< Mambo ya Walawi 8 >

1 Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “Walete Aroni na wanawe pamoja naye, mavazi na mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili, na kikapu cha mkate usio na hamira.
Take Aaron and sons his with him and the garments and [the] oil of anointing and - [the] bull of the sin offering and [the] two the rams and [the] basket of unleavened bread.
3 Ita kusanyiko lote kwenye ingilio la hema la kukutania.”
And all the congregation assemble to [the] entrance of [the] tent of meeting.
4 Kwa hiyo Musa akafanya kama Yahweh alivyomwamru, nalo kusanyiko lilikuja pamoja mbele ya ingilio la hema la kukutania. Kisha Musa akaliambia kusanyiko,
And he did Moses just as he had commanded Yahweh him and it assembled the congregation to [the] entrance of [the] tent of meeting.
5 “Hivi ndivyo alivyotuamru Yahweh tutende.”
And he said Moses to the congregation this [is] the word which he has commanded Yahweh to do.
6 Musa akamleta Aroni na wanawe na kuwaosha kwa maji.
And he presented Moses Aaron and sons his and he washed them with water.
7 Akamvika Aroni kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini na kumfunga ukumbuu kiunoni mwake, akamvika joho la nje lenye mikono mirefu na kumvika kile kizibao chenye vipande viwili tumboni na mgongoni na kukifunga kuzunguka kiunoni mwake kwa mshipi uliosokotwa kwa ustadi na kukikaza mwilini mwake.
And he put on him the tunic and he girded him with the sash and he clothed him the robe and he put on him the ephod and he girded him with [the] girdle of the ephod and he girded [the] ephod to him with it.
8 Kisha Musa akaweka kifuko kifuani mwa Aroni, na ndani ya kifuko hicho akaweka Urimu na Thumimu.
And he placed on him the breastpiece and he put into the breastpiece the Urim and the Thummim.
9 Na kisha akamfunga kiremba kichwani, na juu ya kiremba kwa mbele, akaweka bamba la dhahabu; liwe taji takatifu, kama Yahweh alivyomwamru yeye.
And he placed the turban on head his and he placed on the turban to [the] front of face his [the] plate of gold [the] crown of holiness just as he had commanded Yahweh Moses.
10 Musa akayatwaa hayo mafuta ya upako, akalipaka lile hema la kukutania na kila kitu kilichokuwamo ndani yake na kuvitenga kwa ajili ya Yahweh.
And he took Moses [the] oil of anointing and he anointed the tabernacle and all that [was] in it and he set apart as holy them.
11 Akayanyunyiza hayo mafuta juu ya madhabahu mara saba, na kisha akaipaka mafuta hiyo madhabahu na vyombo vyake vyote, na sinia la kunawia na kitako chake ili kuvitenga wa ajili ya Yahweh.
And he spattered some of it on the altar seven times and he anointed the altar and all utensils its and the laver and base its to set apart as holy them.
12 Akamimina sehemu ya mafuta ya upako juu ya kichwa cha Aroni na kisha akampaka mafuta ili kumtenga.
And he poured some of [the] oil of anointing on [the] head of Aaron and he anointed him to set apart as holy him.
13 Musa akawaleta wana wa Aroni na kuwavika kila mmoja kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini. Kila mmoja wao akamfunga kwa ukumbuu kiunoni mwake na kuwafunga vitambaa vya kitani kichwani pao, kama vile Yahweh alivyokuwa amemru Musa.
And he presented Moses [the] sons of Aaron and he clothed them tunics and he girded them a sash and he bound on to them headdresses just as he had commanded Yahweh Moses.
14 Musa akamleta huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha fahali ambaye wamemelete kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
And he brought near [the] bull of the sin offering and he leaned Aaron and sons his hands their on [the] head of [the] bull of the sin offering.
