< Mambo ya Walawi 6 >

1 Bwana alisema na Musa kumwabia,
And the Lord spoke to Moses, saying,
2 “Kama mtu akifanya dhambi na kuvunja amri kinyume na Bwana, kama kujihusisha na uongo dhidi ya jirani yake kuhusu kitu fulani cha kutokuwa mwaminifu, au kama akidanganya au kuiba au amemdhurumu jirani.
The soul which shall have sinned, and willfully overlooked the commandments of the Lord, and shall have dealt falsely in the affairs of his neighbor in the matter of a deposit, or concerning fellowship, or concerning plunder, or has in anything wronged his neighbor,
3 Au akiokota kitu fulani ambacho jirani yake amepoteza na kusema uongo kuhusu hicho, na kuapa kwa uongo au kwa mambo kama haya ambayo watu wanaweza kutenda dhambi.
or has found that which was lost, and shall have lied concerning it, and shall have sworn unjustly concerning [any] one of all the things, whatever a man may do, so as to sin hereby;
4 Ndipo itakuwa hivi, kama ametenda dhambi na hatia, kwamba lazima akirudishe kwa vyovyote alichoiba au kudanganya au amedhurumu au kitu kilichopotea naye kukiokota.
it shall come to pass, whenever he shall have sinned, and transgressed, that he shall restore the plunder which he has seized, or [redress] the injury which he has committed, or restore the deposit which was entrusted to him, or the lost article which he has found of any kind, about which he swore unjustly, he shall even restore it in full; and he shall add to it a fifth part besides; he shall restore it to him whose it is in the day in which he happens to be convicted.
5 Au kama amedanganya kwa jambo lolote, lazima atakirudisha kamilina kuongezea sehemu ya tano kwa kumlipa anayedai, kwa siku ile anayopatikana na hatia.
And he shall bring to the Lord for his trespass, a ram of the flock, without blemish, of value to the amount of the thing in which he trespassed.
6 Ataleta sadka ya hatia kwa Bwana: kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi lake kulingana na thamani yake, kama sadaka ya hatia kwa kuhani.
And the priest shall make atonement for him before the Lord, and he shall be forgiven for any one of all the things which he did and trespassed in it.
7 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele ya Bwana, atakuwa amesamehewa kulingana na chochote kilicho mfanya kuwa na hatia.”
And the Lord spoke to Moses, saying,
8 Ndipo Bwana alisema na Musa kumwambia,
Charge Aaron and his sons, saying,
9 “Mwagize Haruni na wanawe, kusema, 'hii ni sheria ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa lazima iwe juu ya makaa ya madhabahu usiku wote hata asubuhi, na moto wa madhabahu utaendelea kuwaka.
This [is] the law of whole burnt offering; this is the whole burnt offering in its burning on the altar all the night till the morning; and the fire of the altar shall burn on it, it shall not be put out.
10 Kuhani atavaa nguo zake za kitani na atavaa nguo za kitani ndani yake. Atatoa majivu yaliyobaki baada ya moto kutekeza sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu, na ataweka majivu pembeni mwa madhabahu.
And the priest shall put on the linen tunic, and he shall put the linen drawers on his body; and shall take away that which has been thoroughly burnt, which the fire shall have consumed, even the whole burnt offering from the altar, and he shall put it near the altar.
11 Atavua mavazi haya na kuvaa mavazi mengine ili kuchukua majivu nje ya kambi na kupeleka mahali palipo safi.
And he shall put off his robe, and put on another robe, and he shall take forth the offering that has been burnt without the camp into a clean place.
12 Moto katika madhabahu utaendelea kuwaka. Usizimike, na kuhani ataongeza kuni kila asubuhi. Atapanga juu yake sadaka ya kuteketezwa kama inavyotakiwa, na atateketeza juu yake mafuta ya sadaka ya amani.
And the fire on the altar shall be kept burning on it, and shall not be extinguished; and the priest shall burn on it wood every morning, and shall heap on it the whole burnt offering, and shall lay on it the fat of the peace-offering.
13 Moto lazima utaendelea kuwaka katika madhabahu, kamwe usizimike.
And the fire shall always burn on the altar; it shall not be extinguished.
14 Hii ni sheria ya sadaka ya nafaka. Wana wa Haruni watatoa mbele ya Bwana katika madhabahu.
This is the law of the sacrifice, which the sons of Aaron shall bring near before the Lord, before the altar.
15 Kuhani atachukua konzi ya unga laini wa sadaka ya nafaka na mafuta na ubani ambao uko juu ya sadaka ya nafaka, atateketeza juu ya madhabahu kuleta harufu nzuri ya shukrani ya kumpendeza Bwana.
