< Mambo ya Walawi 8 >

1 Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
Yahweh spoke to Moses, saying,
2 “Walete Aroni na wanawe pamoja naye, mavazi na mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili, na kikapu cha mkate usio na hamira.
“Take Aaron and his sons with him, the garments and the anointing oil, the bull for the sin offering, the two rams, and the basket of unleavened bread.
3 Ita kusanyiko lote kwenye ingilio la hema la kukutania.”
Assemble all the assembly at the entrance to the tent of meeting.”
4 Kwa hiyo Musa akafanya kama Yahweh alivyomwamru, nalo kusanyiko lilikuja pamoja mbele ya ingilio la hema la kukutania. Kisha Musa akaliambia kusanyiko,
So Moses did as Yahweh commanded him, and the assembly came together at the entrance to the tent of meeting.
5 “Hivi ndivyo alivyotuamru Yahweh tutende.”
Then Moses said to the assembly, “This is what Yahweh has commanded to be done.”
6 Musa akamleta Aroni na wanawe na kuwaosha kwa maji.
Moses brought Aaron and his sons and washed them with water.
7 Akamvika Aroni kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini na kumfunga ukumbuu kiunoni mwake, akamvika joho la nje lenye mikono mirefu na kumvika kile kizibao chenye vipande viwili tumboni na mgongoni na kukifunga kuzunguka kiunoni mwake kwa mshipi uliosokotwa kwa ustadi na kukikaza mwilini mwake.
He put on Aaron the tunic and tied the sash around his waist, clothed him with the robe and put the ephod on him, and then he tied the ephod around him with the finely-woven waistband and bound it to him.
8 Kisha Musa akaweka kifuko kifuani mwa Aroni, na ndani ya kifuko hicho akaweka Urimu na Thumimu.
He placed the breastpiece on him, and in the breastpiece he put the Urim and the Thummim.
9 Na kisha akamfunga kiremba kichwani, na juu ya kiremba kwa mbele, akaweka bamba la dhahabu; liwe taji takatifu, kama Yahweh alivyomwamru yeye.
He set the turban on his head, and on the turban, in front, he set the golden plate, the holy crown, as Yahweh had commanded him.
10 Musa akayatwaa hayo mafuta ya upako, akalipaka lile hema la kukutania na kila kitu kilichokuwamo ndani yake na kuvitenga kwa ajili ya Yahweh.
Moses took the anointing oil, anointed the tabernacle and everything in it and set them apart to Yahweh.
11 Akayanyunyiza hayo mafuta juu ya madhabahu mara saba, na kisha akaipaka mafuta hiyo madhabahu na vyombo vyake vyote, na sinia la kunawia na kitako chake ili kuvitenga wa ajili ya Yahweh.
He sprinkled the oil on the altar seven times, and anointed the altar and all its utensils, and the washbasin and its base, to set them apart to Yahweh.
12 Akamimina sehemu ya mafuta ya upako juu ya kichwa cha Aroni na kisha akampaka mafuta ili kumtenga.
He poured some of the anointing oil on Aaron's head and anointed him to set him apart.
13 Musa akawaleta wana wa Aroni na kuwavika kila mmoja kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini. Kila mmoja wao akamfunga kwa ukumbuu kiunoni mwake na kuwafunga vitambaa vya kitani kichwani pao, kama vile Yahweh alivyokuwa amemru Musa.
Moses brought Aaron's sons and clothed them with tunics. He tied sashes around their waists and wrapped linen cloth around their heads, as Yahweh had commanded him.
14 Musa akamleta huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha fahali ambaye wamemelete kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Moses brought the bull for the sin offering, and Aaron and his sons laid their hands on the head of the bull that they had brought for the sin offering.
15 Musa akamchinja, na kisha akachukua sehemu ya damu yake kwa kidole chake na kuiweka juu ya mpembe za madhabahu, akaitakasa hiyo madhabahu, na kuitenga kwa Mungu, ambapo kwa kufanya hivyo, aliisababisha madhabahu kuwa sehemu ya kufaa kwa kufanyia upatanisho.
He killed it, and he took the blood and put it on the horns of the altar with his finger, purified the altar, poured out the blood at the base of the altar, and set it apart for God in order to make atonement for it.
16 Akachukua mafuta yote yaliyokuwa sehemu za ndani, kile kiwambo cha ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake, Musa akaichoma hiyo nyama yote juu ya madhabahu.
He took all the fat that was on the inner parts, the covering of the liver, and the two kidneys and their fat, and Moses burned it all on the altar.
17 Lakini yule fahali, ngozi yake, nyama yake na kinyesi chake, akavichoma nje ya kambi, kama vile Yehweh alivyokuwa amemwamru yeye.
But the bull, its hide, its meat, and its dung he burned outside the camp, as Yahweh had commanded him.
18 Musa akamleta yule konndoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo kondoo.
Moses presented the ram for the burnt offering, and Aaron and his sons laid their hands on the head of the ram.
19 Musa akamchinja kondoo na kuinyunyizia damu yake kila upande wa madhabahu.
He killed it and sprinkled its blood against every side of the altar.
20 Naye akamkatakata kondoo vipande vipande na akakiteketeza kichwa chake pamoja na vile vipande na mafuta.
He cut the ram into pieces and burned the head and the pieces and the fat.
21 Akaziosha kwa maji zile sehemu za ndani pamoja na miguu na akamteketeza kandoo mzima juu ya madhabahu. Ilikuwa ni dhabihu ya kuteketezwa na ilitoa harufu ya kupendeza, sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
He washed the inner parts and the legs with water, and he burned the whole ram on the altar. It was a burnt offering and produced a sweet aroma, an offering made by fire to Yahweh as Yahweh had commanded Moses.
