< Waamuzi 8 >

1 Watu wa Efraimu wakamwambia Gideoni, “Ni nini hiki umetutenda? Haukuita wakati ulipokwenda kupigana na Midiani.” Wakamwambia kwa nguvu.
Then the men of Ephraim sayde vnto him, Why hast thou serued vs thus that thou calledst vs not, when thou wentest to fight with the Midianites? and they chode with him sharply.
2 Akawaambia, “Nimefanya nini sasa kulinganisha na mlichofanya ninyi? Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?
To whom he said, What haue I now done in comparison of you? is not the gleaning of grapes of Ephraim better, then the vintage of Abiezer?
3 Mungu amewapa ushindi juu ya wakuu wa Midiani-Orebu na Zeeb! Mimi nimefanya nini ukilinganisha na ninyi?” Hasira yao ikashuka chini aliposema hili.
God hath deliuered into your handes the princes of Midian, Oreb and Zeeb: and what was I able to do in comparison of you? and when he had thus spoken, then their spirits abated toward him.
4 Gideoni alikuja Yordani na akavuka juu yake, yeye na watu mia tatu waliokuwa pamoja naye. Walikuwa wamechoka, lakini bado waliendelea kufuatilia.
And Gideon came to Iorden to passe ouer, hee, and the three hundreth men that were with him, weary, yet pursuing them.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali wape mikate kwa watu wanaonifuata, kwa kuwa wamechoka, nami niwafuatilia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.
And he said vnto the men of Succoth, Giue, I pray you, morsels of bread vnto the people that follow me (for they be wearie) that I may follow after Zebah, and Zalmunna Kings of Midian.
6 Na wakuu wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna sasa ipo mikononi mwako? Kwa nini tulipe jeshi lako mikate?”
And the princes of Succoth sayde, Are the handes of Zebah and Zalmunna nowe in thine hads, that we should giue bread vnto thine army?
7 Gideoni akasema, “Bwana akitupa ushindi juu ya Zeba na Salmunna, nitainyunyiza ngozi yenu kwa miiba ya jangwani na michongoma.
Gideon then sayde, Therefore when the Lord hath deliuered Zebah and Zalmunna into mine hand, I will teare your flesh with thornes of the wildernes and with breers.
8 Akatoka huko, akaenda Penieli, akawaambia watu maneno hayo hayo; lakini watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyojibu.
And he went vp thence to Penuel, and spake vnto them likewise, and the men of Penuel answered him, as the men of Succoth answered.
9 Akawaambia pia watu wa Penieli, akasema, “Nitakapokuja kwa amani, nitauangusha mnara huu.”
And he sayd also vnto the men of Penuel, When I come againe in peace, I will breake downe this towre.
10 Sasa Zeba na Salmuna walikuwa huko Karkori pamoja na jeshi lao, karibu na watu elfu kumi na tano, wote waliosalia nje ya jeshi lote la watu wa Mashariki, kwa kuwa walianguka watu 120, 000 waliofundishwa kupigana na upanga.
Now Zebah and Zalmunna were in Karkor, and their hostes with them, about fifteene thousande, all that were left of all the hostes of them of the East: for there was slaine an hundreth and twentie thousand men, that drew swordes.
11 Gideoni akapanda barabara iliyochukuliwa na wakaazi wa hema, Noba na Yogbena. Akalishinda jeshi la adui, kwa sababu hawakuwa wanatarajia shambulio.
And Gideon went through them that dwelt in Tabernacles on the East side of Nobah and Iogbehah, and smote the hoste: for the hoste was carelesse.
12 Zeba na Salmuna walikimbia, na Gideoni alipowafuata, akawatwaa wafalme wawili wa Midiani-Zeba na Salmunna- na kulifanya jeshi lote kuwa na hofu.
And when Zebah and Zalmunna fled, hee followed after them, and tooke the two kings of Midian, Zebah and Zalmunna, and discomfited all the hoste.
13 Gideoni, mwana wa Yoashi, alirudi kutoka kwenye vita kwenda kupitia Heresi.
So Gideon the sonne of Ioash returned from battel, the sunne being yet hie,
14 Akamkimbilia kijana mmoja wa watu wa Sukothi na kutafuta ushauri kutoka kwake. Kijana huyo alimwelezea viongozi wa Sukothi na wazee wake, watu sabini na saba.
And tooke a seruant of the me of Succoth, and inquired of him: and he wrote to him the princes of Succoth and the Elders thereof, euen seuentie and seuen men.
15 Gideoni akaja kwa watu wa Sukothi, akasema, “Tazameni Zeba na Salmuna, ambao mlinidhihaki kwa ajili yao, nikasema, 'Je! mmemshinda Zeba na Salmuna? Hatujui kwamba tunapaswa kulipa jeshi lako mkate.”
And he came vnto the men of Succoth, and sayd, Behold Zebah and Zalmunna, by whome ye vpbrayded me, saying, Are the hands of Zebah and Zalmunna already in thine hands, that we should giue bread vnto thy weary men?
16 Gideoni akawachukua wazee wa mji, naye akawaadhibu watu wa Sukothi pamoja na miiba ya jangwa na michongoma.
Then he tooke the Elders of the citie, and thornes of the wildernes and breers, and did teare the men of Succoth with them.
17 Akaangusha mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji huo.
Also he brake downe the towre of Penuel, and slew the men of the citie.
18 Gideoni akamwambia Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliwauawa Tabori?” Wakajibu, “Kama wewe ulivyo, ndivyo walivyokuwa. Kila mmoja wao alionekana kama mwana wa mfalme.”