15 Musa akamchinja, na kisha akachukua sehemu ya damu yake kwa kidole chake na kuiweka juu ya mpembe za madhabahu, akaitakasa hiyo madhabahu, na kuitenga kwa Mungu, ambapo kwa kufanya hivyo, aliisababisha madhabahu kuwa sehemu ya kufaa kwa kufanyia upatanisho.
And he cut [the] throat of [it] and he took Moses the blood and he put [it] on [the] horns of the altar all around with finger his and he cleansed from sin the altar and the blood he poured to [the] base of the altar and he set apart as holy it to make atonement on it.
16 Akachukua mafuta yote yaliyokuwa sehemu za ndani, kile kiwambo cha ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake, Musa akaichoma hiyo nyama yote juu ya madhabahu.
And he took all the fat which [was] on the entrails and [the] lobe of the liver and [the] two the kidneys and fat their and he made [them] smoke Moses the altar towards.
17 Lakini yule fahali, ngozi yake, nyama yake na kinyesi chake, akavichoma nje ya kambi, kama vile Yehweh alivyokuwa amemwamru yeye.
And the bull and hide its and flesh its and offal its he burned with fire from [the] outside of the camp just as he had commanded Yahweh Moses.
18 Musa akamleta yule konndoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo kondoo.
And he presented [the] ram of the burnt offering and they leaned Aaron and sons his hands their on [the] head of the ram.
19 Musa akamchinja kondoo na kuinyunyizia damu yake kila upande wa madhabahu.
And he cut [the] throat of [it] and he sprinkled Moses the blood on the altar all around.
20 Naye akamkatakata kondoo vipande vipande na akakiteketeza kichwa chake pamoja na vile vipande na mafuta.
And the ram he cut in pieces into pieces its and he made smoke Moses the head and the pieces and the suet.
21 Akaziosha kwa maji zile sehemu za ndani pamoja na miguu na akamteketeza kandoo mzima juu ya madhabahu. Ilikuwa ni dhabihu ya kuteketezwa na ilitoa harufu ya kupendeza, sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
And the entrails and the legs he washed with water and he made smoke Moses all the ram the altar towards [was] a burnt offering it to an odor of soothing [was] a fire offering it to Yahweh just as he had commanded Yahweh Moses.
22 Kisha Musa akamleta yule kondoo dume mwingine, kondoo wa kuwekwa wakfu, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo.
And he presented the ram second [the] ram of installation offering and they leaned Aaron and sons his hands their on [the] head of the ram.
23 Aroni akamchinja, naye Musa akachukua sehemu ya damu na kuiweka kwenye ncha ya sikio la Aroni la kulia, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye kidole kikumbwa cha mguu wake wa kulia.
And he cut [the] throat of [it] - and he took Moses some of blood its and he put [it] on [the] lobe of [the] ear of Aaron right and on [the] thumb of hand his right and on [the] big toe of foot his right.
24 Akawaleta wana wa Aroni, naye akaweka sehemu ya damu ya kondoo yule kwenye ncha ya sikio lao la kulia, kwenye dole gumba lao cha mkono wa kulia na kwenye kidole chao kikubwa cha mguu wa kulia. Kisha Musa akainyunyiza damu ya huyo kila upande wa madhabahu
And he presented [the] sons of Aaron and he put Moses some of the blood on [the] lobe of ear their right and on [the] thumb of hand their right and on [the] big toe of foot their right and he sprinkled Moses the blood on the altar all around.
25 Naye akayatwaa yale mafuta, mafuta ya mkiani, mafuta liyolikuwa sehemu za ndani, na mafuta yafunikayo ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake na paja la kulia.
And he took the fat and the fat tail and all the fat which [was] on the entrails and [the] lobe of the liver and [the] two the kidneys and fat their and [the] thigh of the right.
26 Akachukua mkate mmoja kutoka kwenye kikapu cha mikate isiyo na hamira ambayoo ilikuwa mbele za Yahweh, akatwaa mkate moja usio na hamira, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na mkate mwemba wa kaki na akaiweka juu ya mafuta na juu ya paja la kulia la kondoo.
