< Mambo ya Walawi 6 >

1 Bwana alisema na Musa kumwabia,
The Lord spoke to Moses, saying:
2 “Kama mtu akifanya dhambi na kuvunja amri kinyume na Bwana, kama kujihusisha na uongo dhidi ya jirani yake kuhusu kitu fulani cha kutokuwa mwaminifu, au kama akidanganya au kuiba au amemdhurumu jirani.
The soul who will have sinned, and, despising the Lord, will have denied to his neighbor the deposit which he had entrusted to his safekeeping, or who will have extorted anything by force, or who will have made a false accusation,
3 Au akiokota kitu fulani ambacho jirani yake amepoteza na kusema uongo kuhusu hicho, na kuapa kwa uongo au kwa mambo kama haya ambayo watu wanaweza kutenda dhambi.
or who will have found a lost thing and then also withheld it by swearing falsely, or who will have done any other of the many things by which men usually sin:
4 Ndipo itakuwa hivi, kama ametenda dhambi na hatia, kwamba lazima akirudishe kwa vyovyote alichoiba au kudanganya au amedhurumu au kitu kilichopotea naye kukiokota.
being convicted of the offense, he shall restore
5 Au kama amedanganya kwa jambo lolote, lazima atakirudisha kamilina kuongezea sehemu ya tano kwa kumlipa anayedai, kwa siku ile anayopatikana na hatia.
all that he wanted to obtain by fraud, the whole plus an additional fifth part, to the owner against whom he brought the damage.
6 Ataleta sadka ya hatia kwa Bwana: kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi lake kulingana na thamani yake, kama sadaka ya hatia kwa kuhani.
Then, on behalf of his sin, he shall offer an immaculate ram from the flock, and he shall give it to the priest, according to the estimation and measure of the offense.
7 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele ya Bwana, atakuwa amesamehewa kulingana na chochote kilicho mfanya kuwa na hatia.”
And he shall pray for him in the sight of the Lord, and he shall be released from any one of those things that he did when he sinned.
8 Ndipo Bwana alisema na Musa kumwambia,
And the Lord spoke to Moses, saying:
9 “Mwagize Haruni na wanawe, kusema, 'hii ni sheria ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa lazima iwe juu ya makaa ya madhabahu usiku wote hata asubuhi, na moto wa madhabahu utaendelea kuwaka.
Instruct Aaron and his sons: This is the law of a holocaust. It shall be burned upon the altar, all night until morning. The fire shall be from the same altar.
10 Kuhani atavaa nguo zake za kitani na atavaa nguo za kitani ndani yake. Atatoa majivu yaliyobaki baada ya moto kutekeza sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu, na ataweka majivu pembeni mwa madhabahu.
The priest shall be vested with the tunic and the linen undergarments. And he shall take up the ashes of that which the devouring fire has consumed, and, placing them next to the altar,
11 Atavua mavazi haya na kuvaa mavazi mengine ili kuchukua majivu nje ya kambi na kupeleka mahali palipo safi.
he shall strip off his former vestments, and being clothed with others, he shall carry them beyond the camp, and he shall cause them to be consumed, even to glowing embers, in a very clean place.
12 Moto katika madhabahu utaendelea kuwaka. Usizimike, na kuhani ataongeza kuni kila asubuhi. Atapanga juu yake sadaka ya kuteketezwa kama inavyotakiwa, na atateketeza juu yake mafuta ya sadaka ya amani.
But the fire on the altar shall burn always, for the priest shall nourish it by placing wood under it each day in the morning. And, laying down the holocaust, he shall burn the fat of the peace offerings upon it.
13 Moto lazima utaendelea kuwaka katika madhabahu, kamwe usizimike.
This is the perpetual fire which shall never fail upon the altar.
14 Hii ni sheria ya sadaka ya nafaka. Wana wa Haruni watatoa mbele ya Bwana katika madhabahu.
This is the law of the sacrifice and the libations, which the sons of Aaron shall offer in the sight of the Lord, and before the altar.
15 Kuhani atachukua konzi ya unga laini wa sadaka ya nafaka na mafuta na ubani ambao uko juu ya sadaka ya nafaka, atateketeza juu ya madhabahu kuleta harufu nzuri ya shukrani ya kumpendeza Bwana.
The priest shall take a handful of fine wheat flour, which has been sprinkled with oil, and all the frankincense, which has been placed upon the flour, and he shall burn it upon the altar as a memorial of most sweet odor to the Lord.
