< Mambo ya Walawi 11 >

1 Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
And the LORD spoke unto Moses and to Aaron, saying unto them:
2 “Sungumzeni na watu wa Israeli muwaambie, 'Hivi ndivyo viumbe vyenye uhai ambavyo mwaweza kula miongoni mwa wanyama walioko juu ya nchi.
Speak unto the children of Israel, saying: These are the living things which ye may eat among all the beasts that are on the earth.
3 Mnaweza kula mnyama yeyote aliye na kwato zenye kugawanyika na ambaye pia hucheua.
Whatsoever parteth the hoof, and is wholly cloven-footed, and cheweth the cud, among the beasts, that may ye eat.
4 Hata hivyo, kuna baadhi ya wanyama ambao ama hawacheui au hana kwato zilizogawanyika, nanyi msiwale hao, wanyama kama ngamia, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika. Kwa hiyo ngamia ni najisi kwenu.
Nevertheless these shall ye not eat of them that only chew the cud, or of them that only part the hoof: the camel, because he cheweth the cud but parteth not the hoof, he is unclean unto you.
5 Pimbi pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyo pia ni najisi kwenu.
And the rock-badger, because he cheweth the cud but parteth not the hoof, he is unclean unto you.
6 Na sungura pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyu naye ni najisi kwenu.
And the hare, because she cheweth the cud but parteth not the hoof, she is unclean unto you.
7 Na nguruwe pia: ingawaje yeye anazo kwato zilizogawanyika lakini hacheui, kwa hiyo yeye ni najisi kwenu.
And the swine, because he parteth the hoof, and is cloven-footed, but cheweth not the cud, he is unclean unto you.
8 Msile aina yoyote ya nyama yao, wala msiiguse mizoga yao. Hao ni najisi kwenu.
Of their flesh ye shall not eat, and their carcasses ye shall not touch; they are unclean unto you.
9 Nao wanyama waishio majini mnaoweza kuwala ni wale wote walio na mapezi na magamba, iwe waliomo baharini au mitoni.
These may ye eat of all that are in the waters: whatsoever hath fins and scales in the waters, in the seas, and in the rivers, them may ye eat.
10 Lakini viumbe wote hai wasio na mapezi na magamba waliomo baharini au mitoni, pamoja na wale waendao majini na viumbe hai waliomo majini —watakuwa chukizo kwenu.
And all that have not fins and scales in the seas, and in the rivers, of all that swarm in the waters, and of all the living creatures that are in the waters, they are a detestable thing unto you,
11 Kwa kuwa watakuwa chukizo, msile nyama yao, pia mizoga yao sharti itakuwa chukizo.
and they shall be a detestable thing unto you; ye shall not eat of their flesh, and their carcasses ye shall have in detestation.
12 Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majini ni lazima kiwe chukizo kwenu.
Whatsoever hath no fins nor scales in the waters, that is a detestable thing unto you.
13 Nao ndege mtakaowachukia na msiopaswa kuwala ni hawa wafuatao: tai, furukombe, kipungu,
And these ye shall have in detestation among the fowls; they shall not be eaten, they are a detestable thing: the great vulture, and the bearded vulture, and the ospray;
14 mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga,
and the kite, and the falcon after its kinds;
15 kila aina ya kunguru,
every raven after its kinds;
16 kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe, na aina yoyote ya mwewe.
and the ostrich, and the night-hawk, and the sea-mew, and the hawk after its kinds;
17 Ni lazima pia bundi mdogo na bundi mkubwa muwaone kuwa chukizo, mnandi,
and the little owl, and the cormorant, and the great owl;
18 bundi mweupe na mwari,
and the horned owl, and the pelican, and the carrion-vulture;
19 korongo na ina zote za koikoi, huduhudi na popo pia.
and the stork, and the heron after its kinds, and the hoopoe, and the bat.
20 Wadudu wote wenye mabawa wanatembea kwa miguu minne kwenu ni machukizo.
All winged swarming things that go upon all fours are a detestable thing unto you.
