< Luka 1 >

1 Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
Ker so že mnogi vzeli v roko, da po vrsti uredijo izjavo o teh stvareh, ki se najbolj gotovo verjamejo med nami,
2 kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
celo kakor so nam jih izročili [tisti], ki so bili od začetka priče in služabniki besede,
3 Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
se je tudi meni zdelo dobro, od samega začetka imeti popolno razumevanje o vseh stvareh, da tebi, nadvse odlični Teófil, napišem po vrsti,
4 Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
da lahko spoznaš zanesljivost o teh besedah, o katerih si bil poučen.
5 Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
V dneh Heroda, judejskega kralja, je bil nek duhovnik, imenovan Zaharija, iz Abíjeve skupine, in njegova žena je bila izmed Aronovih hčera in njeno ime je bilo Elizabeta.
6 Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
Oba sta bila pravična pred Bogom in sta brez krivde živela po vseh Gospodovih zapovedih in odredbah.
7 Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
Ker je bila Elizabeta jalova nista imela nobenega otroka in oba sta bila zelo zvrhana v letih.
8 Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
In pripetilo se je, medtem ko je pred Bogom opravljal duhovniško službo, po vrstnem redu svoje skupine,
9 Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
glede na navado duhovniške službe, je bil na njem žreb, da zažge kadilo, ko je odšel v Gospodov tempelj.
10 Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
Celotna množica ljudi pa je ob času zažiganja kadila zunaj molila.
11 Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
In prikazal se mu je Gospodov angel, stoječ na desni strani kadilnega oltarja.
12 Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
Ko pa ga je Zaharija zagledal, se je vznemiril in strah ga je spreletel.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
Toda angel mu je rekel: »Ne boj se, Zaharija, kajti tvoja molitev je uslišana in tvoja žena Elizabeta ti bo rodila sina in ti boš klical njegovo ime Janez.
14 Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
Imel boš radost in veselje in mnogi se bodo veselili ob njegovem rojstvu.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
Kajti velik bo v Gospodovih očeh in ne bo pil niti vina niti močne pijače in celó od maternice svoje matere bo izpolnjen s Svetim Duhom.
16 Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
In mnoge izmed Izraelovih otrok bo obrnil h Gospodu, njihovemu Bogu.
17 Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
Pred njim bo šel z Elijevim duhom in močjo, da obrne srca očetov k otrokom in neposlušne k modrosti pravičnih; da pripravi ljudstvo, pripravljeno za Gospoda.«
18 Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
Zaharija je angelu rekel: »Po čem bom to spoznal? Kajti starec sem in moja žena je zelo zvrhana v letih.«
19 Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
Angel mu odgovori in reče: »Jaz sem Gabriel, ki stojim v prisotnosti Boga in poslan sem, da ti govorim in da ti pokažem te vesele novice.
20 Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
Glej, ker nisi verjel mojim besedam, ki se bodo uresničile ob njihovem pravem času, boš postal nem in ne boš mogel govoriti do dne, ko se bodo te besede izpolnile.«
21 Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
In ljudje so čakali na Zaharija in se čudili, da se je tako dolgo mudil v templju.
22 Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
Ko pa je prišel ven, jim ni mogel spregovoriti, in zaznali so, da je videl v templju videnje, kajti dajal jim je znamenja, ostal pa je brez besed.
23 Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
Pripetilo se je, kakor hitro so bili dnevi njegovega služenja dovršeni, da se je odpravil k svoji lastni hiši.
24 Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
Po teh dneh je njegova žena Elizabeta spočela in se pet mesecev skrivala, rekoč:
25 “Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
»Tako je Gospod ravnal z menoj v dneh, v katerih je pogledal name, da odvzame mojo grajo izmed ljudi.«
26 Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
V šestem mesecu pa je bil od Boga poslan angel Gabriel v galilejsko mesto, imenovano Nazaret,
27 kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
k devici, zaročeni z možem, katerega ime je bilo Jožef, iz Davidove hiše; in devici je bilo ime Marija.
28 Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
Angel je vstopil k njej in rekel: »Pozdravljena, ti, ki si zelo spoštovana, Gospod je s teboj, blagoslovljena si med ženskami.«
29 Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
Ko pa ga je zagledala, je bila ob njegovem govoru zaskrbljena in v svojih mislih preudarjala, kakšne vrste pozdrav naj bi to bil.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
Angel ji je rekel: »Ne boj se, Marija, kajti pri Bogu si našla naklonjenost.
31 Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
Glej, v svoji maternici boš spočela in rodila sina in njegovo ime boš klicala JEZUS.
32 Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
Velik bo in imenovan bo Sin Najvišjega; in Gospod Bog mu bo dal prestol njegovega očeta Davida
33 Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
in nad Jakobovo hišo bo vladal večno in njegovemu kraljestvu ne bo konca.« (aiōn g165)
34 Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
Potem je Marija rekla angelu: »Kako se bo to zgodilo, glede na to, da ne poznam moškega?«
35 Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
Angel je odgovoril in ji rekel: »Sveti Duh bo prišel nadte in moč Najvišjega te bo obsenčila, zato bo tudi ta sveta oseba, ki bo rojena od tebe, imenovana Božji Sin.
36 Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
Glej, tvoja sestrična Elizabeta je prav tako v svoji visoki starosti spočela sina, in to je šesti mesec z njo, ki je bila imenovana jalova.
