< Mambo ya Walawi 14 >

1 Yahwe alizungumza na Musa, akisema,
Yahweh spoke to Moses, saying,
2 “Hii itakuwa sheria kwaajili ya mtu aliyekufa kwenye siku ya utakaso. Lazima aletwe kwa kuhani.
“This will be the law for the diseased person on the day of his cleansing. He must be brought to the priest.
3 Kuhani atakwenda nje ya kambi kumchunguza mtu kuona kama madhara ya ugonjwa wa ngozi yameponywa.
The priest will go out of the camp to examine the person to see if the infectious skin disease is healed.
4 Ndipo kuhani ataamuru kwamba mtu mwenye kutakaswa lazima achukue ndege safi wawili, waliohai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
Then the priest will command that the one to be cleansed must take two live, clean birds, cedar wood, scarlet yarn, and hyssop.
5 Kuhani atamwamuru kuua moja ya hao ndege juu ya maji safi yaliyo kwenye chungu cha udongo.
The priest will command him to kill one of the birds over fresh water that is in a clay pot.
6 Ndipo kuhani atamchukua ndege aliyehai na mti wa mwerezi, na kitani nyekundu na hisopo, na vyote hivi, pamoja na ndege aliyehai atavichovya kwenye damu ya ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
The priest will then take the live bird and the cedar wood, and the scarlet yarn and the hyssop, and he will dip all these things, including the live bird, in the blood of the bird that was killed over the fresh water.
7 Ndipo kuhani atanyunyiza maji haya mara saba juu ya mtu anayetakaswa katika ugonjwa, na ndipo kuhani atamtangaza kuwa msafi. Ndipo kuhani atamwachia ndege aliyehai katika eneo wazi.
Then the priest will sprinkle this water seven times onto the person who is to be cleansed from the disease, and then the priest will pronounce him to be clean. Then the priest will release the living bird into the open fields.
8 Mtu aliyetakaswa atafua nguo zake, atanyoa nywele zake zote, ataoga kwa maji, na ndipo atakuwa safi. Baada ya hayo lazima aje kwenye kambi, lakini ataishi nje ya hema lake kwa siku saba.
The person who is being cleansed will wash his clothes, shave off all his hair, and bathe himself in water, and then he will be clean. After that he must come into the camp, but he will live outside his tent for seven days.
9 Katika siku ya saba lazima anyoe nywele za kichwa chake, na lazima pia anyoe ndevu zake na nyusi. Lazima anyoe nywele zake zote, na lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji; ndipo atakuwa safi.
On the seventh day he must shave all his hair off his head, and he must also shave off his beard and eyebrows. He must shave off all his hair, and he must wash his clothes and bathe himself in water; then he will be clean.
10 Katika siku ya nane lazima achukue dume wa wana kondoo wawili wasio na lawama, mwana kondoo jike wa mwaka mmoja asiye na lawama, na tatu ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa mafuta kama sadaka ya nafaka, na kipimo kimoja cha mafuta.
On the eighth day he must take two male lambs without blemish, one female lamb a year old without blemish, and three-tenths of an ephah of fine flour mixed with oil as a grain offering, and one log of oil.
11 Kuhani ambaye amemtakasa mtu atamsimamisha mtu ambaye aliyemtakasa, pamoja na vile vitu, mbele ya Yahwe mahali pa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
The priest who cleanses him will stand the person who is to be cleansed, along with those things, before Yahweh at the entrance to the tent of meeting.
12 Kuhani atachukua mmoja wa wanakondoo dume na kumtoa kama sadaka ya hatia, pamoja na kipimo cha mafuta; atavitikisa kwa sadaka ya kutikiswa mbele ya Yahwe.
The priest will take one of the male lambs and offer it as a guilt offering, together with the log of oil; he will wave them for a wave offering before Yahweh.
13 Lazima aue mwana kondoo dume mahali ambapo wanapochinjia sadaka ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa, katika eneo la hema, sababu sadaka ya dhambi ni ya kuhani, kama afanyavyo sadaka ya hatia, kwasababu ni takatifu zaidi.
He must kill the male lamb in the place where they kill the sin offerings and the burnt offerings, in the area of the tabernacle, for the sin offering belongs to the priest, as does the guilt offering, because it is most holy.