16 Haruni na wanae watakula sadaka inayobaki, italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu. Watakula katika ua ya hema ya kukutania.
And the remaining portion of the flour, Aaron shall eat with his sons, without leaven. And he shall eat it in the holy place, in the atrium of the tabernacle.
17 Haitaokwa pamoja na chachu. Nimewapa kama sehemu ya sadaka yangu itolewayo kwa moto, ni takatifu sana, kama sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
Yet for this reason, it shall not be leavened, because part of it is offered as an incense of the Lord. The Holy of holies shall it be, just as what is offered on behalf of sin and of transgression.
18 Kwa nyakati zote zijazo kupitia watu wa kizazi chako, mwanaume yeyote mzaliwa kutoka kwa Haruni aweza kula ni sehemu yake, ichukuliwayo katika sadaka ya Bwana kwa moto. Yeyote anayeigusa atakuwa mtakatifu.”
Only the males of the stock of Aaron shall eat it. This shall be an everlasting ordinance in your generations concerning the sacrifices of the Lord. All who will touch these shall be sanctified.
19 Bwana aliongea tena na Musa kumwambia,
And the Lord spoke to Moses, saying:
20 “Hii ni sadaka ya Haruni na wanawe ambayo watatoa kwa Bwana katika siku ambayo kila mwana atawekwa wakfu: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama kawaida sadaka ya nafaka nusu yake asubuhi na nusu yake jioni.
This is the oblation of Aaron and of his sons, which they must offer to the Lord in the day of their anointing. They shall offer a tenth part of an ephah of fine wheat flour as a perpetual sacrifice, half of it in the morning, and half of it in the evening.
21 Itatengenezwa na mafuta katika kikaango, utaileta ikiwa imeandaliwa imeokwa katika vipande utatoa sadaka ya nafaka ili kuleta harufu nzuri kwa Bwana.
It shall be sprinkled with oil and fried in a frying pan. Then it shall be offered hot, as a most sweet odor to the Lord,
22 Mwana wa Kuhani Mkuu atakayekuwa Kuhani Mkuu mpya kutoka miongoni mwa wanawe ataitoa. Kama amri ya milele, yote itateketezwa kwa Bwana.
by the priest who by law succeeds his father. And it shall be entirely burned on the altar.
23 Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itatekezwa yote. Haitaliwa kamwe.”
For every sacrifice of the priest shall be consumed by fire; neither shall anyone eat from it.
24 Bwana alisema tena Musa, kumwambia,
Then the Lord spoke to Moses, saying:
25 “Sema na Haruni na watoto wake kwamba, 'Hii ni sheria ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi lazima kuchinjwa mahali pa sadaka ya kuteketezwa itachinjwa mbeleya Bwana. Ni takatifu sana.
Say to Aaron and his sons: This is the law of the victim for sin. In the place where the holocaust is offered, it shall be immolated in the sight of the Lord. It is the Holy of holies.
26 Kuhani atakayeitoa kwa ajili ya dhambi ndiye atakayeila. Italiwa mahali patakatifu katika ua wa hema ya kukutania.
The priest who offers it shall eat it in the holy place, in the atrium of the tabernacle.
27 Yeyote atakayeigusa nyama yake atakuwa ni mtakatifu na kama damu itadondokea mavazi yatafuliwa mahali palipodondokewa, mahali patakatifu.
Whatever will touch its flesh shall be sanctified. If a garment will be sprinkled with its blood, it shall be washed in a holy place.
28 Lakini chungu kikipikiwa kitavunjwa, kama imepikiwa katika chombo cha shaba, lazima kitasuguliwa na kusafishwa kwa maji.
Then the earthen vessel, in which it was soaked, shall be broken. But if the vessel will be of brass, it shall be scoured and washed with water.
29 Mwanaume yeyote miongoni mwa makuhani anaweza kula nyama hiyo kwa sababu ni takatifu sana.
Every male of priestly descent shall feed on its flesh, because it is the Holy of holies.
30 Na hakuna sadaka ya dhambi italiwa ambayo damu yake imeletwa katika hema ya kukutania kufanya upatanisho katika mahali patakatifu. Ni lazima iteketezwe.
For the victim that is slain for sin, whose blood is carried into the tabernacle of the testimony, for expiation in the Sanctuary, shall not be eaten, but it shall be consumed by fire.

< Mambo ya Walawi 6 >