< Waamuzi 8 >

1 Watu wa Efraimu wakamwambia Gideoni, “Ni nini hiki umetutenda? Haukuita wakati ulipokwenda kupigana na Midiani.” Wakamwambia kwa nguvu.
And the men of Ephraim said unto him—What is this thing thou hast done to us, in not calling us, when thou wentest to fight with Midian? And they did chide with him, sharply.
2 Akawaambia, “Nimefanya nini sasa kulinganisha na mlichofanya ninyi? Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?
And he said unto them, What have I done, now, in comparison with you? Is not the grape-gleaning of Ephraim better than the vintage of Abiezer?
3 Mungu amewapa ushindi juu ya wakuu wa Midiani-Orebu na Zeeb! Mimi nimefanya nini ukilinganisha na ninyi?” Hasira yao ikashuka chini aliposema hili.
Into your hand, hath God delivered the princes of Midian—Oreb and Zeeb, what then had I been able to do in comparison with you? Then, was their spirit softened toward him, when he had spoken this word.
4 Gideoni alikuja Yordani na akavuka juu yake, yeye na watu mia tatu waliokuwa pamoja naye. Walikuwa wamechoka, lakini bado waliendelea kufuatilia.
And Gideon came towards the Jordan, being about to pass over—he, and the three hundred men who were with him, faint yet pursuing.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali wape mikate kwa watu wanaonifuata, kwa kuwa wamechoka, nami niwafuatilia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.
So he said unto the men of Succoth, Give, I pray you, loaves of bread to the people that are following me; for, faint, they are, and, I, am in pursuit of Zebah and Zalmunna, kings of Midian.
6 Na wakuu wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna sasa ipo mikononi mwako? Kwa nini tulipe jeshi lako mikate?”
And the princes of Succoth said, Are the palms of the hands of Zebah and Zalmunna already in thy power, —that we should give to thine army bread?
7 Gideoni akasema, “Bwana akitupa ushindi juu ya Zeba na Salmunna, nitainyunyiza ngozi yenu kwa miiba ya jangwani na michongoma.
And Gideon said, Therefore, when Yahweh hath delivered Zebah and Zalmunna into my power, then will I tear your flesh with the thorns of the wilderness, and with the nettles.
8 Akatoka huko, akaenda Penieli, akawaambia watu maneno hayo hayo; lakini watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyojibu.
So he went up from thence, to Penuel, and spake unto them in like manner, —and the men of Penuel answered him, as had answered the men of Succoth.
9 Akawaambia pia watu wa Penieli, akasema, “Nitakapokuja kwa amani, nitauangusha mnara huu.”
So he spake to the men of Penuel also, saying, —When I return with success, I will break down this tower.
10 Sasa Zeba na Salmuna walikuwa huko Karkori pamoja na jeshi lao, karibu na watu elfu kumi na tano, wote waliosalia nje ya jeshi lote la watu wa Mashariki, kwa kuwa walianguka watu 120, 000 waliofundishwa kupigana na upanga.
Now, Zebah and Zalmunna, were in Karkor, and their hosts with them, about fifteen thousand, all that were left out of all the host of the sons of the east, —and, the fallen, were a hundred and twenty thousand men, who had drawn the sword.
11 Gideoni akapanda barabara iliyochukuliwa na wakaazi wa hema, Noba na Yogbena. Akalishinda jeshi la adui, kwa sababu hawakuwa wanatarajia shambulio.
So Gideon went up by the way of the tent-dwellers, on the east of Nobah and Jogbehah, and smote the host, when, the host, had become secure.
12 Zeba na Salmuna walikimbia, na Gideoni alipowafuata, akawatwaa wafalme wawili wa Midiani-Zeba na Salmunna- na kulifanya jeshi lote kuwa na hofu.
And when Zebah and Zalmunna fled, then he pursued them, and captured the two kings of Midian—Zebah and Zalmunna, and, all the host, put he in terror.
13 Gideoni, mwana wa Yoashi, alirudi kutoka kwenye vita kwenda kupitia Heresi.
And Gideon son of Joash returned from the battle, —from the ascent of Heres;
14 Akamkimbilia kijana mmoja wa watu wa Sukothi na kutafuta ushauri kutoka kwake. Kijana huyo alimwelezea viongozi wa Sukothi na wazee wake, watu sabini na saba.
and caught a young man, of the men of Succoth, and enquired of him, —so he wrote down for him the princes of Succoth, and the elders thereof, seventy-seven men.
15 Gideoni akaja kwa watu wa Sukothi, akasema, “Tazameni Zeba na Salmuna, ambao mlinidhihaki kwa ajili yao, nikasema, 'Je! mmemshinda Zeba na Salmuna? Hatujui kwamba tunapaswa kulipa jeshi lako mkate.”
Then came he in unto the men of Succoth, and said, Lo! Zebah and Zalmunna, —concerning whom ye did taunt me, saying—Are the palms of the hands of Zebah and Zalmunna already in thy power, that we should give to thy weary men bread?
16 Gideoni akawachukua wazee wa mji, naye akawaadhibu watu wa Sukothi pamoja na miiba ya jangwa na michongoma.
So he took the elders of the city, and the thorns of the wilderness and the nettles, and taught therewith the men of Succoth:
17 Akaangusha mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji huo.
the tower of Penuel also, brake he down, —and slew the men of the city.
18 Gideoni akamwambia Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliwauawa Tabori?” Wakajibu, “Kama wewe ulivyo, ndivyo walivyokuwa. Kila mmoja wao alionekana kama mwana wa mfalme.”