14 Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu yule wa kutakaswa, katika dole gumba la kulia, katika dole la mguu wa kulia.
The priest will take some of the blood of the guilt offering and put it on the tip of the right ear of the person who is to be cleansed, on the thumb of his right hand, and on the big toe of his right foot.
15 Ndipo kuhani atachukua mafuta kutoka chombo na kuyamimina katika kiganja cha mkono wake wa kushoto, na kuzamisha kidole chake katika mafuta hayo yaliyo kwenye mkono wa kushoto,
Then the priest will take oil from the log and pour it into the palm of his own left hand,
16 na kunyunyiza baadhi ya mafuta kwa kidole mara saba mbele za Yahwe.
and dip his right finger in the oil that is in his left hand, and sprinkle some of the oil with his finger seven times before Yahweh.
17 kuhani ataweka mafuta yaliyobaki kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu wa kutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wa kulia, na katika dole kubwa la mguu wa kulia. Lazima aweke mafuta haya juu ya damu kutoka kwenye sadaka ya hatia.
The priest will put the rest of the oil in his hand on the tip of the right ear of the person to be cleansed, on the thumb of his right hand, and on the big toe of his right foot. He must put this oil on top of the blood from the guilt offering.
18 Kama kwa mafuta yaliyosalia kwamba katika mkono wa kuhani, atayaweka juu ya kichwa cha mtu ambaye atakaswaye, na kuhani atafanya utakaso kwaajili yake mbele za Yahwe.
As for the rest of the oil that is in the priest's hand, he will put it on the head of the person who is to be cleansed, and the priest will make atonement for him before Yahweh.
19 Ndipo kuhani atatoa sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwaajili yake atakaswaye kwa sababu ya kutokuwa safi kwake, na badaye ataua sadaka ya kuchomwa.
Then the priest will offer the sin offering and make atonement for him who is to be cleansed because of his uncleanness, and afterward he will kill the burnt offering.
20 Ndipo kuhani atatoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka juu ya madhabahu. Kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya mtu huyo, na ndipo atakuwa safi.
Then the priest will offer the burnt offering and the grain offering on the altar. The priest will make atonement for the person, and then he will be clean.
21 Kwa namna hiyo, kama mtu ni masikini na hawezi kumudu matoleo haya, ndipo anaweza kuchukua kondoo mmoja dume kama sadaka ya hatia ya kutikiswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe, na moja ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka, na chombo cha mafuta,
However, if the person is poor and cannot afford these sacrifices, then he may take one male lamb as a guilt offering to be waved, to make atonement for himself, and one-tenth of an ephah of fine flour mixed with oil as a grain offering, and a log of oil,
22 pamoja na njiwa wawili au kinda mbili za njiwa, ambao anaweza kupata; ndege mmoja atakuwa sadaka ya dhambi na mwingine sadaka ya kuteketezwa.
together with two doves or two young pigeons, such as he is able to get; one bird will be a sin offering and the other a burnt offering.
23 Katika siku ya nane lazima awalete kwa kuhani kwaajili ya utakaso, pakuigilia katika hema ya mkutano, mbele ya Yahwe.
On the eighth day he must bring them for his cleansing to the priest, to the entrance to the tent of meeting, before Yahweh.
24 Kuhani atachukua mwana kondoo kwaajili ya sadaka, na atachukua pamoja na kiasi cha mafuta ya mzeituni, na ataviinua juu kama anaviwasilisha kwa Yahwe.
The priest will take the lamb for an offering, and he will take with it the log of olive oil, and he will lift them high as he presents them to Yahweh.
25 Atamuua mwana kondoo kwaajili ya sadaka ya hatia, na atachukua baadhi ya ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka juu ya ncha ya sikio la kulia la yule wakutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye dole kubwa la mguu, wa kulia.
He will kill the lamb for the guilt offering, and he will take some of the blood of the guilt offering and put it on the tip of the right ear of the one who is to be cleansed, on the thumb of his right hand, and on the big toe of his right foot.
26 Ndipo kuhani atamimina baadhi ya mafuta katika kiganja cha mkono wake wa kushoto,
Then the priest will pour some of the oil into the palm of his own left hand,
27 na atanyunyiza kwa kidole chake cha kulia baadhi ya mafuta ambayo yako kwenye mkono wa kushoto mara saba mbele za Yahwe.
and he will sprinkle with his right finger some of the oil that is in his left hand seven times before Yahweh.
