< Waamuzi 8 >

1 Watu wa Efraimu wakamwambia Gideoni, “Ni nini hiki umetutenda? Haukuita wakati ulipokwenda kupigana na Midiani.” Wakamwambia kwa nguvu.
The men of Ephraim said to Gideon, “What is this you have done to us? You did not call us when you went to fight against Midian.” Then they had a violent argument with him.
2 Akawaambia, “Nimefanya nini sasa kulinganisha na mlichofanya ninyi? Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?
He said to them, “What have I done now compared to you? Are not the gleanings of Ephraim's grapes better than the full grape harvest of Abiezer?
3 Mungu amewapa ushindi juu ya wakuu wa Midiani-Orebu na Zeeb! Mimi nimefanya nini ukilinganisha na ninyi?” Hasira yao ikashuka chini aliposema hili.
God has given you victory over the princes of Midian—Oreb and Zeeb! What have I accomplished compared to you?” Their anger toward him died down when he said this.
4 Gideoni alikuja Yordani na akavuka juu yake, yeye na watu mia tatu waliokuwa pamoja naye. Walikuwa wamechoka, lakini bado waliendelea kufuatilia.
Gideon came to the Jordan and crossed over it, he and the three hundred men who were with him. They were exhausted, yet they still kept up the pursuit.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali wape mikate kwa watu wanaonifuata, kwa kuwa wamechoka, nami niwafuatilia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.
He said to the men of Succoth, “Please give loaves of bread to the people who follow me, for they are exhausted, and I am pursuing Zebah and Zalmunna, the kings of Midian.”
6 Na wakuu wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna sasa ipo mikononi mwako? Kwa nini tulipe jeshi lako mikate?”
Then the officials said, “Are the hands of Zebah and Zalmunna now in your hand? Why should we give bread to your army?”
7 Gideoni akasema, “Bwana akitupa ushindi juu ya Zeba na Salmunna, nitainyunyiza ngozi yenu kwa miiba ya jangwani na michongoma.
Gideon said, “When Yahweh has given us victory over Zebah and Zalmunna, I will tear your skin with the desert thorns and briers.”
8 Akatoka huko, akaenda Penieli, akawaambia watu maneno hayo hayo; lakini watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyojibu.
He went up from there to Peniel and spoke to the people there in the same way, but the men of Peniel answered him just as the men of Succoth had answered.
9 Akawaambia pia watu wa Penieli, akasema, “Nitakapokuja kwa amani, nitauangusha mnara huu.”
He spoke also to the men of Peniel and said, “When I come again in peace, I will pull down this tower.”
10 Sasa Zeba na Salmuna walikuwa huko Karkori pamoja na jeshi lao, karibu na watu elfu kumi na tano, wote waliosalia nje ya jeshi lote la watu wa Mashariki, kwa kuwa walianguka watu 120, 000 waliofundishwa kupigana na upanga.
Now Zebah and Zalmunna were in Karkor with their army, about fifteen thousand men, all who remained out of the entire army of the people of the East, for there had fallen 120,000 men who drew the sword.
11 Gideoni akapanda barabara iliyochukuliwa na wakaazi wa hema, Noba na Yogbena. Akalishinda jeshi la adui, kwa sababu hawakuwa wanatarajia shambulio.
Gideon went up the road taken by tent dwellers, past Nobah and Jogbehah. He defeated the enemy army, because they were not expecting an attack.
12 Zeba na Salmuna walikimbia, na Gideoni alipowafuata, akawatwaa wafalme wawili wa Midiani-Zeba na Salmunna- na kulifanya jeshi lote kuwa na hofu.
Zebah and Zalmunna fled, and as Gideon pursued them, he captured the two kings of Midian—Zebah and Zalmunna—and set their whole army into a panic.
13 Gideoni, mwana wa Yoashi, alirudi kutoka kwenye vita kwenda kupitia Heresi.
Gideon, son of Joash, returned from the battle going through the pass of Heres.
14 Akamkimbilia kijana mmoja wa watu wa Sukothi na kutafuta ushauri kutoka kwake. Kijana huyo alimwelezea viongozi wa Sukothi na wazee wake, watu sabini na saba.
He caught a young man of Succoth and questioned him. The young man wrote down the names of seventy-seven officials and elders of Succoth.
15 Gideoni akaja kwa watu wa Sukothi, akasema, “Tazameni Zeba na Salmuna, ambao mlinidhihaki kwa ajili yao, nikasema, 'Je! mmemshinda Zeba na Salmuna? Hatujui kwamba tunapaswa kulipa jeshi lako mkate.”
Gideon came to the men of Succoth and said, “Look at Zebah and Zalmunna, about whom you mocked me and said, 'Have you already conquered Zebah and Zalmunna? We do not know that we should give bread to your army.'”
16 Gideoni akawachukua wazee wa mji, naye akawaadhibu watu wa Sukothi pamoja na miiba ya jangwa na michongoma.
Gideon took the elders of the city, and he punished the men of Succoth with the desert thorns and briers.
17 Akaangusha mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji huo.
Then he pulled down the tower of Peniel and killed the men of that city.
18 Gideoni akamwambia Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliwauawa Tabori?” Wakajibu, “Kama wewe ulivyo, ndivyo walivyokuwa. Kila mmoja wao alionekana kama mwana wa mfalme.”