And from [the] basket of unleavened bread which - [was] before Yahweh he took a round perforated bread of unleavened bread one and a round perforated bread of bread of oil one and a thin bread one and he placed [them] on the fat and on [the] thigh of the right.
27 Akaiweka yote mikoni mwa Aroni na katika mikono ya wanawe na kuitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa
And he put everything on [the] palms of Aaron and on [the] palms of sons his and he waved them a wave-offering before Yahweh.
28 Kisha Musa akaichukua mikate hiyo kutoka mikononi mwao na kuiteketeza juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Zilikuwa ni sadaka ya kuwekwa wakfu na ilitoa harufu ya kupendeza. Ilikuwa sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto.
And he took Moses them from on palms their and he made [them] smoke the altar towards on the burnt offering [were] installation offerings they to an odor of soothing [was] a fire offering it to Yahweh.
29 Musa akakichukua kidari na kukitikisa kuwa sadaka ya kutikiswa kwa Yahweh. Ilikuwa ni mgao wa Musa wa kondoo wa kuwekewa mikono kwa makuhani, Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru yeye.
And he took Moses the breast and he waved it a wave-offering before Yahweh from [the] ram of installation offering to Moses it belonged to a portion just as he had commanded Yahweh Moses.
30 Musa akatwaa sehemu ya mafuta ya upako na damu iliyokuwa juu ya madhabahu; naye akayanyunyiza haya juu ya nguo za Aroni, juu ya nguo zake mwenyewe na juu ya nguo za wana wa Aruni waliokua pamoja naye. Kwa njia hii alimtenga Aroni na nguo zake, na wanawe na nguo zao kwa ajili ya Yahweh.
And he took Moses some of [the] oil of anointing and some of the blood which [was] on the altar and he spattered [it] on Aaron on garments his and on sons his and on [the] garments of sons his with him and he set apart as holy Aaron garments his and sons his and [the] garments of sons his with him.
31 Kwa hiyo Musa akawambia Aruni na wanawe, “Ipikeni nyama mbele ya ingilio la hema la kukutania, na hapo mtaila pamoja na mkate ulio kwenye kikapu cha kuwekwa wakfu, kama ilivyoamriwa, kusema, 'Aroni na wanawe wataila.'
And he said Moses to Aaron and to sons his boil the meat [the] entrance of [the] tent of meeting and there you will eat it and the bread which [is] in [the] basket of the installation offering just as I commanded saying Aaron and sons his they will eat it.
32 Masalio yoyote ya nyama na mikate utayateketeza kwa moto.
And the remainder in the meat and in the bread with fire you will burn.
33 Na hamtatoka kwenye ingilio la hema la kukutania kwa muda wa siku saba, hata zitakapotimia siku za kuwekwa mikono kwenu. Kwa kuwa kwa muda wa siku saba, Yahweh atawaweka wakfu.
And from [the] entrance of [the] tent of meeting not you must go out seven days until [the] day are completed [the] days of installation your for seven days he will fill hand your.
34 Kilichotendeka siku hii— Yahweh ndiye amekiamru kitendekeke ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
Just as someone has done on the day this he has commanded Yahweh to do to make atonement on you.
35 Mtakaa kwenye ingilio la hema la kukutania mchana na usiku siku saba, nanyi ishikeni amri ya Yahweh ili msije mkafa, kwa sababu hivi ndivyo ilivyoamriwa.
And [the] entrance of [the] tent of meeting you will remain by day and night seven days and you will keep [the] duty of Yahweh and not you will die for thus I have been commanded.
36 Kwa hiyo Aroni na wanawe wakafanya mambo yote ambayo Yahweh alikuwa amewaamru kwa kinywa cha Musa.
And he did Aaron and sons his all the things which he had commanded Yahweh by [the] hand of Moses.

< Mambo ya Walawi 8 >