28 Ndipo kuhani ataweka kiasi cha mafuta ambayo yako kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la yule mtu wa kutakaswa, katika dole gumba lake la mkono wa kulia, na dole kubwa la mguu wa kulia, maeneo yale yale ambayo kaweka damu ya sadaka ya hatia.
The priest will then put some of the oil that is in his hand on the tip of the right ear of the one who is to be cleansed, on the thumb of his right hand, and on the big toe of his right foot, the same places where he put the blood of the guilt offering.
29 Ataweka mafuta yaliyobaki yaliyo mkononi mwake juu ya yule wakutakaswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe.
He will put the rest of the oil that is in his hand on the head of the one who is to be cleansed, to make atonement for him before Yahweh.
30 Lazima atoe sadaka ya njiwa au makinda ya njiwa, yale ambayo mtu ameweza kupata -
He must offer one of the doves or young pigeons, such as the person has been able to get—
31 moja kama ya sadaka ya dhambi na nyingine kama sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Ndipo kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya yule ambaye atatakaswa mbele za Yahwe.
one as a sin offering and the other as a burnt offering, along with the grain offering. Then the priest will make atonement for the one who is to be cleansed before Yahweh.
32 Hii ni sheria kwaajili ya mtu kwake kuna athari za ugonjwa wa ngozi, ambaye hawezi kumudu kiwango cha sadaka kwaajili ya utakaso wake.”
This is the law for a person in whom there is an infectious skin disease, who is not able to afford the standard offerings for his cleansing.”
33 Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
Yahweh spoke to Moses and to Aaron, saying,
34 “Wakati mtakuja katika nchi ya Kanaani ambayo nimewapa kama miliki, na kama naweka ukungu unaenea ndani ya nyumba katika nchi ya miliki yenu,
“When you have come into the land of Canaan which I gave to you as a possession, and if I put mildew that spreads in a house in the land of your possession,
35 ndipo yeye ambaye anamiliki nyumba ile lazima aje na kumwambia kuhani. Lazima aseme 'Inaonekana kwangu kuna kitu fulani kama ukungu ndani ya nyumba yangu.'”
then he who owns the house must come and tell the priest. He must say, 'There seems to me to be something like mildew in my house.'
36 Ndipo kuhani ataamuru kwamba watoe vitu vyote ndani kabla hajaenda ndani kuona uthibitisho wa ukungu, kiasi kwamba hakuna ndani ya nyumba kitakachofanywa najisi. Badaye kuhani lazima aende ndani kuona humo ndani.
Then the priest will command that they empty the house before he goes in to see the evidence of mildew, so that nothing in the house will be made unclean. Afterward the priest must go in to see the house.
37 Yeye lazima achunguze ukungu kuona kama umo katika kuta za nyumba, na kuona ikiwa kunaonekana ukijani au wekundu katika bonde za mwonekano wa kuta.
He must examine the mildew to see if it is in the house walls, and to see whether it appears greenish or reddish in the depressions in the wall's surface.
38 Kama nyumba inao ukungu, ndipo kuhani atatoka nje ya nyuma na kufunga mlango wa nyumba kwa siku saba.
If the house does have mildew, then the priest will go out of the house and shut the door to the house for seven days.
39 Ndipo kuhani atarudi tena katika siku ya saba na kuichunguza kuona kama ukungu umeenea katika kuta za nyumba.
Then the priest will return again on the seventh day and examine it to see if the mildew has spread in the walls of the house.
40 Kama hivyo, ndipo kuhani ataamuru kwamba wayaondoe mawe ambayo ukungu umepatikana na yatupwe katika sehemu najisi nje ya mji.
If it has, then the priest will command that they take out the stones in which the mildew has been found and throw them into an unclean place outside the city.
41 Yeye atataka kuta zote za ndani ya nyumba zikwanguliwe, na lazima achukue vitu vilivyochafuliwa na hivyo vilivyokwanguliwa nje ya mji na kuvitupa kwenye eneo lisilosafi.
He will require all the inside walls of the house to be scraped, and they must take the contaminated material that is scraped off outside the city and dump it into the unclean place.