22 Kisha Musa akamleta yule kondoo dume mwingine, kondoo wa kuwekwa wakfu, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo.
Then Moses presented the other ram, the ram of consecration, and Aaron and his sons laid their hands on the head of the ram.
23 Aroni akamchinja, naye Musa akachukua sehemu ya damu na kuiweka kwenye ncha ya sikio la Aroni la kulia, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye kidole kikumbwa cha mguu wake wa kulia.
Aaron killed it, and Moses took some of its blood and put it on the tip of Aaron's right ear, on the thumb of his right hand, and on the big toe of his right foot.
24 Akawaleta wana wa Aroni, naye akaweka sehemu ya damu ya kondoo yule kwenye ncha ya sikio lao la kulia, kwenye dole gumba lao cha mkono wa kulia na kwenye kidole chao kikubwa cha mguu wa kulia. Kisha Musa akainyunyiza damu ya huyo kila upande wa madhabahu
He brought Aaron's sons, and he put some of the blood on the tip of their right ear, on the thumb of their right hand, and on the big toe of their right foot. Then Moses sprinkled its blood against every side of the altar.
25 Naye akayatwaa yale mafuta, mafuta ya mkiani, mafuta liyolikuwa sehemu za ndani, na mafuta yafunikayo ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake na paja la kulia.
He took the fat, the fat tail, all the fat that was on the inner parts, the covering of the liver, the two kidneys and their fat, and the right thigh.
26 Akachukua mkate mmoja kutoka kwenye kikapu cha mikate isiyo na hamira ambayoo ilikuwa mbele za Yahweh, akatwaa mkate moja usio na hamira, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na mkate mwemba wa kaki na akaiweka juu ya mafuta na juu ya paja la kulia la kondoo.
Out of the basket of bread without yeast that was before Yahweh, he took one loaf without yeast, and one loaf of oiled bread, and one wafer, and placed them on the fat and on the right thigh.
27 Akaiweka yote mikoni mwa Aroni na katika mikono ya wanawe na kuitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa
He put it all in the hands of Aaron and in the hands of his sons and waved them before Yahweh as a wave offering.
28 Kisha Musa akaichukua mikate hiyo kutoka mikononi mwao na kuiteketeza juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Zilikuwa ni sadaka ya kuwekwa wakfu na ilitoa harufu ya kupendeza. Ilikuwa sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto.
Then Moses took them from off their hands and burned them on the altar for the burnt offering. They were a consecration offering and produced a sweet aroma. It was an offering made by fire to Yahweh.
29 Musa akakichukua kidari na kukitikisa kuwa sadaka ya kutikiswa kwa Yahweh. Ilikuwa ni mgao wa Musa wa kondoo wa kuwekewa mikono kwa makuhani, Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru yeye.
Moses took the breast and waved it as a wave offering to Yahweh. It was Moses' share of the ram for the priests' ordination, as Yahweh had commanded him.
30 Musa akatwaa sehemu ya mafuta ya upako na damu iliyokuwa juu ya madhabahu; naye akayanyunyiza haya juu ya nguo za Aroni, juu ya nguo zake mwenyewe na juu ya nguo za wana wa Aruni waliokua pamoja naye. Kwa njia hii alimtenga Aroni na nguo zake, na wanawe na nguo zao kwa ajili ya Yahweh.
Moses took some of the anointing oil and the blood that was on the altar; he sprinkled these on Aaron, on his clothes, on his sons, and on his sons' clothes with him. In this way he set apart Aaron and his clothes, and his sons and their clothes to Yahweh.
31 Kwa hiyo Musa akawambia Aruni na wanawe, “Ipikeni nyama mbele ya ingilio la hema la kukutania, na hapo mtaila pamoja na mkate ulio kwenye kikapu cha kuwekwa wakfu, kama ilivyoamriwa, kusema, 'Aroni na wanawe wataila.'
So Moses said to Aaron and to his sons, “Boil the meat at the entrance to the tent of meeting, and there eat it and the bread that is in the basket of consecration, as I commanded, saying, 'Aaron and his sons will eat it.'
32 Masalio yoyote ya nyama na mikate utayateketeza kwa moto.
Whatever remains of the meat and of the bread you must burn.
33 Na hamtatoka kwenye ingilio la hema la kukutania kwa muda wa siku saba, hata zitakapotimia siku za kuwekwa mikono kwenu. Kwa kuwa kwa muda wa siku saba, Yahweh atawaweka wakfu.
You must not go out from the entrance of the tent of meeting for seven days, until the days of your ordination are fulfilled. For Yahweh will consecrate you for seven days.
34 Kilichotendeka siku hii— Yahweh ndiye amekiamru kitendekeke ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
What has been done this day— Yahweh has commanded to be done to make atonement for you.
35 Mtakaa kwenye ingilio la hema la kukutania mchana na usiku siku saba, nanyi ishikeni amri ya Yahweh ili msije mkafa, kwa sababu hivi ndivyo ilivyoamriwa.
You will stay day and night for seven days at the entrance to the tent of meeting, and keep the command of Yahweh, so you will not die, because this is what I have been commanded.”
36 Kwa hiyo Aroni na wanawe wakafanya mambo yote ambayo Yahweh alikuwa amewaamru kwa kinywa cha Musa.
So Aaron and his sons did all the things which Yahweh had commanded them through Moses.

< Mambo ya Walawi 8 >