< Mambo ya Walawi 10 >

1 Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua kila mtu kifukizo chake, akaweka moto ndani yake, na kisha uvumba. Kisha wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa.
Nadab and Abihu, the sons of Aaron [Light-bringer], each took his censer, and put fire in it, and laid incense on it, and offered strange fire before Adonai, which he had not enjoined them.
2 Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh na kuwala, nao wakafa mbele za Yahweh.
Fire came out from before Adonai, and devoured them, and they died before Adonai.
3 Kisha Musa akamwambia Aroni, Hivi ndiyo Yahweh alivyokuwa akizunguzia aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wajao mbele zangu. Nami nitatukuzwa mbele za watu wote.'” Naye Aroni hakusema neno lolote.
Then Moses [Drawn out] said to Aaron [Light-bringer], “This is what Adonai spoke of, saying, ‘I will show myself holy to those who come near me, and before all the people I will be glorified.’” Aaron [Light-bringer] held his peace.
4 Musa akamwita Mishaeli na Elzafani, wana wa Uzieli mjomba wa Aroni, naye akamwambia, “njoo huku na uwatowe ndugu zako nje ya kambi watoke mbele ya hema.”
Moses [Drawn out] called Mishael and Elzaphan, the sons of Uzziel the dod ·uncle· of Aaron [Light-bringer], and said to them, “Draw near, carry your brothers from before the sanctuary out of the camp.”
5 Hivyo wakakaribia na kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani, nao wakawapeleka nje ya kambi, kama Musa alivyokuwa ameelekeza. Kisha Musa akamwambia Aroni na wanawe wengine wawili, Eliezari na Ithamari, “
So they came near, and carried them in their coats out of the camp, as Moses [Drawn out] had said.
6 Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu, ili kwamba msije mkafa, na kwamba Yahweh asilikasirikie kusanyiko zima. Lakini waacheni jamaa zenu, nyumba yote ya Israeli waweze kufanya ibada za maombolezo kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto.
Moses [Drawn out] said to Aaron [Light-bringer], and to Eleazar [Help of God] and to Ithamar, his sons, “Don’t let the hair of your heads go loose, and don’t tear your clothes; so that you don’t die, and so that he not be angry with all the congregation; but let your brothers, the whole house of Israel [God prevails], bewail the burning which Adonai has kindled.
7 Msiende nje kutoka kwenye ingilio la hema la kukutania, ama sivyo mtakufa, kwa kuwa mafuta ya Yahweh ya upako yako juu yenu.” Kwa hiyo wakatenda sawasawa na maelekezo ya Musa.
You shall not go out from the door of the Tent of Meeting, lest you die; for the anointing oil of Adonai is on you.” They did according to the word of Moses [Drawn out].
8 Mungu akazungumza na Aroni, akisema,
Then Adonai said to Aaron [Light-bringer],
9 “Msinywe mvinyo wala kinywaji kikali, wewe, au wanao wanaobaki pamoja nawe, ili kwamba mtakapoingia kwenye hema ya kukutania msije mkafa. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu,
“You and your sons are not to drink wine or strong drink whenever you go into the Tent of Meeting, or you will die. This shall be a regulation forever throughout all your generations.
10 ili kupaambanua kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida, na kati ya najisi na safi,
You are to make a distinction between the holy and the common, and between the unclean and the clean.
11 ili kwamba mweze kuwafundisha watu wa Israeli amri zote ambazo Yahweh ameziamru kwa kinywa cha Musa.
You are to teach the children of Israel [God prevails] all the statutes which Adonai has spoken to them by Moses [Drawn out].”
12 Musa akazungumza na Aroni na wanawe wawili waliosalia; Eliazari naIthamari, Twaeni sadaka ya nafaka inayobaki kutokana na sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto, nanyi ileni kando ya madhabahu bila hamiara, kwa kuwa ni takatifu sana.
Moses [Drawn out] spoke to Aaron [Light-bringer], and to Eleazar [Help of God] and to Ithamar, his sons who were left, “Take the meal offering that remains of the offerings of Adonai made by fire, and eat it without yeast beside the altar; for it is most holy;
13 lazima mtaila mahali patatifu kwa sababu huo ni mgao wako wewe na mgao wa wanao wa matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, kwa kuwa hivi ndivyo limeamriwa niwaambie.
and you shall eat it in a holy place, because it is your chok ·portion·, and your sons’ chok ·portion·, of the offerings of Adonai made by fire: for so I am enjoined.
14 Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh, yapasa mzile mahali palipo safi panapokubalika kwa Mungu. Wewe mwenyewe, wanao na binti zako waliopamoja nawe mtakula sehemu hizo, kwa kuwa zimetolewa kuwa mgao wako na mgao wa wanao kutokana na dhabihu ya sadaka ya ushirika wa watu wa Israeli.
The breast that is waved and the thigh that is raised you shall eat in a clean place, you, and your sons, and your daughters with you: for they are given as your chok ·portion·, and your sons’ chok ·portion·, out of the sacrifices of the peace offerings of the children of Israel [God prevails].
15 Lile paja lililotolewa na kidari kilichotikiswa, ni lazima ziletwe pamoja na sadaka ya mafuta iliyofanywa kwa moto, ili kutikiswa mbele za Yahweh. Nazo zitakuwa zako wewe na wanao kuwa mgao wenu daima, kama Yahweh alivyoamru.
The thigh that is raised and the breast that is waved they shall bring with the offerings made by fire of the fat, to wave it for a wave offering before Adonai: and it shall be yours, and your sons’ with you, as a chok ·portion· forever; as Adonai has enjoined.”
16 Kisha Musa akauliza kuhusu yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye akagundua kwamba alikuwa ametekezwa kwa moto. Kwa hiyo akawakasirikia Eliazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia; akawaambia,
Moses [Drawn out] diligently inquired about the goat of the sin offering, and, behold, it was burned: and he was angry with Eleazar [Help of God] and with Ithamar, the sons of Aaron [Light-bringer] who were left, saying,
17 “Kwa nini hamjaila sadaka ya dhambi katika eneo la hema, kwa kuwa ni takatifu sana, na kwa kuwa Yahweh amishaitoa kwenu ili kuchukua uovu wa kusanyiko, ili kufanya upatanisho kwa aijli yao mbele zake?
“Why haven’t you eaten the sin offering in the place of the sanctuary, since it is most holy, and he has given it you to bear the iniquity of the congregation, to make atonement for them before Adonai?
18 Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema, kwa hiyo iliwapasa kwa hakika kuwa mekwisha ila kwenye eneo la hema, kama nilivyoagiza?
Behold, its blood was not brought into the inner part of the sanctuary: you certainly should have eaten it in the sanctuary, as I enjoined.”
19 Kisha Aroni akamjibu Musa, “Tazama, leo walitoa sadaka yao ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele za Yahweh, na jambo hili vilevile limetendeka kwangu leo. Ikiwa nimeshakula sadaka ya dhambi leo, Je! Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?”
Aaron [Light-bringer] spoke to Moses [Drawn out], “Behold, today they have offered their sin offering and their burnt offering before Adonai; and such things as these have happened to me. If I had eaten the sin offering today, would it have been pleasing in Adonai’s sight?”
20 Naye Musa aliposikia hivyo, akaridhika.
When Moses [Drawn out] sh'ma ·heard obeyed· that, it was pleasing in his sight.

< Mambo ya Walawi 10 >