< Waamuzi 8 >

1 Watu wa Efraimu wakamwambia Gideoni, “Ni nini hiki umetutenda? Haukuita wakati ulipokwenda kupigana na Midiani.” Wakamwambia kwa nguvu.
Les hommes d'Ephraïm dirent à Gédéon: Pourquoi nous as-tu fait l'injure de ne point nous appeler quand tu marchais pour combattre les Madianites? Et ils lui parlèrent durement.
2 Akawaambia, “Nimefanya nini sasa kulinganisha na mlichofanya ninyi? Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?
Et il leur dit: Qu'ai-je fait maintenant qui égale ce que vous avez fait? Une petite grappe d'Ephraïm ne vaut-t-elle pas mieux que la vendange d'Abiézer?
3 Mungu amewapa ushindi juu ya wakuu wa Midiani-Orebu na Zeeb! Mimi nimefanya nini ukilinganisha na ninyi?” Hasira yao ikashuka chini aliposema hili.
Le Seigneur a livré à vos mains les chefs de Madian, Oreb et Zeb. Aurais-je pu faire autant que vous? Alors, leur courroux se détourna de lui, quand il leur eut dit cette parole.
4 Gideoni alikuja Yordani na akavuka juu yake, yeye na watu mia tatu waliokuwa pamoja naye. Walikuwa wamechoka, lakini bado waliendelea kufuatilia.
Ensuite, Gédéon marcha au Jourdain, il le traversa, et les trois cents hommes avec lui; ils étaient affamés, mais ils poursuivaient toujours.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali wape mikate kwa watu wanaonifuata, kwa kuwa wamechoka, nami niwafuatilia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.
Et Gédéon dit aux hommes de Socchoth: Donnez-moi des pains pour nourrir le peuple qui me suit, car ils tombent de défaillance; et voilà que je poursuis Zébé et Salmana, rois de Madian.
6 Na wakuu wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna sasa ipo mikononi mwako? Kwa nini tulipe jeshi lako mikate?”
Mais les chefs de Socchoth dirent: Est-ce que la main de Zébé et de Salmana est déjà dans ta main, pour que nous donnions des vivres à ta troupe?
7 Gideoni akasema, “Bwana akitupa ushindi juu ya Zeba na Salmunna, nitainyunyiza ngozi yenu kwa miiba ya jangwani na michongoma.
Et Gédéon dit: A cause de votre refus, lorsque le Seigneur aura livré à nos mains Zébé et Salmana, je broierai vos chairs à force de coups d'épines du désert et de Barcenim.
8 Akatoka huko, akaenda Penieli, akawaambia watu maneno hayo hayo; lakini watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyojibu.
De là, il monta en Phanuel, où il leur fit la même demande; les hommes de Phanuel lui répondirent de la même manière que ceux de Socchoth.
9 Akawaambia pia watu wa Penieli, akasema, “Nitakapokuja kwa amani, nitauangusha mnara huu.”
Et Gédéon dit aux hommes de Phanuel: A mon retour, après la paix, je démolirai cette tour.
10 Sasa Zeba na Salmuna walikuwa huko Karkori pamoja na jeshi lao, karibu na watu elfu kumi na tano, wote waliosalia nje ya jeshi lote la watu wa Mashariki, kwa kuwa walianguka watu 120, 000 waliofundishwa kupigana na upanga.
Or, Zébé et Salmana étaient alors en Carcar; leur camp renfermait environ quinze mille hommes, débris de tout le camp des étrangers; et ceux qui avaient péri n'étaient pas moins de cent vingt mille portant l'épée.
11 Gideoni akapanda barabara iliyochukuliwa na wakaazi wa hema, Noba na Yogbena. Akalishinda jeshi la adui, kwa sababu hawakuwa wanatarajia shambulio.
Et Gédéon prit le chemin des ennemis dont les tentes étaient à l'orient de Nabé et de Jégébal, et il attaqua le camp, et le camp était sans méfiance.
12 Zeba na Salmuna walikimbia, na Gideoni alipowafuata, akawatwaa wafalme wawili wa Midiani-Zeba na Salmunna- na kulifanya jeshi lote kuwa na hofu.