Then said he unto Zebah and unto Zalmunna, What manner of men were they, whom ye slew at Tabor? And they said, As thou art, so were they, each one, as handsome as the sons of a king.
19 Gideoni akasema, 'Wao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama Bwana anaishivyo, kama mngewaacha hai, nisingewauwa.”
And he said: My brethren, sons of my mother, they were! As Yahweh liveth, if ye had saved them alive, I would not have slain you.
20 Akamwambia Yetheri (mzaliwa wake wa kwanza), “Simama uwaue!” Lakini kijana huyo hakutoa upanga wake kwa kuwa aliogopa, kwa sababu alikuwa bado kijana mdogo.
So he said to Jether his firstborn, Up! slay them. But the youth drew not his sword, for he feared, because he was yet a youth.
21 Ndipo Zeba na Salmuna wakasema, simama mwenyewe, utuue! Kwa maana kama mtu alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake. Gideoni akasimama na kumwua Zeba na Salmuna. Pia aliondoa mapambo yaliyokuwa juu ya shingo za ngamia zao.
Then said Zebah and Zalmunna—Up! thou, and fall upon us, for, like the man, is his might. So Gideon arose, and slew Zebah and Zalmunna, and took the crescents that were on the necks of their camels.
22 Ndipo wana wa Israeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, mtoto wako, na mjukuu wako; kwa sababu umetuokoa mikononi mwa Midiani.”
Then said the men of Israel, unto Gideon, Rule over us—even thou, and thy son, and thy son’s son, —for thou hast saved us out of the power of Midian.
23 Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala mtoto wangu hatatawala juu yenu. Bwana atatawala juu yenu.”
And Gideon said unto them, I, will not rule over you, neither shall my son rule over you, —Yahweh, shall rule over you.
24 Gideoni akawaambia, “Nina haja yangu niitakayo kwenu kwamba kila mmoja wenu atanipe pete kutoka kwenye nyara zake.” (Wamidiani walikuwa na pete za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)
And Gideon said unto them—I would make to you a request, Give me, then, every man the nose-ring of his spoil. For they had, nose-rings of gold, for, Ishmaelites, they were.
25 Wakamjibu, “Tunafurahi kukupa.” Wakatandika vazi na kila mtu akatupa pete kutoka kwenye nyara zake.
And they said, We will, freely give. So they spread out a mantle, and cast therein, every man the nose-ring of his spoil.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilikuwa shekeli 1, 700 za dhahabu. Nyara hizi zilikuwa ni pamoja na mapambo ya makoja, vidani, nguo ya rangi ya zambarau waliyovaa na wafalme wa Midiani, na zaidi ya minyororo iliyokuwa karibu na shingo za ngamia zao.
And so it was, that the weight of the nose-rings of gold which he requested, was a thousand and seven hundred [shekels] of gold, —besides the crescents, and the pendants, and the raiment of purple that were upon the kings of Midian, and besides the ornaments that were on the necks of their camels.
27 Gideoni akafanya efodi kutoka katika pete na kuiweka katika mji wake, huko Ofra, na Israeli wote wakaiandama kwa ukahaba na kuabudu. Ilikuwa mtego kwa Gideoni na kwa wale walio nyumbani kwake.
And Gideon made thereof an Ephod, and set it up in his own city, in Ophrah, and all Israel went unchastely astray after it there, —so it became, to Gideon and to his house, a snare.
28 Kwa hiyo Midiani ilishindwa mbele ya watu wa Israeli na hawakuinua vichwa vyao tena. Na nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini siku za Gideoni.
Thus was Midian subdued, before the sons of Israel, neither did they again lift up their head, —and the land had rest forty years, in the days of Gideon.
29 Yerubaali, mwana wa Yoashi, akaenda akakaa nyumbani kwake.
So then Jerubbaal, son of Joash, went and dwelt in his own house.
30 Gideoni alikuwa na wana sabini, waliokuwa uzao wake, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
And, Gideon, had seventy sons, sprung from his own loins, —for, many wives, had he.
31 Mwanamke wake, aliyekuwa Shekemu, akamzaa pia mwana, na Gideoni akampa jina lake Abimeleki.
And, his concubine who was in Shechem, she also, bare him a son, —and he gave him the name of Abimelech.
32 Gideoni, mwana wa Yoashi, akafa katika uzee mzuri, akazikwa huko Ofra katika kaburi la baba yake Joashi, wa jamaa ya Abiyezeri.
And Gideon, son of Joash, died in a good old age, —and was buried in the grave of Joash his father, in Ophrah, of the Abiezrites.
33 Ikawa, Gideoni alipokufa, watu wa Israeli wakageuka tena na kujifanyia ukahaba wenyewe kwa kuabudu Mabaali. Wamlifanya Baali Berith kuwa mungu wao.
And it came to pass that, as soon as Gideon was dead, the sons of Israel turned back, and went unchastely astray after the Baals, —and appointed them Baal-berith, to be god:
34 Watu wa Israeli hawakukumbuka kumtukuza Bwana, Mungu wao, aliyewaokoa kutoka kwa mikono ya adui zao kila upande.
so the sons of Israel remembered not Yahweh, their own God, —who had rescued them out of the hand of all their enemies, on every side;
35 Hawakuweka ahadi zao kwa nyumba ya Yerubaali (yaani Gidioni), kwa ajili ya mema yote aliyoyafanya katika Israeli.
neither dealt they in lovingkindness with the house of Jerubbaal [namely] Gideon, —according to all the goodness wherewith he had dealt with Israel.

< Waamuzi 8 >