotoa chakula cha mchana au cha jioni, usiwaalike rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au majirani zako matajiri, ili kwamba wao wasije wakakualika wewe ukapata malipo.
He also said to the one who had invited him, “When you make a dinner or a supper, do not call your friends, nor your brothers, nor your kinsmen, nor rich neighbors, or perhaps they might also return the favor, and pay you back.
13 Badala yake, unapofanya sherehe, waalike maskini, vilema, viwete na vipofu,
But when you make a feast, ask the poor, the maimed, the lame, or the blind;
14 na wewe utabarikiwa, kwa sababu hawawezi kukulipa. Kwa maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki.”
and you will be blessed, because they do not have the resources to repay you. For you will be repaid in the resurrection of the righteous.”
15 Wakati mmoja wa wale walioketi mezani pamoja na Yesu aliposikia hayo, naye akamwambia, “Amebarikiwe yule atakayekula mkate katika Ufalme wa Mungu!”
When one of those who sat at the table with him heard these things, he said to him, “Blessed is he who will feast in God’s Kingdom!”
16 Lakini Yesu akamwambia, “Mtu mmoja aliandaa sherehe kubwa, akaalika watu wengi.
But he said to him, “A certain man made a great supper, and he invited many people.
17 Wakati sherehe ilipokuwa tayari, alimtuma mtumishi wake kuwaambia wale walioalikwa, `'Njooni, kwa sababu vitu vyote vimekwisha kuwekwa tayari.'
He sent out his servant at supper time to tell those who were invited, ‘Come, for everything is ready now.’
18 Wote, wakaanza kuomba radhi. Wa kwanza akamwambia mtumishi, 'Nimenunua shamba, lazima niende kuliona. Tafadhali unisamehe.'
They all as one began to make excuses. “The first said to him, ‘I have bought a field, and I must go and see it. Please have me excused.’
19 Na mwingine akasema, `'Nimenunua jozi tano za ng'ombe, na mimi naenda kuwajaribu. Tafadhali uniwie radhi.'
“Another said, ‘I have bought five yoke of oxen, and I must go try them out. Please have me excused.’
20 Na mtu mwingine akasema, 'Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.'
“Another said, ‘I have married a wife, and therefore I cannot come.’
21 Mtumishi akarudi na kumwambia bwana wake mambo hayo. Yule mwenye nyumba alikasirika akamwambia mtumishi wake, `'Nenda upesi mitaani na katika vichochoro vya mji ukawalete hapa maskini, vilema, vipofu na walemavu.”
“That servant came, and told his lord these things. Then the master of the house, being angry, said to his servant, ‘Go out quickly into the streets and lanes of the city, and bring in the poor, maimed, blind, and lame.’
22 Mtumimishi akasema, `Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa bado kuna nafasi.'
“The servant said, ‘Lord, it is done as you commanded, and there is still room.’
23 Bwana akamwambia mtumishi, 'Nenda katika njia kuu na vichochoro na uwashurutishe watu waingie, ili nyumba yangu ijae.
“The lord said to the servant, ‘Go out into the highways and hedges, and compel them to come in, that my house may be filled.
24 Kwamaana nawaambia, katika wale walioalikwa wa kwanza hapana atakayeonja sherehe yangu. '
For I tell you that none of those men who were invited will taste of my supper. For many are called, but few are chosen.’”
25 Sasa umati mkubwa walikuwa wanakwenda pamoja naye, naye akageuka na akawaambia,
Now great multitudes were going with him. He turned and said to them,
26 'Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, mama yake, mke wake, watoto wake, ndugu zake waume na wanawake- ndio, na hata maisha yake pia -hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
“If anyone comes to me, and does not disregard his own father, mother, wife, children, brothers, and sisters, yes, and his own life also, he cannot be my disciple.
27 Mtu asipochukua msalaba wake na kuja nyuma yangu hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
Whoever does not bear his own cross and come after me, cannot be my disciple.
28 Maana ni nani kati yenu, ambaye anatamani kujenga mnara hataketi kwanza akadirie gharama kwa mahesabu kama ana kile anachohitaji ili kukamilisha hilo?
For which of you, desiring to build a tower, does not first sit down and count the cost, to see if he has enough to complete it?
29 Vinginevyo, baada ya kuweka msingi na kushindwa kumaliza, wote walioona wataanza kumdhihaki,
Or perhaps, when he has laid a foundation and is not able to finish, everyone who sees begins to mock him,
30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.'
saying, ‘This man began to build and was not able to finish.’
31 Au mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine katika vita, ambae hatakaa chini kwanza na kuchukua ushauri kuhusu kama ataweza, pamoja na watu elfu kumi kupigana na mfalme mwingine anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?
Or what king, as he goes to encounter another king in war, will not sit down first and consider whether he is able with ten thousand to meet him who comes against him with twenty thousand?
32 Na kama sivyo, wakati jeshi la wengine bado liko mbali, hutuma balozi kutaka masharti ya amani.
Or else, while the other is yet a great way off, he sends an envoy and asks for conditions of peace.
33 Kwa hiyo basi, yeyote kati yenu ambaye hataacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
So therefore, whoever of you who does not renounce all that he has, he cannot be my disciple.
34 Chumvi ni nzuri, lakini ikiwa Chumvi imepoteza ladha yake, jinsi gani inaweza kuwa chumvi tena?
“Salt is good, but if the salt becomes flat and tasteless, with what do you season it?
35 Haina matumizi kwa udongo au hata kwa mbolea. hutupwa mbali. Yeye aliye na masikio ya kusikia, na asikie.”
It is fit neither for the soil nor for the manure pile. It is thrown out. He who has ears to hear, let him hear.”

< Luka 14 >