37 Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
Kajti z Bogom nič ne bo nemogoče.«
38 Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
Marija je rekla: »Glej, Gospodova pomočnica; naj se mi zgodi glede na tvojo besedo.« In angel je odšel od nje.
39 Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
Marija je v tistih dneh vstala in z naglico odšla v hribovito deželo, v Judovo mesto
40 Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
in vstopila v Zaharijevo hišo ter pozdravila Elizabeto.
41 Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
In pripetilo se je, ko je Elizabeta zaslišala Marijin pozdrav, da je dete poskočilo v njeni maternici in Elizabeta je bila izpolnjena s Svetim Duhom
42 Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
in zaklicala z močnim glasom ter rekla: »Blagoslovljena si ti med ženskami in blagoslovljen je sad tvoje maternice.
43 Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
Od kod je meni to, da bi prišla k meni mati mojega Gospoda?
44 Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
Kajti glej, brž ko je glas tvojega pozdrava zazvenel v mojih ušesih, je dete v moji maternici od radosti poskočilo.
45 Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
Blagoslovljena je tista, ki je verovala, kajti izpolnile se bodo te besede, ki so ji bile povedane od Gospoda.«
46 Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
Marija je rekla: »Moja duša poveličuje Gospoda
47 na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
in moj duh se veseli v Bogu, mojem Odrešeniku.
48 Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
Kajti ozrl se je na nizek stan svoje pomočnice, kajti glej, odslej me bodo vsi rodovi imenovali blagoslovljeno.
49 Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
Kajti tisti, ki je mogočen, mi je storil velike stvari in sveto je njegovo ime.
50 Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
In njegovo usmiljenje je od roda do roda nad tistimi, ki se ga bojijo.
51 Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
S svojim laktom je pokazal moč, ponosne je razgnal v domišljiji njihovih src.
52 Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
Mogočne je odstranil z njihovih prestolov in povišal te z nizkim položajem.
53 Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
Lačne je napolnil z dobrinami, bogate pa je odpustil prazne.
54 Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
Pomagal je svojemu služabniku Izraelu, v spomin na svoje usmiljenje,
55 (kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
kakor je govoril našim očetom, Abrahamu in njegovemu semenu na veke.« (aiōn g165)
56 Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
Marija je z njo ostala približno tri mesece in se vrnila v svojo lastno hišo.
57 Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
Torej prišel je Elizabetin polni čas, ko naj bi rodila; in rodila je sina.
58 Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
Njeni sosedje in njeni sorodniki so slišali, kako je Gospod nad njo izkazal veliko usmiljenje in veselili so se z njo.
59 Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
Pripetilo pa se je, da so na osmi dan prišli, da obrežejo otroka in poimenovali so ga Zaharija, po imenu njegovega očeta.
60 Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
Njegova mati pa je odgovorila in rekla: »Ne tako, temveč se bo imenoval Janez.«
61 Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
Oni pa so ji rekli: »Nikogar v tvojem sorodstvu ni, ki je poimenovan s tem imenom.«
62 Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
In naredili so znamenja njegovemu očetu, kako bi ga on imenoval.
63 Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
In prosil je za pisalno deščico ter napisal, rekoč: »Njegovo ime je Janez.« In vsi so se čudili.
64 Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
In njegova usta so se takoj odprla in njegov jezik se je sprostil in spregovoril je ter hvalil Boga.
65 Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
In strah je prišel na vse, ki so prebivali naokoli njih; in vse te besede so se razglasile naokoli po vsej judejski hriboviti deželi.
66 Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
In vsi, ki so jih slišali, so si jih položili v svoja srca, rekoč: »Kakšne vrste otrok bo to!« In Gospodova roka je bila z njim.
67 Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
In njegov oče Zaharija je bil izpolnjen s Svetim Duhom in prerokoval, rekoč:
68 “Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
»Blagoslovljen bodi Gospod, Izraelov Bog; kajti obiskal je in odkupil svoje ljudi
69 Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
in za nas je dvignil rog rešitve duš v hiši svojega služabnika Davida,
70 kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
kakor je govoril po ustih svojih svetih prerokov, ki so bili, odkar je svet nastal, (aiōn g165)
71 Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
da bi bili mi lahko rešeni pred našimi sovražniki in iz roke vseh, ki nas sovražijo,
72 Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
da opravi usmiljenje, obljubljeno našim očetom in se spomni svoje svete zaveze,
73 kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
prisege, s katero je prisegel našemu očetu Abrahamu,
74 Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
da nam bo zagotovil, da mu bomo osvobojeni iz roke svojih sovražnikov, lahko služili brez strahu,
75 katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
v svetosti in pravičnosti pred njim, vse dni našega življenja.
76 Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
Ti pa, otrok, boš imenovan prerok Najvišjega, kajti šel boš pred Gospodov obraz, da pripraviš njegove poti,
77 kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
da daš njegovim ljudem spoznanje o rešitvi duš z odpuščanjem njihovih grehov,
78 Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
po nežnem usmiljenju našega Boga; po katerem nas je obiskalo svitanje od zgoraj,
79 kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
da da svetlobo tem, ki sedijo v temi in v smrtni senci, da vodi naša stopala na pot miru.«
80 Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.
Otrok pa je rasel in se krepil v duhu in bil je v puščavah do dneva njegove pojavitve Izraelu.

< Luka 1 >