< Maombolezo 5 >

1 Kumbuka, Yahweh, yaliyo tutokea na uone aibu yetu.
Remember, Jehovah, what has come on us. Look, and see our disgrace.
2 Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni; nyumba zetu kwa wageni.
Our inheritance is turned over to strangers, our houses to foreigners.
3 Tumekuwa yatima, bila baba, na mama zetu ni kama wajane.
We are orphans and fatherless. Our mothers are like widows.
4 Lazima tulipe fedha kwa maji tunayo kunywa, na tulipe fedha kupata mbao zetu.
We have to pay for a drink of water; our wood is sold to us.
5 Hao wanakuja kwetu wamekaribia nyuma yetu; tumechoka na hatuwezi pata mapumziko.
Our pursuers are on our necks; we are weary, and have no rest.
6 Tumejitoa kwa Misri na kwa Assiria tupate chakula cha kutosha.
We have submitted to the Egyptians and to the Assyrians, to get enough bread.
7 Baba zetu walifanya dhambi, na hawapo tena, na tumebeba dhambi zao.
Our fathers sinned, and are no more; but we have borne their iniquities.
8 Watumwa walitutawala, na hakuna wa kutuokoa na mikono yao.
Servants rule over us: There is none to deliver us out of their hand.
9 Tunapata mkate wetu pale tunapo hatarisha maisha, kwasababu ya upanga wa nyikani.
We get our bread at the peril of our lives, because of the sword in the wilderness.
10 Ngozi zetu zimekuwa na moto kama jiko kwasababu ya joto la njaa.
Our skin is hot like an oven, because of the burning heat of famine.
11 Wanawake wanabakwa Sayuni, na mabikra katika mji wa Yuda.
They raped the women in Zion, the virgins in the cities of Judah.
12 Watoto wa mfalme wamenyongwa na mikono yao, na hakuna heshima inayoonyeshwa kwa wazee.
Princes were hung by their hands; elders were shown no respect.
13 Wanaume vijana wanalizimishwa kusaga mbegu kwa jiwe la kusagia, na wavulana wanajikwa chini ya vifurushi vya kuni.
The young men grind at the mill; the boys stagger under loads of wood.
14 Wazee wameacha lango la mji, na vijana wameacha miziki.
The elders have gone from the gate, the young men from their music.
15 Furaha ya moyo imekoma na kucheza kwetu kumegeuka kilio.
The joy of our heart has ceased; our dancing is turned into mourning.
16 Taji limeanguka kichwani mwetu; ole wetu, kwa kuwa tumetenda dhambi!
The crown is fallen from our head; woe to us, for we have sinned.
17 Kwa kuwa moyo wetu umekuwa unaumwa, na machozi yetu ya fifia, kwa vitu hivi macho yetu yanafifia
For this our heart is faint; for these things our eyes grow dim.
18 maana Mlima Sayuni umelala ukiwa, mbwa wa mitaani wacheza juu yake.
For the mountain of Zion, which is desolate; the foxes walk on it.
19 Lakini wewe, Yahweh, unatawala milele, na utaketi katika kiti chako cha enzi vizazi na vizazi. Kwanini unatusahau milele?
But you, Jehovah, abide forever; your throne is from generation to generation.
20 Kwanini unatutelekeza kwa siku nyingi?
Why do you keep on forgetting us? Why do you forsake us so long?
21 Turejeshe kwako, Yahweh, na sisi tutarejea. Fanya upya siku zetu kama zilivyo kuwa hapo zamani -
Restore us to you, Jehovah, and we shall be restored; renew our days as in former times,
22 vinginevyo labda uwe umetukataa na una hasira kwetu kupita kiasi.
unless you have completely rejected us and are angry with us beyond measure.

< Maombolezo 5 >