< Waamuzi 8 >

1 Watu wa Efraimu wakamwambia Gideoni, “Ni nini hiki umetutenda? Haukuita wakati ulipokwenda kupigana na Midiani.” Wakamwambia kwa nguvu.
Then the descendants of Ephraim said to Gideon, “Why have you acted toward us like this? When you went out to fight against the people of Midian, why did you not summon us [to help you]?” They rebuked Gideon severely.
2 Akawaambia, “Nimefanya nini sasa kulinganisha na mlichofanya ninyi? Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?
But Gideon replied, “I have done [RHQ] very little compared with what you have done! My small clan of descendants of Abiezer only started the battle, but [your very large group of] descendants of Ephraim [helped me to finish the task very well. It is like] the final grapes of the harvest being much better than the first grapes that are picked.
3 Mungu amewapa ushindi juu ya wakuu wa Midiani-Orebu na Zeeb! Mimi nimefanya nini ukilinganisha na ninyi?” Hasira yao ikashuka chini aliposema hili.
God enabled you to defeat Oreb and Zeeb, the generals of the army from Midian. That is [RHQ] much more important than what I did!” After Gideon told them that, they no longer resented what he had done.
4 Gideoni alikuja Yordani na akavuka juu yake, yeye na watu mia tatu waliokuwa pamoja naye. Walikuwa wamechoka, lakini bado waliendelea kufuatilia.
Then Gideon and his 300 men [went east and] crossed the Jordan [River]. Although they were very tired, they continued to pursue their enemies.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali wape mikate kwa watu wanaonifuata, kwa kuwa wamechoka, nami niwafuatilia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.
When they arrived at Succoth [town], Gideon said to the town leaders, “Please give my men some food! They are very tired. We are pursuing Zebah and Zalmunna, the kings of Midian.”
6 Na wakuu wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna sasa ipo mikononi mwako? Kwa nini tulipe jeshi lako mikate?”
But the leaders of Succoth replied, “You have not caught [RHQ] Zebah and Zalmunna yet. So why should we give food to your troops [now? Catch them first, and then we will give you food].”
7 Gideoni akasema, “Bwana akitupa ushindi juu ya Zeba na Salmunna, nitainyunyiza ngozi yenu kwa miiba ya jangwani na michongoma.
Gideon replied, “[Because you said that], after Yahweh enables us to defeat Zebah and Zalmunna, we will return. And then we will make whips from thorns from the desert, and with them we will rip the flesh off your bones!”
8 Akatoka huko, akaenda Penieli, akawaambia watu maneno hayo hayo; lakini watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyojibu.
From there, Gideon [and his 300 men] went to Peniel and asked for food there, but the people gave him the same answer.
9 Akawaambia pia watu wa Penieli, akasema, “Nitakapokuja kwa amani, nitauangusha mnara huu.”
So he said to the men of Peniel, “After I defeat those kings, I will return and tear down this tower!”
10 Sasa Zeba na Salmuna walikuwa huko Karkori pamoja na jeshi lao, karibu na watu elfu kumi na tano, wote waliosalia nje ya jeshi lote la watu wa Mashariki, kwa kuwa walianguka watu 120, 000 waliofundishwa kupigana na upanga.
By that time, Zebah and Zalmunna had gone to Karkor [town] with 15,000 troops. They were all that were left of the armies that had come from the east. 120,000 of their men had already been killed.
11 Gideoni akapanda barabara iliyochukuliwa na wakaazi wa hema, Noba na Yogbena. Akalishinda jeshi la adui, kwa sababu hawakuwa wanatarajia shambulio.
Gideon [and his men] went east along the road on which caravans travel. They went past Nobah and Jogbehah [villages] and arrived at the enemy camp by surprise.
12 Zeba na Salmuna walikimbia, na Gideoni alipowafuata, akawatwaa wafalme wawili wa Midiani-Zeba na Salmunna- na kulifanya jeshi lote kuwa na hofu.
Zebah and Zalmunna fled, but Gideon’s men pursued them and captured them and all their warriors.
13 Gideoni, mwana wa Yoashi, alirudi kutoka kwenye vita kwenda kupitia Heresi.
After that, Gideon and his men [took Zebah and Zalmunna with them and] started to return, going through Heres Pass.
14 Akamkimbilia kijana mmoja wa watu wa Sukothi na kutafuta ushauri kutoka kwake. Kijana huyo alimwelezea viongozi wa Sukothi na wazee wake, watu sabini na saba.
There he captured a young man from Succoth, and demanded that he write down the names of all of the leaders in the town. The young man wrote down seventy-seven names.
15 Gideoni akaja kwa watu wa Sukothi, akasema, “Tazameni Zeba na Salmuna, ambao mlinidhihaki kwa ajili yao, nikasema, 'Je! mmemshinda Zeba na Salmuna? Hatujui kwamba tunapaswa kulipa jeshi lako mkate.”
Then Gideon and his men returned to Succoth and said to those leaders, “Here are Zebah and Zalmunna. When we were here before, you made fun of me and said ‘You have not [RHQ] caught Zebah and Zalmunna yet! After you catch them, we will give your exhausted men some food.’”
16 Gideoni akawachukua wazee wa mji, naye akawaadhibu watu wa Sukothi pamoja na miiba ya jangwa na michongoma.
Then Gideon’s men took the town leaders and whipped them with whips made from briers from the desert, to teach them [that they deserved to be punished for not giving them any food].
17 Akaangusha mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji huo.
Then [they went to] Peniel and tore down the tower, and killed all the men in the town.
18 Gideoni akamwambia Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliwauawa Tabori?” Wakajibu, “Kama wewe ulivyo, ndivyo walivyokuwa. Kila mmoja wao alionekana kama mwana wa mfalme.”
