< Luka 12 >

1 Kwa wakati huo, maelfu mengi ya watu walikusanyika pamoja, kiasi cha kuanza kukanyagana, akaanza kusema na wanafunzi wake kwanza, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo ambayo ni unafiki”
Meanwhile the people had gathered in thousands, so that they trod upon one another, when Jesus, addressing himself to his disciples, began by saying to them: “Be on your guard against the leaven — that is, the hypocrisy — of the Pharisees.
2 Na hapatakuwepo na siri iliyofichika ambayo haitafunuliwa, wala jambo lililofichwa ambalo halitajulikana.
There is nothing, however covered up, which will not be uncovered, nor anything kept secret which will not become known.
3 Na lolote mlilolisema katika giza, litasikiwa katika mwanga. Na yoyote mliyoyasema kwenye sikio ndani ya vyumba vyenu vya ndani vilivyofungwa yatatangazwa juu ya paa la nyumba.
Hence all that you have said in the dark will be heard in the light, and what you have spoken in the ear, within closed doors, will be proclaimed upon the housetops.
4 Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili na kisha hawana kitu kingine cha kufanya,
To you who are my friends I say, Do not be afraid of those who kill the body, but after that can do no more.
5 Lakini nitawaonya mtakaye mwogopa. Mwogopeni yule ambaye baada ya kuwa ameua, ana mamlaka ya kutupa jehanamu. Ndiyo, nawaambiani ninyi, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
I will show you of whom you should be afraid. Be afraid of him who, after killing you, has the power to fling you into the Pit. Yes, I say, be afraid of him. (Geenna g1067)
6 Je shomoro watano hawauzwi kwa sarafu mbili? hata hivyo hakuna hata mmoja wao atakayesahaulika mbele za Mungu.
Are not five sparrows sold for a penny? Yet not one of them has escaped God’s notice.
7 Lakini mjue kuwa, nywele za vichwa vyenu vimehesabiwa. Msiogope. Ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
No, the very hairs of your head are all numbered. Do not be afraid; you are of more value than many sparrows.
8 Ninawaambia, yeyote atakayenikiri Mimi mbele za watu, Mwana wa Adamu atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
Every one, I tell you, who shall acknowledge me before his fellow men, the Son of Man, also, will acknowledge before God’s angels;
9 Lakini yeyeyote atakayenikana mbele za watu naye atakanwa mbele ya Malaika wa Mungu.
but he, who disowns me before his fellow men, will be altogether disowned before God’s angels.
10 Yeyote atakayesema neno baya juu ya Mwana wa Adamu, atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu, hatasamehewa.
Every one who shall say anything against the Son of Man will be forgiven, but for him who slanders the Holy Spirit there will be no forgiveness.
11 Watakapowapeleka mbele za wakuu wa masinagogi, watawala, na wanye mamlaka, msiogope juu na namna ya kuongea katika kujitetea au nini mtakachosema,
Whenever they take you before the Synagogue Courts or the magistrates or other authorities, do not be anxious as to how you will defend yourselves, or what your defence will be, or what you will say;
12 kwa kuwa Roho Mtakatifu atawafundisha namna mtakavyosema kwa wakati huo.”
for the Holy Spirit will show you at the moment what you ought to say.”
13 Mtu mmoja katika kusanyiko akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu anigawie sehemu ya uruthi wangu.”
“Teacher,” a man in the crowd said to Jesus, “tell my brother to share the property with me.”
14 Yesu akamjibu, ni nani aliye niweka kuwa mwamuzi na mpatanishi kati yenu?
But Jesus said to him: “Man, who made me a judge or an arbiter between you?”
15 Ndipo akawaambia, Jihadharini na kila namna ya tamaa, kwa sababu uzima wa mtu hauko katika wingi wa vitu alivyo navyo.”
And then he added: “Take care to keep yourselves free from every form of covetousness; for even in the height of his prosperity a man’s true Life does not depend on what he has.”
16 Yesu akawaambia mfano, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana,
Then Jesus told them this parable — “There was once a rich man whose land was very fertile;
17 na akajiuliza ndani yake, akisema, nitafanyaje kwani sina mahali pa kuhifadhi mazao yangu?
and he began to ask himself ‘What shall I do, for I have nowhere to store my crops?
18 Akasema, nitafanya hivi. Nitavunja ghala zangu ndogo na kujenga iliyo kubwa, na kuyahifadhi mazao yangu yote na vitu vingine.
This is what I will do,’ he said; ‘I will pull down my barns and build larger ones, and store all my grain and my goods in them;
19 Nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, umejiwekea akiba ya vitu vingi kwa miaka mingi. Pumzika, ule, unywe na kustarehe.”
and I will say to myself, Now you have plenty of good things put by for many years; take your ease, eat, drink, and enjoy yourself.’
20 Lakini Mungu akamwambia, ewe mtu mpumbavu, usiku wa leo wanahitaji roho kutoka kwako, na vitu vyote ulivyoviandaa vitakuwa vya nini?
But God said to the man ‘Fool! This very night your life is being demanded; and as for all you have prepared — who will have it?’