Et Zébé et Salmana s'étant enfuis, il les poursuivit, il les prit, et frappa d'épouvante l'armée entière.
13 Gideoni, mwana wa Yoashi, alirudi kutoka kwenye vita kwenda kupitia Heresi.
Ensuite, Gédéon, fils de Joas, revint de la bataille des hauteurs d'Arès, où il l'avait livrée.
14 Akamkimbilia kijana mmoja wa watu wa Sukothi na kutafuta ushauri kutoka kwake. Kijana huyo alimwelezea viongozi wa Sukothi na wazee wake, watu sabini na saba.
Et il surprit un jeune garçon des hommes de Socchoth; il le questionna, et il écrivit, d'après lui, les noms des chefs et des anciens de Socchoth: soixante-dix-sept hommes.
15 Gideoni akaja kwa watu wa Sukothi, akasema, “Tazameni Zeba na Salmuna, ambao mlinidhihaki kwa ajili yao, nikasema, 'Je! mmemshinda Zeba na Salmuna? Hatujui kwamba tunapaswa kulipa jeshi lako mkate.”
Et Gédéon se rendit auprès des chefs de Socchoth, et il dit: Voici Zébé et Salmana, au sujet desquels vous m'avez outragé, disant: Est-ce que la main de Zébé et de Salmana est dans ta main, pour que nous donnions des vivres à tes hommes défaillants?
16 Gideoni akawachukua wazee wa mji, naye akawaadhibu watu wa Sukothi pamoja na miiba ya jangwa na michongoma.
Puis, il prit les anciens de la ville; il prit des épines du désert et de Barcenim, et il fit meurtrir de coups avec les épines les hommes de la ville.
17 Akaangusha mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji huo.
Et il démolit la tour de Phanuel, et il tua les hommes de la ville.
18 Gideoni akamwambia Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliwauawa Tabori?” Wakajibu, “Kama wewe ulivyo, ndivyo walivyokuwa. Kila mmoja wao alionekana kama mwana wa mfalme.”
Et il dit à Zébé et Salmana: Comment étaient les hommes que vous avez tués au mont Thabor? Et ils dirent: Tel nous te voyons, tels ils étaient; ils semblaient des fils des rois.
19 Gideoni akasema, 'Wao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama Bwana anaishivyo, kama mngewaacha hai, nisingewauwa.”
Et Gédéon dit.: C'étaient mes frères, fils de ma mère, vive le Seigneur! Si vous les aviez épargnés, je ne vous ferais point mourir.
20 Akamwambia Yetheri (mzaliwa wake wa kwanza), “Simama uwaue!” Lakini kijana huyo hakutoa upanga wake kwa kuwa aliogopa, kwa sababu alikuwa bado kijana mdogo.
Puis, il dit à Jéther, son premier-né: Lève-toi, et tue-les. Mais le jeune homme ne tira point son épée, car il avait crainte, parce qu'il était jeune encore.
21 Ndipo Zeba na Salmuna wakasema, simama mwenyewe, utuue! Kwa maana kama mtu alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake. Gideoni akasimama na kumwua Zeba na Salmuna. Pia aliondoa mapambo yaliyokuwa juu ya shingo za ngamia zao.
Zébé et Salmana dirent: Lève-toi toi-même, et tombe sur nous, car ta force est celle d'un homme. Gédéon se leva donc, et il tua Zébé et Salmana. Et il prit les croissants qui ornaient le cou de leurs chameaux.
22 Ndipo wana wa Israeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, mtoto wako, na mjukuu wako; kwa sababu umetuokoa mikononi mwa Midiani.”
Israël dit alors à Gédéon: Seigneur, règne sur nous, toi et ton fils et le fils de ton fils, parce que tu nous as sauvés des mains de Madian.
23 Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala mtoto wangu hatatawala juu yenu. Bwana atatawala juu yenu.”
Mais Gédéon leur dit: Je ne règnerai point sur vous, et mon fils ne règnera point sur vous; le Seigneur règnera sur vous.