21 Lakini manaweza kula wadudu wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ya kurukia ardhini yenye vifundo.
Yet these may ye eat of all winged swarming things that go upon all fours, which have jointed legs above their feet, wherewith to leap upon the earth;
22 Na manaweza kula kula aina zote za nzige, senene, parare, au panzi.
even these of them ye may eat: the locust after its kinds, and the bald locust after its kinds, and the cricket after its kinds, and the grasshopper after its kinds.
23 Lakini wadudu wote warukao wenye miguu minne ni chulkizo kwenu.
But all winged swarming things, which have four feet, are a detestable thing unto you.
24 Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao.
And by these ye shall become unclean; whosoever toucheth the carcass of them shall be unclean until even.
25 Na yeyote atakayeokota mojawapo wa mizoga yao ni lazima atazifua ngua zake naye atakuwa najisi hata jioni.
And whosoever beareth aught of the carcass of them shall wash his clothes, and be unclean until the even.
26 Mnyama yeyote ambaye anazo kwato ziliachana ambazo hazikugawanyika kabisa au hacheui huyo ni najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa najisi.
Every beast which parteth the hoof, but is not cloven footed, nor cheweth the cud, is unclean unto you; every one that toucheth them shall be unclean.
27 Mnyama yeyote anayetembea kwa vitanga vyake miongoni mwa wanyama waendao kwa miguu yote minne ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mzoga kama huo atakuwa najisi hata jioni.
And whatsoever goeth upon its paws, among all beasts that go on all fours, they are unclean unto you; whoso toucheth their carcass shall be unclean until the even.
28 Na yeyote aokotaye mzoga kama huo ni zazima atazifua nguo zake na kuwa najisi hata jioni. Wanyama hawa watakuwa najisi kwenu.
And he that beareth the carcass of them shall wash his clothes, and be unclean until the even; they are unclean unto you.
29 Kuhusiana na wanyama wataambaao juu ya ardhi, hawa ndiyo walio najisi kwenu: kicheche, panya, aina zote za mijusi mikubwa, guruguru,
And these are they which are unclean unto you among the swarming things that swarm upon the earth: the weasel, and the mouse, and the great lizard after its kinds,
30 kenge, mijusi ya ukutani, goromoe, na kinyonga.
and the gecko, and the land-crocodile, and the lizard, and the sand-lizard, and the chameleon.
31 Wanyama hawa wote ambao hutambaa, hawa ndiyo watakuwa najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa njisi hata jioni.
These are they which are unclean to you among all that swarm; whosoever doth touch them, when they are dead, shall be unclean until the even.
32 Na iwapo mmoja wao anakufa na kuanguka juu ya chombo, chombo hicho kitakuwa najisi, ama kiwe kimetengenezwa kwa mbao, nguo, ngozi, au gunia. Kiwe chombo cha namna gani na kiwe kwa matumizi gani, ni lazima kitalowekwa katika maji nacho kitakuwa najisi hata jio. Kisha kitakuwa safi.
And upon whatsoever any of them, when they are dead, doth fall, it shall be unclean; whether it be any vessel of wood, or raiment, or skin, or sack, whatsoever vessel it be, wherewith any work is done, it must be put into water, and it shall be unclean until the even; then shall it be clean.
33 Kwa hiyo kila chungu ambacho mnyama najisi atakiangukia juu yake au ndani yake, chochote kilichomo kwenye chungu hicho kitakuwa najisi, na ni lazima mtakivunja chungu hicho.
And every earthen vessel whereinto any of them falleth, whatsoever is in it shall be unclean, and it ye shall break.
34 Vyakula vyote ambavyo ni safi na kilichuhusiwa kuliwa, lakini kikaingiwa na maji kutoka kwenye chungu najisi kilichoanguka, nacho kitakuwa najisi.
All food therein which may be eaten, that on which water cometh, shall be unclean; and all drink in every such vessel that may be drunk shall be unclean.
35 Na kitu chochote kinachoweza kunywewa kutoka kwenye chungu kama hicho kitakuwa najisi. Kila kitu kitakachoangukiwa juu yake na kipande cha mzoga wa mnyama najisi nacho kitakuwa najisi, ama liwe ni jiko au vyungu vya kupikia. Ni najisi na ni lazima kiwe najisi kwenu.