Then saide he vnto Zebah and Zalmunna, What maner of men were they, whom ye slew at Tabor? and they answered, As thou art, so were they: euery one was like the children of a King.
19 Gideoni akasema, 'Wao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama Bwana anaishivyo, kama mngewaacha hai, nisingewauwa.”
And he said, They were my brethren, euen my mothers children: as the Lord liueth, if ye had saued their liues, I would not slay you.
20 Akamwambia Yetheri (mzaliwa wake wa kwanza), “Simama uwaue!” Lakini kijana huyo hakutoa upanga wake kwa kuwa aliogopa, kwa sababu alikuwa bado kijana mdogo.
Then he sayde vnto Iether his first borne sonne, Vp, and slay them: but the boy drew not his sword: for he feared, because he was yet yong.
21 Ndipo Zeba na Salmuna wakasema, simama mwenyewe, utuue! Kwa maana kama mtu alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake. Gideoni akasimama na kumwua Zeba na Salmuna. Pia aliondoa mapambo yaliyokuwa juu ya shingo za ngamia zao.
Then Zebah and Zalmunna sayd, Rise thou, and fall vpon vs: for as the man is, so is his strength. And Gideon arose and slew Zebah and Zalmunna, and tooke away the ornamentes, that were on their camels neckes.
22 Ndipo wana wa Israeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, mtoto wako, na mjukuu wako; kwa sababu umetuokoa mikononi mwa Midiani.”
Then the men of Israel sayd vnto Gideon, Reigne thou ouer vs, both thou, and thy sonne, and thy sonnes sonne: for thou hast deliuered vs out of the hand of Midian.
23 Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala mtoto wangu hatatawala juu yenu. Bwana atatawala juu yenu.”
And Gideon sayde vnto them, I will not reigne ouer you, neither shall my childe reigne ouer you, but the Lord shall reigne ouer you.
24 Gideoni akawaambia, “Nina haja yangu niitakayo kwenu kwamba kila mmoja wenu atanipe pete kutoka kwenye nyara zake.” (Wamidiani walikuwa na pete za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)
Againe Gideon sayd vnto them, I would desire a request of you, that you would giue mee euery man the earings of his pray (for they had golden earings because they were Ismaelites)
25 Wakamjibu, “Tunafurahi kukupa.” Wakatandika vazi na kila mtu akatupa pete kutoka kwenye nyara zake.
And they answered, Wee will giue them. And they spred a garment, and did cast therein euery man the earings of his pray.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilikuwa shekeli 1, 700 za dhahabu. Nyara hizi zilikuwa ni pamoja na mapambo ya makoja, vidani, nguo ya rangi ya zambarau waliyovaa na wafalme wa Midiani, na zaidi ya minyororo iliyokuwa karibu na shingo za ngamia zao.
And the weight of the golden earings that he required, was a thousande and seuen hundreth shekels of golde, beside collers and iewels, and purple rayment that was on the kings of Midian, and beside the cheynes that were about their camels neckes.
27 Gideoni akafanya efodi kutoka katika pete na kuiweka katika mji wake, huko Ofra, na Israeli wote wakaiandama kwa ukahaba na kuabudu. Ilikuwa mtego kwa Gideoni na kwa wale walio nyumbani kwake.
And Gideon made an Ephod thereof, and put it in Ophrah his citie: and all Israel went a whoring there after it, which was the destruction of Gideon and his house.
28 Kwa hiyo Midiani ilishindwa mbele ya watu wa Israeli na hawakuinua vichwa vyao tena. Na nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini siku za Gideoni.
Thus was Midian brought lowe before the children of Israel, so that they lift vp their heads no more: and the countrey was in quietnes fourtie yeeres in the dayes of Gideon.
29 Yerubaali, mwana wa Yoashi, akaenda akakaa nyumbani kwake.
Then Ierubbaal the sonne of Ioash went, and dwelt in his owne house.
30 Gideoni alikuwa na wana sabini, waliokuwa uzao wake, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
And Gideon had seuentie sonnes begotten of his body: for he had many wiues.
31 Mwanamke wake, aliyekuwa Shekemu, akamzaa pia mwana, na Gideoni akampa jina lake Abimeleki.
And his concubine that was in Shechem, bare him a sonne also, whose name he called Abimelech.
32 Gideoni, mwana wa Yoashi, akafa katika uzee mzuri, akazikwa huko Ofra katika kaburi la baba yake Joashi, wa jamaa ya Abiyezeri.
So Gideon the sonne of Ioash dyed in a good age, and was buried in the sepulchre of Ioash his father in Ophrah, of the father of ye Ezrites.
33 Ikawa, Gideoni alipokufa, watu wa Israeli wakageuka tena na kujifanyia ukahaba wenyewe kwa kuabudu Mabaali. Wamlifanya Baali Berith kuwa mungu wao.
But when Gideon was dead, the children of Israel turned away and went a whoring after Baalim, and made Baal-berith their God.
34 Watu wa Israeli hawakukumbuka kumtukuza Bwana, Mungu wao, aliyewaokoa kutoka kwa mikono ya adui zao kila upande.
And the children of Israel remembred not the Lord their God, which had deliuered the out of the hands of all their enemies on euery side.
35 Hawakuweka ahadi zao kwa nyumba ya Yerubaali (yaani Gidioni), kwa ajili ya mema yote aliyoyafanya katika Israeli.
Neither shewed they mercy on the house of Ierubbaal, or Gideon, according to al the goodnesse which he had shewed vnto Israel.

< Waamuzi 8 >