21 Ndivyo itakavyokuwa kwa kila mtu anayejiwekea mali na si kujitajirisha kwa ajili ya Bwana.
So it is with those who lay by wealth for themselves and are not rich to the glory of God.”
22 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Kwa hiyo nawaambia msihofu juu ya maisha yenu ya kuwa mtakula nini au juu ya miili yenu ya kuwa mtavaa nini
And Jesus said to his disciples: “That is why I say to you, Do not be anxious about the life here — what you can get to eat; nor yet about your body — what you can get to wear.
23 Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
For life is more than food, and the body than its clothes.
24 Angalieni ndege wa angani, hawalimi wala hawavuni. Hawana chumba wala ghala ya kuhifadhia, lakini Baba yenu huwalisha. Ninyi si bora zaidi kuliko ndege!
Think of the ravens — they neither sow nor reap; they have neither storehouse nor barn; and yet God feeds them! And how much more precious are you than birds!
25 Ni yupi kati yenu ambaye akijisumbua ataweza kuongeza dhiraa moja katika maisha yake?
But which of you, by being anxious, can prolong his life a moment?
26 Ikiwa basi hamuwezi kufanya hicho kitu kidogo kilicho rahisi kwa nini basi kusumbukia hayo mengine?
And, if you cannot do even the smallest thing, why be anxious about other things?
27 Angalieni maua -yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayasokoti. Lakini nawaambia, hata Sulemani katika utukufu wake wote hakuvikwa kama mojawapo ya haya,
Think of the lilies, and how they grow. They neither toil nor spin; yet, I tell you, even Solomon in all his splendour was not robed like one of these.
28 Kama Mungu huyavika vizuri majani ya kondeni, ambayo leo yapo, na kesho hutupwa kwenye moto. Je si zaidi atawavika ninyi? enyi wa imani haba!
If, even in the field, God so clothes the grass which is living to-day and to-morrow will be thrown into the oven, how much more will he clothe you, O men of little faith!
29 Msisumbukie juu ya kuwa mtakula nini au mtakunywa nini, wala msiwe na hofu.
And you — do not be always seeking what you can get to eat or what you can get to drink; and do not waver.
30 Kwa kuwa Mataifa yote ya dunia husumbukia mambao yao. Na Baba yenu anajua ya kuwa mnahitaji hayo.
These are the things for which all the nations of the world are seeking, and your Father knows that you need them.
31 Lakini tafuteni ufalme wake kwanza, na hayo mengine mtazidishiwa,
No, seek his Kingdom, and these things shall be added for you.
32 msiogope, enyi kundi dogo, kwa sababu Baba yenu anafurahia kuwapa ninyi huo ufalme.
So do not be afraid, my little flock, for your Father has been pleased to give you the Kingdom.
33 Uzeni mali zenu na mkawape maskini, mjifanyie mifuko isiyoishiwa hazina ya mbinguni isiyokoma, sehemu ambapo wezi hawatakaribia wala nondo haitaweza kuharibu.
Sell what belongs to you, and give in charity. Make yourselves purses that will not wear out — an inexhaustible treasure in Heaven, where no thief comes near, or moth works ruin.
34 Kwa kuwa palipo na hazina yako, ndipo na roho yako itakapokuwepo.
For where your treasure is, there also will your heart be.
35 Nguo zenu ndefu ziwe zimefungwa kwa mkanda, na taa zenu zihakikishwe kuwa zinaendelee kuwaka,
Make yourselves ready, with your lamps alight;
36 na muwe kama watu wanaomtazamia Bwana wao kutoka kwenye sherehe ya harusi, ili kwamba akija na kupiga hodi, wataweze kumfungulia mlango kwa haraka.
and be like men who are waiting for their Master’s return from his wedding, so that, when he comes and knocks, they may open the door for him at once.
37 Wamebarikiwa wale watumishi, ambao Bwana atawakuta wako macho. Hakika atafunga nguo yake ndefu kwa mkanda, kisha atawaketisha chini kwa chakula, na kisha kuwahudumia.
Happy are those servants whom, on his return, the Master will find watching. I tell you that he will make himself ready, and bid them take their places at table, and will come and wait upon them.
38 Kama Bwana atakuja kwa zamu ya pili ya ulinzi ya usiku, au hata zamu ya tatu ya ulinzi, na kuwakuta wakiwa tayari, itakuwa ni heri kwa hao watumishi.
Whether it is late at night, or in the early morning that he comes, if he finds all as it should be, then happy are they.
39 Zaidi ya hayo, mjue hili, kama bwana mwenye nyumba angelijua saa ambayo mwivi anakuja, asingeliruhusu nyumba yake ifunjwe.
This you do know, that, had the owner of the house known at what time the thief was coming, he would have been on the watch, and would not have let his house be broken into.
40 Iweni tayari pia kwani hamjui ni wakati gani mwana wa Adamu atarudi.
Do you also prepare, for when you are least expecting him the Son of Man will come.”
41 Petro akasema, “Bwana, watuambia sisi wenyewe hii mifano, au unamwambia kila mtu?
“Master,” said Peter, “are you telling this parable with reference to us or to every one?”