And every thing whereupon any part of their carcass falleth shall be unclean; whether oven, or range for pots, it shall be broken in pieces; they are unclean, and shall be unclean unto you.
36 Chemchemi au kisima cha maji ya kunywa yanapokusanyika patabaki kuwa safi iwapo kiumbe najisi kama hicho kitaangukia humo. Lakini ikiwa yeyote anaugusa mzoga wa mnyama aliye najisi uliomo ndani ya maji, yeye atakuwa najisi.
Nevertheless a fountain or a cistern wherein is a gathering of water shall be clean; but he who toucheth their carcass shall be unclean.
37 Iwapo sehehemu yoyote ya mzoga wa mnyama aliyenajisi inaangukia juu ya mbegu zozote zilizo kwa ajili ya kupanda. Mbegu hizo zitakuwa bado zingali safi.
And if aught of their carcass fall upon any sowing seed which is to be sown, it is clean.
38 Lakini kama maji yanawekwa juu ya mbegu, na kama sehemu ya mzoga unaangukia juu yake, nazo zitakuwa najisi kwenu.
But if water be put upon the seed, and aught of their carcass fall thereon, it is unclean unto you.
39 Iwapo mnyama yeyote awezaye kuliwa anakufa, naye yeyote amgusaye atakuwa najisi hata jioni.
And if any beast, of which ye may eat, die, he that toucheth the carcass thereof shall be unclean until the even.
40 Na yeyote alaye chochote cha mzoga huo atalazimika kufua nguo zake naye atakuwa anjisi hata jioni. Na yeyote aokotaye mzoga kama huo atafua nguo zake na kuwa najisi hata jioni.
And he that eateth of the carcass of it shall wash his clothes, and be unclean until the even; he also that beareth the carcass of it shall wash his clothes, and be unclean until the even.
41 Kila mnyama atambaaye juu ya ardhi atakuwa chukizo; hatakuwa wa kuliwa.
And every swarming thing that swarmeth upon the earth is a detestable thing; it shall not be eaten.
42 Chochote kitambaacho kwa kujivuta juu ya tumbo lake, na chochote kitembeacho kwa miguu yake yote minne, au chochote kilicho na miguu mingi—wanyama wote ambao hutambaa juu ya nchi, hawa msiwale, kwa sababu watakuwa machukizo.
Whatsoever goeth upon the belly, and whatsoever goeth upon all fours, or whatsoever hath many feet, even all swarming things that swarm upon the earth, them ye shall not eat; for they are a detestable thing.
43 Msijinajisi wenyewe kwa kiumbe chochote nnajisi kitaambacho; msijinasi wenyewe kwavyo, ili kwamba msije mkachafuliwa navyo.
Ye shall not make yourselves detestable with any swarming thing that swarmeth, neither shall ye make yourselves unclean with them, that ye should be defiled thereby.
44 Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu. Nanyi lazima muwe watakatifu, kwa hiyo na iweni watakatifu, kwa sababu Mimi ni mtakatifu. Haiwapasi kujichafua kwa aina yoyote ya kiendacho juu ya nchi.
For I am the LORD your God; sanctify yourselves therefore, and be ye holy; for I am holy; neither shall ye defile yourselves with any manner of swarming thing that moveth upon the earth.
45 Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh, aliyewaleta ninyi kutoka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo lazima muwe watakatifu, kwa kuwa Mimi ni mtakatifu.
For I am the LORD that brought you up out of the land of Egypt, to be your God; ye shall therefore be holy, for I am holy.
46 Hii ndiyo sheria kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho majini, na ya kila kiumbe kitambaacho juu ya nchi,
This is the law of the beast, and of the fowl, and of every living creature that moveth in the waters, and of every creature that swarmeth upon the earth;
47 kwa jili ya kilie kinachopaswa kutofautishwa kati ya kilicho najisi na kilicho safi, na kati ya vitu vilivyokufa na vilivyo hai ambavyo vyaweza kuliwa na vitu vyenye uihai visivyoweza kuliwa.”
to make a difference between the unclean and the clean, and between the living thing that may be eaten and the living thing that may not be eaten.

< Mambo ya Walawi 11 >