< Mambo ya Walawi 10 >

1 Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua kila mtu kifukizo chake, akaweka moto ndani yake, na kisha uvumba. Kisha wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa.
Then Aaron’s sons, Nadab and Abihu, took each man his censer and placed therein fire, and put thereon incense, —and brought near before Yahweh strange fire, which he had not commanded them.
2 Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh na kuwala, nao wakafa mbele za Yahweh.
Then came there forth fire from before Yahweh, and consumed them, —and they died before Yahweh.
3 Kisha Musa akamwambia Aroni, Hivi ndiyo Yahweh alivyokuwa akizunguzia aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wajao mbele zangu. Nami nitatukuzwa mbele za watu wote.'” Naye Aroni hakusema neno lolote.
Then said Moses unto Aaron—The very thing, that Yahweh spake, saying—In them that draw near to me, must I be hallowed, And before the faces of all the people, must I get myself honour, —And Aaron, was dumb.
4 Musa akamwita Mishaeli na Elzafani, wana wa Uzieli mjomba wa Aroni, naye akamwambia, “njoo huku na uwatowe ndugu zako nje ya kambi watoke mbele ya hema.”
Then called Moses unto Mishael, and unto Elzaphan, sons of Uzziel, uncle of Aaron, —and said unto them—Draw near bear away your brethren from before the sanctuary, unto the outside of the camp.
5 Hivyo wakakaribia na kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani, nao wakawapeleka nje ya kambi, kama Musa alivyokuwa ameelekeza. Kisha Musa akamwambia Aroni na wanawe wengine wawili, Eliezari na Ithamari, “
So they drew near and bare them away, in their tunics, unto the outside of the camp, —as spake Moses.
6 Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu, ili kwamba msije mkafa, na kwamba Yahweh asilikasirikie kusanyiko zima. Lakini waacheni jamaa zenu, nyumba yote ya Israeli waweze kufanya ibada za maombolezo kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto.
Then said Moses unto Aaron and to Eleazar and to Ithamar, his sons—Your heads, ye may not bare and your garments, ye shall not rend so shall ye not die, neither against all the assembly, will he be wroth, —but let, your brethren the whole house of Israel, bewail the consuming fire wherewith Yahweh hath consumed.
7 Msiende nje kutoka kwenye ingilio la hema la kukutania, ama sivyo mtakufa, kwa kuwa mafuta ya Yahweh ya upako yako juu yenu.” Kwa hiyo wakatenda sawasawa na maelekezo ya Musa.
But, from the entrance of the tent of meeting, shall ye not go forth, lest ye die, for, the anointing oil of Yahweh is upon you. And they did according to the word of Moses.
8 Mungu akazungumza na Aroni, akisema,
Then spake Yahweh unto Aaron, saying:
9 “Msinywe mvinyo wala kinywaji kikali, wewe, au wanao wanaobaki pamoja nawe, ili kwamba mtakapoingia kwenye hema ya kukutania msije mkafa. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu,
Wine and strong drink, thou mayest not drink, —thou nor thy sons with thee when ye enter into the tent of meeting, so shall ye not die, —an age-abiding statute to your generations;
10 ili kupaambanua kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida, na kati ya najisi na safi,
That ye may make a difference, between the sacred and the common, —and between the unclean and the clean;
11 ili kwamba mweze kuwafundisha watu wa Israeli amri zote ambazo Yahweh ameziamru kwa kinywa cha Musa.
And may teach the sons of Israel, —all the statutes which Yahweh hath spoken unto them, by the mediation of Moses.
12 Musa akazungumza na Aroni na wanawe wawili waliosalia; Eliazari naIthamari, Twaeni sadaka ya nafaka inayobaki kutokana na sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto, nanyi ileni kando ya madhabahu bila hamiara, kwa kuwa ni takatifu sana.
Then spake Moses unto Aaron and unto Eleazar and unto Ithamar his sons that were left, Take ye the meal-offering that is left of the altar-flames of Yahweh, and eat it unleavened beside the altar, —for, most holy, it is;
13 lazima mtaila mahali patatifu kwa sababu huo ni mgao wako wewe na mgao wa wanao wa matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, kwa kuwa hivi ndivyo limeamriwa niwaambie.
therefore shall ye eat it in a holy place, for, thine by statute, and thy sons’ by statute, it is, from among the altar-flames of Yahweh, —for, so, am I commanded.
14 Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh, yapasa mzile mahali palipo safi panapokubalika kwa Mungu. Wewe mwenyewe, wanao na binti zako waliopamoja nawe mtakula sehemu hizo, kwa kuwa zimetolewa kuwa mgao wako na mgao wa wanao kutokana na dhabihu ya sadaka ya ushirika wa watu wa Israeli.
And the wave-breast, and the heave-shoulder, shall ye eat in clean place, thou, and thy sons and thy daughters with thee, —for as thine by statute and thy sons’ by statute, have they been given, from among the peace-offerings of the sons of Israel.
15 Lile paja lililotolewa na kidari kilichotikiswa, ni lazima ziletwe pamoja na sadaka ya mafuta iliyofanywa kwa moto, ili kutikiswa mbele za Yahweh. Nazo zitakuwa zako wewe na wanao kuwa mgao wenu daima, kama Yahweh alivyoamru.
The heave-shoulder and the wave-breast upon the altar-flames of the fat portions, shall they bring in, to wave as a wave-offering, before Yahweh, —so shall they be thine, and thy sons’ with thee, by an age-abiding statute, As Yahweh hath commanded.
16 Kisha Musa akauliza kuhusu yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye akagundua kwamba alikuwa ametekezwa kwa moto. Kwa hiyo akawakasirikia Eliazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia; akawaambia,
Now, as for the sin-bearing goat, Moses diligently sought it but lo! it had been burnt up, —then was he wroth against Eleazar and against Ithamar, the sons of Aaron that were left, saying:
17 “Kwa nini hamjaila sadaka ya dhambi katika eneo la hema, kwa kuwa ni takatifu sana, na kwa kuwa Yahweh amishaitoa kwenu ili kuchukua uovu wa kusanyiko, ili kufanya upatanisho kwa aijli yao mbele zake?
Wherefore did ye not eat the sin-bearer in the holy place? for most, holy, it is, —and thee same, hath he given you that ye may bear the iniquity of the assembly, to put a propitiatory-covering over them before Yahweh.
18 Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema, kwa hiyo iliwapasa kwa hakika kuwa mekwisha ila kwenye eneo la hema, kama nilivyoagiza?
Lo! the blood thereof had not been taken into the holy place, within, —ye should have, indeed eaten, it, in a holy place, as I commanded.
19 Kisha Aroni akamjibu Musa, “Tazama, leo walitoa sadaka yao ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele za Yahweh, na jambo hili vilevile limetendeka kwangu leo. Ikiwa nimeshakula sadaka ya dhambi leo, Je! Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?”
Then spake Aaron unto Moses—Lo! this very day, when they had brought near their own sin-bearer, and their own ascending-sacrifice, there befell me such things as these, —if, then, I had eaten of the sin-bearer this day, would it have been well-pleasing in the eyes of Yahweh?
20 Naye Musa aliposikia hivyo, akaridhika.
And, when Moses heard that, then was it well-pleasing in his eyes.

< Mambo ya Walawi 10 >