42 Bwana akawaambia, “Ni nani mtumwa mwaminifu au mwenye hekima ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wengine, ili awagawie chakula chao kwa wakati mwafaka?
“Who, then,” replied the Master, “is that trustworthy steward, the careful man, who will be placed by his master over his establishment, to give them their rations at the proper time?
43 Amebarikiwa mtumishi yule, ambaye bwana wake akija atamkuta akifanya yale aliyoagizwa.
Happy will that servant be whom his master, when he comes home, shall find doing this.
44 Hakika nawaambia ninyi ya kuwa atamweka juu ya mali yake yote.
His master, I tell you, will put him in charge of the whole of his property.
45 Lakini Mtumishi yule akisema moyoni mwake, “bwana wangu anachelewa kurudi; hivyo akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, kisha akaanza kula, kunywa na kulewa,
But should that servant say to himself ‘My master is a long time coming,’ and begin to beat the menservants and the maidservants, and to eat and drink and get drunk,
46 bwana wake yule mtumwa atakuja katika siku asiyotegemea na saa asiyoijua, naye atamkata vipande vipande na kumuweka katika sehemu pamoja na wasiokuwawaaminifu'
that servant’s master will come on a day when he does not expect him, and at an hour of which he is unaware, and will flog him severely and assign him his place among the untrustworthy.
47 Mtumishi, anayejua mapenzi ya bwana wake, naye hakujiandaaa wala hakufanya sawa sawa na mapenzi yake, atapigwa viboko vingi.
The servant who knows his master’s wishes and yet does not prepare and act accordingly will receive many lashes;
48 Lakini mtumishi asiyejua mapenzi ya bwana wake, lakini akafanya yanayostahili adhabu, atapigwa viboko vichache. Kwa kuwa yeye aliyepewa vingi, vingi hudaiwa kutoka kwake, na yeye aliyeaminiwa kwa vingi, kwake vitadaiwa vingi zaidi.
while one who does not know his master’s wishes, but acts so as to deserve a flogging, will receive but few. From every one to whom much has been given much will be expected, and from the man to whom much has been entrusted the more will be demanded.
49 Nimekuja kuwasha moto duniani, na natamani iwe umekwishawaka,
I came to cast fire upon the earth; and what more can I wish, if it is already kindled?
50 Lakini nina ubatizo ambao nitabatizwa, na nina huzuni mpaka utkapokamilika!
There is a baptism that I must undergo, and how great is my distress until it is over!
51 Je mnafikiri kuwa nimekuja kuleta amani duniani? Hapana, Nawaambieni, badala yake nimeleta mgawanyiko.
Do you think that I am here to give peace on earth? No, I tell you, but to cause division.
52 Tangu sasa na kuendelea kutakuwa na watu watano katika nyumba moja wamegawanyika, na watatu watakuwa kinyume na wawili, na wawili watakuwa kinyume na watatu.
For from this time, if there are five people in a house, they will be divided, three against two, and two against three.
53 Watagawanyika, baba atakuwa kinyume na mwanae, na mwanae atakuwa kinyume na babaye, mama atakuwa kinyume na binti yake, na binti atakuwa kinyume na mama yake, Mama mkwe atakuwa kinyume na mkwe wake naye mkwe atakuwa kinyume na mama mkwe wake.
‘Father will be opposed to son and son to father, mother to daughter and daughter to mother, mother-in-law to her daughter-in-law and daughter-in-law to her mother-in-law.’”
54 Yesu akawa anawaambia makutano pia, “Mara muonapo mawingu yakitokea magharibi, mnasema nyakati za mvua zimewadia; na ndivyo inavyo kuwa,
And to the people Jesus said: “When you see a cloud rising in the west, you say at once ‘There is a storm coming,’ and come it does.
55 Na upepo wa kusini ukivuma, mnasema, Patakuwepo na joto kali, na ndivyo inavyokuwa.
And when you see that the wind is in the south, you say ‘It will be burning hot,’ and so it proves.
56 Enyi wanafiki, mnaweza kutafsiri mwonekano wa nchi na anga, lakini inakuwaje hamuwezi kuutafsiri wakati uliopo?
Hypocrites! You know how to judge of the earth and the sky; how is it, then, that you cannot judge of this time?
57 Ni kwa nini kila mmoja wenu asipambanue lililo sahihi kwake kulifanya wakati ambapo angali na nafasi ya kufanya hivyo?
Why do not you yourselves decide what is right?
58 Maana mkienda na mshitaki wako mbele ya hakimu, jitahidi kupatana na mshitaki wako mungali bado mko njiani asije akakupeleka kwa hakimu, na hakimu akupeleka kwa ofisa, na ofisa akakutupa gerezani.
When, for instance, you are going with your opponent before a magistrate, on your way to the court do your best to be quit of him; for fear that he should drag you before the judge, then the judge will hand you over to the bailiff of the court, and the bailiff throw you into prison.
59 Nakuambia, hutatoka huko hadi umelipa mpaka senti ya mwisho.
You will not, I tell you, come out until you have paid the very last farthing.”

< Luka 12 >