Then Gideon said to Zebah and Zalmunna, “The men you killed near Tabor [Mountain], what did they look like?” They replied, “They were like you; they all looked like they were sons of a king.”
19 Gideoni akasema, 'Wao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama Bwana anaishivyo, kama mngewaacha hai, nisingewauwa.”
Gideon replied, “They were my brothers! Just as surely as Yahweh lives, I would not kill you if you had not killed them.”
20 Akamwambia Yetheri (mzaliwa wake wa kwanza), “Simama uwaue!” Lakini kijana huyo hakutoa upanga wake kwa kuwa aliogopa, kwa sababu alikuwa bado kijana mdogo.
Then he turned to his oldest son, Jether. He said to him, “Kill them!” But Jether was only a boy, and he was afraid, so he did not pull out his dagger [to kill them].
21 Ndipo Zeba na Salmuna wakasema, simama mwenyewe, utuue! Kwa maana kama mtu alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake. Gideoni akasimama na kumwua Zeba na Salmuna. Pia aliondoa mapambo yaliyokuwa juu ya shingo za ngamia zao.
Then Zebah and Zalmunna said to Gideon, “Do not ask a young boy to do the work that a man should do!” So Gideon killed both of them. Then he took the gold ornaments from the necks of their camels.
22 Ndipo wana wa Israeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, mtoto wako, na mjukuu wako; kwa sababu umetuokoa mikononi mwa Midiani.”
Then a group of Israeli men [came to] Gideon and said to him, “You be our ruler! [We want] you and your son and your grandsons [to] be our rulers, because you rescued us from the Midian army.”
23 Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala mtoto wangu hatatawala juu yenu. Bwana atatawala juu yenu.”
But Gideon replied, “No, I will not rule over you, and my son will not rule over you. Yahweh will rule over you.”
24 Gideoni akawaambia, “Nina haja yangu niitakayo kwenu kwamba kila mmoja wenu atanipe pete kutoka kwenye nyara zake.” (Wamidiani walikuwa na pete za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)
Then he said, “I request only one thing. I request that each of you give me one earring from the things you captured after the battle.” [All the men descended from Ishmael wore gold earrings.]
25 Wakamjibu, “Tunafurahi kukupa.” Wakatandika vazi na kila mtu akatupa pete kutoka kwenye nyara zake.
They replied, “We will be glad to give earrings to you!” So they spread a cloth [on the ground], and each man threw on it one gold earring that he had taken [from a man he had killed in the battle].
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilikuwa shekeli 1, 700 za dhahabu. Nyara hizi zilikuwa ni pamoja na mapambo ya makoja, vidani, nguo ya rangi ya zambarau waliyovaa na wafalme wa Midiani, na zaidi ya minyororo iliyokuwa karibu na shingo za ngamia zao.
The weight of all the earrings was (43 pounds/19.4 kg.). That did not include other things [that they gave to Gideon]—the other ornaments or the pendants or the clothes that the kings of Midian wore or the gold chains that were on the necks of their camels.
27 Gideoni akafanya efodi kutoka katika pete na kuiweka katika mji wake, huko Ofra, na Israeli wote wakaiandama kwa ukahaba na kuabudu. Ilikuwa mtego kwa Gideoni na kwa wale walio nyumbani kwake.
Gideon made/decorated a sacred vest from the gold, and later he put it in his hometown, Ophrah. But soon the Israeli people started to worship the vest. So it became like a trap [MET] for the people, [causing them to worship it instead of worshiping only God].
28 Kwa hiyo Midiani ilishindwa mbele ya watu wa Israeli na hawakuinua vichwa vyao tena. Na nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini siku za Gideoni.
That is how the Israelis defeated the people from Midian. The people of Midian did not become strong enough to attack Israel again. So while Gideon was alive, there was peace in the land for 40 years.
29 Yerubaali, mwana wa Yoashi, akaenda akakaa nyumbani kwake.
Gideon went back home to live there.
30 Gideoni alikuwa na wana sabini, waliokuwa uzao wake, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
He had many wives, and they bore him seventy sons.
31 Mwanamke wake, aliyekuwa Shekemu, akamzaa pia mwana, na Gideoni akampa jina lake Abimeleki.
He also had a slave wife in Shechem [town], who bore him a son whom he named Abimelech.
32 Gideoni, mwana wa Yoashi, akafa katika uzee mzuri, akazikwa huko Ofra katika kaburi la baba yake Joashi, wa jamaa ya Abiyezeri.
Gideon died when he was very old. They buried his body in the grave where his father Joash was buried, at Ophrah, in the land belonging to the descendants of Abiether.
33 Ikawa, Gideoni alipokufa, watu wa Israeli wakageuka tena na kujifanyia ukahaba wenyewe kwa kuabudu Mabaali. Wamlifanya Baali Berith kuwa mungu wao.
But as soon as Gideon died, the Israelis [stopped worshiping God and started worshiping the images of the god Baal, like] [MET] adultresses [leave their husbands and go to sleep with other men]. They made a [statue of a] new god called Baal-Berith.
34 Watu wa Israeli hawakukumbuka kumtukuza Bwana, Mungu wao, aliyewaokoa kutoka kwa mikono ya adui zao kila upande.
They forgot about Yahweh, the one who had rescued them from all their enemies that surrounded them.
35 Hawakuweka ahadi zao kwa nyumba ya Yerubaali (yaani Gidioni), kwa ajili ya mema yote aliyoyafanya katika Israeli.
And even though Gideon had done many good things for the Israelis, they were not kind to Gideon’s family.

< Waamuzi 8 >