24 Gideoni akawaambia, “Nina haja yangu niitakayo kwenu kwamba kila mmoja wenu atanipe pete kutoka kwenye nyara zake.” (Wamidiani walikuwa na pete za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)
Et Gédéon ajouta: Je vous ferai une demande: Que chacun me donne, de sa part du butin, les pendants d'oreilles. Ces hommes avaient tous des pendants d'oreilles d'or, parce qu'ils étaient Ismaélites.
25 Wakamjibu, “Tunafurahi kukupa.” Wakatandika vazi na kila mtu akatupa pete kutoka kwenye nyara zake.
Ils répondirent: Nous te les donnerons avec empressement. Aussitôt, il déploya son manteau, et chacun y jeta les pendants d'oreilles de sa part de butin.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilikuwa shekeli 1, 700 za dhahabu. Nyara hizi zilikuwa ni pamoja na mapambo ya makoja, vidani, nguo ya rangi ya zambarau waliyovaa na wafalme wa Midiani, na zaidi ya minyororo iliyokuwa karibu na shingo za ngamia zao.
Le poids des pendants d'oreilles qu'il avait demandés, fut de dix-sept cents sicles d'or, outre les bossettes, les torsades, les vêtements et les robes de pourpre que portaient les rois de Madian, et les ornements qui entouraient le cou de leurs chameaux.
27 Gideoni akafanya efodi kutoka katika pete na kuiweka katika mji wake, huko Ofra, na Israeli wote wakaiandama kwa ukahaba na kuabudu. Ilikuwa mtego kwa Gideoni na kwa wale walio nyumbani kwake.
Gédéon en fit un éphod, et il le plaça en Ephratha, sa ville. Et là, tout Israël se prostitua à l'occasion de cet éphod, qui fut une pierre d'achoppement pour Gédéon et pour sa famille.
28 Kwa hiyo Midiani ilishindwa mbele ya watu wa Israeli na hawakuinua vichwa vyao tena. Na nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini siku za Gideoni.
Et Madian fut réduit à rien devant les fils d'Israël; il ne continua plus de relever la tête, et la terre fut en repos quarante années durant les jours de Gédéon.
29 Yerubaali, mwana wa Yoashi, akaenda akakaa nyumbani kwake.
Jérobaal, fils de Joas, s'en retourna, et demeura dans sa maison.
30 Gideoni alikuwa na wana sabini, waliokuwa uzao wake, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
Il avait soixante-dix fils, nés de lui, parce qu'il avait beaucoup de femmes.
31 Mwanamke wake, aliyekuwa Shekemu, akamzaa pia mwana, na Gideoni akampa jina lake Abimeleki.
Il avait aussi une concubine à Sichem, et celle-là, pareillement, lui donna un fils, qu'elle nomma Abimélech.
32 Gideoni, mwana wa Yoashi, akafa katika uzee mzuri, akazikwa huko Ofra katika kaburi la baba yake Joashi, wa jamaa ya Abiyezeri.
Gédéon, fils de Joas, mourut en sa ville, et il fut enseveli dans le sépulcre de Joas, son père, en Ephratha d'Abi-Esdri.
33 Ikawa, Gideoni alipokufa, watu wa Israeli wakageuka tena na kujifanyia ukahaba wenyewe kwa kuabudu Mabaali. Wamlifanya Baali Berith kuwa mungu wao.
Gédéon mort, les fils d'Israël se pervertirent; ils se prostituèrent aux Baal, et ils firent alliance avec Baal afin qu'il fut leur dieu.
34 Watu wa Israeli hawakukumbuka kumtukuza Bwana, Mungu wao, aliyewaokoa kutoka kwa mikono ya adui zao kila upande.
Et les fils d'Israël ne se souvinrent plus du Seigneur, du Dieu qui les avait délivrés des mains de tous ceux d'alentour qui les opprimaient.
35 Hawakuweka ahadi zao kwa nyumba ya Yerubaali (yaani Gidioni), kwa ajili ya mema yote aliyoyafanya katika Israeli.
Et ils furent sans égard pour la maison de Jérobaal (le même que Gédéon), et ils oublièrent le bien que celui-ci avait fait à Israël.

< Waamuzi 8 >