42 Lazima wayachukue mawe mengine na kuyaweka katika sehemu ya mawe yaliyoondolewa, na lazima watumie udongo mpya kupigia lipu nyumba.
They must take other stones and put them in the place of the stones that were removed, and they must use new clay to plaster the house.
43 Kama ukungu unakuja tena na unaingia katika nyumba ambayo mawe yameondolewa na kuta zimekwanguliwa na kupigwa lipu upya,
If mildew comes again and breaks out in the house in which the stones have been taken away and the walls have been scraped and then replastered,
44 ndipo kuhani lazima aje aingie ndani na kuchunguza nyumba kuona kama ukungu umeenea ndani ya nyumba. Kama hivyo, huo ni ukungu mbaya, na nyumba ni najisi.
then the priest must come in and examine the house to see if mildew has spread in the house. If it has, then it is harmful mildew, and the house is unclean.
45 Nyumba hiyo lazima iangushwe chini. Hayo mawe, mbao, na lipu yote ndani ya nyumba lazima vibebwe kupelekwa nje ya mji kwenye sehemu najisi.
The house must be torn down. The stones, timber, and all the plaster in the house must be carried away out of the city to the unclean place.
46 Kwa nyongeza, yeyote anaenda ndani ya nyumba wakati imefungwa atakuwa najisi mpaka jioni.
In addition, whoever goes into the house during the time it is closed up will be unclean until evening.
47 Na yeyote aliyelala ndani ya nyumba lazima afue nguo zake, na yeyote aliyekula ndani ya nyumba lazima afue nguo zake.
Anyone who slept in the house must wash his clothes, and anyone who ate in the house must wash his clothes.
48 Kama kuhani akaingia hiyo kuichunguza kuona ikiwa ukungu umeenea katika nyumba baada ya nyumba kupigwa lipu, ndipo, kama ukungu umetoweka, ataitangaza nyumba hiyo kuwa ni safi.
If the priest enters the house to examine it to see whether the mildew has spread in the house after the house was plastered, then, if the mildew is gone, he will pronounce the house clean.
49 Ndipo kuhani lazima achukue ndege wawili kuitakasa nyumba, na mti wa mwelezi, na sufu nyekundu, na hisopo.
Then the priest must take two birds to cleanse the house, and cedar wood, and scarlet yarn, and hyssop.
50 Atamuua ndege mmojawapo katika maji masafi kwenye dumu la udongo.
He will kill one of the birds over fresh water in a clay jar.
51 Atachukua mti wa mwerezi, hisopo, sufu nyekundu na ndege aliyehai, na kuvichovya kwenye damu ya ndege aliyekufa, kwenye maji safi, na kunyunyizia nyumba mara saba.
He will take the cedar wood, the hyssop, the scarlet yarn, and the live bird, and dip them in the blood of the killed bird, into the fresh water, and sprinkle the house seven times.
52 Ataitakasa nyumba kwa damu ya ndege na maji safi, pamoja na ndege aliyehai, mti wa mwerezi, hisopo, na sufu nyekundu. Lakini atamwachia ndege aliyehai aende nje ya mji mashambani.
He will cleanse the house with the blood of the bird and with the fresh water, with the live bird, the cedar wood, the hyssop, and the scarlet yarn.
53 Kwa njia hii lazima afanye upatanisho kwaajili ya nyumba, na itakuwa safi.
But he will let the live bird go out of the city into the open fields. In this way he must make atonement for the house, and it will be clean.
54 Hii ni sheria kwa aina zote za athari ya ugonjwa wa ngozi na vitu vyote vinavyosababisha ugonjwa kama huo, na kwaajili ya kuwashwa,
This is the law for all types of infectious skin disease and things that cause such disease, and for an itch,
55 na kwa ukungu kwenye mavazi na nyumba,
and for mildew in clothing and in a house,
56 kwaajili ya uvimbe, kwaajili ya vipele, madoa,
for swelling, for a rash, and for a bright spot,
57 kutambua wakati wowote tatizo hili ni najisi au lini limetakaswa. Hii ni sheria kwaajili ya athari za ugonjwa wa ukungu.
to determine when any of these cases is unclean or when it is clean. This is the law for infectious skin diseases and mildew.”

< Mambo ya Walawi 14 >