Then Gideon said to Zebah and Zalmunna, “What kind of men did you kill at Tabor?” They answered, “As you are, so were they. Every one of them looked like the son of a king.”
19 Gideoni akasema, 'Wao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama Bwana anaishivyo, kama mngewaacha hai, nisingewauwa.”
Gideon said, “They were my brothers, the sons of my mother. As Yahweh lives, if you had saved them alive, I would not kill you.”
20 Akamwambia Yetheri (mzaliwa wake wa kwanza), “Simama uwaue!” Lakini kijana huyo hakutoa upanga wake kwa kuwa aliogopa, kwa sababu alikuwa bado kijana mdogo.
He said to Jether (his firstborn), “Get up and kill them!” But the young man did not draw his sword for he was afraid, because he was still a young boy.
21 Ndipo Zeba na Salmuna wakasema, simama mwenyewe, utuue! Kwa maana kama mtu alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake. Gideoni akasimama na kumwua Zeba na Salmuna. Pia aliondoa mapambo yaliyokuwa juu ya shingo za ngamia zao.
Then Zebah and Zalmunna said, “Get up yourself and kill us! For as the man is, so is his strength.” Gideon rose and killed Zebah and Zalmunna. He also took off the crescent-shaped ornaments that were on their camels' necks.
22 Ndipo wana wa Israeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, mtoto wako, na mjukuu wako; kwa sababu umetuokoa mikononi mwa Midiani.”
Then the men of Israel said to Gideon, “Rule over us—you, your son, and your grandson—because you have saved us out of the hand of Midian.”
23 Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala mtoto wangu hatatawala juu yenu. Bwana atatawala juu yenu.”
Gideon said to them, “I will not rule over you, neither will my son rule over you. Yahweh will rule over you.”
24 Gideoni akawaambia, “Nina haja yangu niitakayo kwenu kwamba kila mmoja wenu atanipe pete kutoka kwenye nyara zake.” (Wamidiani walikuwa na pete za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)
Gideon said to them, “Let me make a request of you: Every one of you would give me the earrings from his plunder.” (The Midianites had golden earrings because they were Ishmaelites.)
25 Wakamjibu, “Tunafurahi kukupa.” Wakatandika vazi na kila mtu akatupa pete kutoka kwenye nyara zake.
They answered, “We are glad to give them to you.” They spread out a cloak and every man threw on it the earrings from his plunder.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilikuwa shekeli 1, 700 za dhahabu. Nyara hizi zilikuwa ni pamoja na mapambo ya makoja, vidani, nguo ya rangi ya zambarau waliyovaa na wafalme wa Midiani, na zaidi ya minyororo iliyokuwa karibu na shingo za ngamia zao.
The weight of the golden earrings that he requested was 1,700 shekels of gold. This plunder was in addition to the crescent ornaments, the pendants, the purple clothing that was worn by the kings of Midian, and in addition to the chains that had been around their camels' necks.
27 Gideoni akafanya efodi kutoka katika pete na kuiweka katika mji wake, huko Ofra, na Israeli wote wakaiandama kwa ukahaba na kuabudu. Ilikuwa mtego kwa Gideoni na kwa wale walio nyumbani kwake.
Gideon made an ephod out of the earrings and put it in his city, in Ophrah, and all Israel prostituted themselves by worshiping it there. It became a trap for Gideon and for those in his house.
28 Kwa hiyo Midiani ilishindwa mbele ya watu wa Israeli na hawakuinua vichwa vyao tena. Na nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini siku za Gideoni.
So Midian was subdued before the people of Israel and they did not raise their heads up again. So the land had peace for forty years in the days of Gideon.
29 Yerubaali, mwana wa Yoashi, akaenda akakaa nyumbani kwake.
Jerub Baal, son of Joash, went and lived in his own house.
30 Gideoni alikuwa na wana sabini, waliokuwa uzao wake, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
Gideon had seventy sons who were his descendants, for he had many wives.
31 Mwanamke wake, aliyekuwa Shekemu, akamzaa pia mwana, na Gideoni akampa jina lake Abimeleki.
His concubine, who was in Shechem, also bore him a son, and Gideon gave him the name Abimelech.
32 Gideoni, mwana wa Yoashi, akafa katika uzee mzuri, akazikwa huko Ofra katika kaburi la baba yake Joashi, wa jamaa ya Abiyezeri.
Gideon, son of Joash, died at a good old age and was buried in the tomb of Joash his father, at Ophrah of the clan of Abiezer.
33 Ikawa, Gideoni alipokufa, watu wa Israeli wakageuka tena na kujifanyia ukahaba wenyewe kwa kuabudu Mabaali. Wamlifanya Baali Berith kuwa mungu wao.
It came about, as soon as Gideon was dead, the people of Israel turned again and prostituted themselves by worshiping the Baals. They made Baal-Berith their god.
34 Watu wa Israeli hawakukumbuka kumtukuza Bwana, Mungu wao, aliyewaokoa kutoka kwa mikono ya adui zao kila upande.
The people of Israel did not remember to honor Yahweh, their God, who had rescued them from the hand of all their enemies on every side.
35 Hawakuweka ahadi zao kwa nyumba ya Yerubaali (yaani Gidioni), kwa ajili ya mema yote aliyoyafanya katika Israeli.
They did not keep their promises to the house of Jerub Baal (that is, Gideon), in return for all the good he had done in Israel.

< Waamuzi 8 >