And he shall take from it a handful of the fine flour of the sacrifice with its oil, and with all its frankincense, which are upon the sacrifice; and he shall offer up on the altar a burnt offering as a sweet smelling savor, a memorial of it to the Lord.
16 Haruni na wanae watakula sadaka inayobaki, italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu. Watakula katika ua ya hema ya kukutania.
And Aaron and his sons shall eat that which is left of it: it shall be eaten without leaven in a holy place, they shall eat it in the court of the tabernacle of witness.
17 Haitaokwa pamoja na chachu. Nimewapa kama sehemu ya sadaka yangu itolewayo kwa moto, ni takatifu sana, kama sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
It shall not be baked with leaven. I have given it as a portion to them of the burnt offerings of the Lord: it is most holy, as the offering for sin, and as the offering for trespass.
18 Kwa nyakati zote zijazo kupitia watu wa kizazi chako, mwanaume yeyote mzaliwa kutoka kwa Haruni aweza kula ni sehemu yake, ichukuliwayo katika sadaka ya Bwana kwa moto. Yeyote anayeigusa atakuwa mtakatifu.”
Every male of the priests shall eat it: it is a perpetual ordinance throughout your generations of the burnt offerings of the Lord; whoever shall touch them shall be hallowed.
19 Bwana aliongea tena na Musa kumwambia,
And the Lord spoke to Moses, saying,
20 “Hii ni sadaka ya Haruni na wanawe ambayo watatoa kwa Bwana katika siku ambayo kila mwana atawekwa wakfu: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama kawaida sadaka ya nafaka nusu yake asubuhi na nusu yake jioni.
This is the gift of Aaron and of his sons, which they shall offer to the Lord in the day in which you shall anoint him; the tenth of an ephah of fine flour for a sacrifice continually, the half of it in the morning, and the half of it in the evening.
21 Itatengenezwa na mafuta katika kikaango, utaileta ikiwa imeandaliwa imeokwa katika vipande utatoa sadaka ya nafaka ili kuleta harufu nzuri kwa Bwana.
It shall be made with oil in a frying-pan; he shall offer it kneaded [and] in rolls, an offering of fragments, an offering of a sweet savor to the Lord.
22 Mwana wa Kuhani Mkuu atakayekuwa Kuhani Mkuu mpya kutoka miongoni mwa wanawe ataitoa. Kama amri ya milele, yote itateketezwa kwa Bwana.
The anointed priest who is in his place, [one] of his sons, shall offer it: it is a perpetual statute, it shall all be consumed.
23 Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itatekezwa yote. Haitaliwa kamwe.”
And every sacrifice of a priest shall be thoroughly burnt, and shall not be eaten.
24 Bwana alisema tena Musa, kumwambia,
And the Lord spoke to Moses, saying,
25 “Sema na Haruni na watoto wake kwamba, 'Hii ni sheria ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi lazima kuchinjwa mahali pa sadaka ya kuteketezwa itachinjwa mbeleya Bwana. Ni takatifu sana.
Speak to Aaron and to his sons, saying, This is the law of the sin-offering; —in the place where they kill the whole burnt offering, they shall kill the sin-offerings before the Lord: they are most holy.
26 Kuhani atakayeitoa kwa ajili ya dhambi ndiye atakayeila. Italiwa mahali patakatifu katika ua wa hema ya kukutania.
The priest that offers it shall eat it: in a holy place it shall be eaten, in the court of the tabernacle of witness.
27 Yeyote atakayeigusa nyama yake atakuwa ni mtakatifu na kama damu itadondokea mavazi yatafuliwa mahali palipodondokewa, mahali patakatifu.
Every one that touches the flesh of it shall be holy, and on whoever’s garment any of its blood shall have been sprinkled, whoever shall have it sprinkled, shall be washed in the holy place.
28 Lakini chungu kikipikiwa kitavunjwa, kama imepikiwa katika chombo cha shaba, lazima kitasuguliwa na kusafishwa kwa maji.
And the earthen vessel, in whichever it shall have been sodden, shall be broken; and if it shall have been sodden in a brazen vessel, he shall scour it and wash it with water.
29 Mwanaume yeyote miongoni mwa makuhani anaweza kula nyama hiyo kwa sababu ni takatifu sana.
Every male among the priests shall eat it: it is most holy to the Lord.
30 Na hakuna sadaka ya dhambi italiwa ambayo damu yake imeletwa katika hema ya kukutania kufanya upatanisho katika mahali patakatifu. Ni lazima iteketezwe.
And no offerings for sin, of whose blood there shall be brought any into the tabernacle of witness to make atonement in the holy place, shall be eaten: they shall be burned with fire.

< Mambo ya Walawi 6 >