< Waamuzi 3 >

1 Sasa Bwana aliyaacha mataifa haya yaijaribu Israeli, yaani kila mtu katika Israeli ambaye hakushiriki vita yoyote huko Kanaani.
Dette var de Folkeslag, HERREN lod blive tilbage for ved dem at sætte Israel Prøve, alle de Israeliter, som ikke havde kendt til Kampene om Kana'an,
2 (Alifanya hivyo ili kuwafundisha vita kizazi kipya cha Waisraeli ambao hawakujua kabla).
alene for Israeliternes Slægters Skyld, for at øve dem i Krig, alene for deres Skyld, som ikke havde kendt noget til de tidligere Krige:
3 Haya ndio mataifa: wafalme watano kutoka kwa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, na Wahivi waliokaa milima ya Lebanoni, kutoka Mlima Baali Hermoni hadi Hamathi.
De fem Filisterfyrster, alle Kana'anæerne, Zidonierne og Hetiterne, som boede i Libanons Bjerge fra Ba'al-Hermon til hen imod Hamat.
4 Mataifa haya yaliachwa kama njia ambayo Bwana angeijaribu Israeli, kuthibitisha kama watazitii amri alizowapa babu zao kupitia Musa.
De blev tilbage, for at Israel ved dem kunde blive sat paa Prøve, saa det kunde komme for Dagen, om de vilde lyde de Bud, HERREN havde givet deres Fædre ved Moses.
5 Basi wana wa Israeli wakakaa kati ya Wakanaani, na Wahiti, na Waamori, na Waperizi, na Wahivi, na Wayebusi.
Og Israeliterne boede blandt Kana'anæerne, Hetiterne, Amoriterne, Perizziterne, Hivviterne og Jebusiterne.
6 Waliwachukua binti zao kuwa wake zao, nao wakawapa wana wao binti zao, nao wakaitumikia miungu yao.
De indgik Ægteskab med deres Døtre og gav deres Sønner deres Døtre til Ægte, og de dyrkede deres Guder.
7 Wana wa Israeli walifanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wakamsahau Bwana, Mungu wao. Waliabudu Baali na Asherah.
Israeliterne gjorde, hvad der var ondt i HERRENS Øjne; de glemte HERREN deres Gud og dyrkede Ba'alerne og Asjererne.
8 Basi, hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawauza mkononi mwa Kushan-rishathaimu mfalme wa Aram Naharaimu. Watu wa Israeli walitumikia Kushan Rishathaimu kwa miaka nane.
Da blussede HERRENS Vrede op imod Israel, og han gav dem til Pris for Kong Kusjan-Risj'atajim af Aram-Naharajim, og Israeliterne stod under Kusjan-Risj'atajim i otte Aar.
9 Watu wa Israeli walipomwomba Bwana, Bwana akamuinua mtu atakayewasaidia wana wa Israeli, na mtu atakayewaokoa: Othnieli mwana wa Kenazi (ndugu mdogo wa Kalebu).
Da raabte Israeliterne til HERREN, og HERREN lod en Befrier fremstaa iblandt Israeliterne, og han frelste dem, nemlig Kenizziten Otniel, Kalebs yngre Broder.
10 Roho wa Bwana akamtia nguvu, naye akahukumu Israeli na akatoka kwenda vitani. Bwana akampa kuishinda Kush-rishataimu mfalme wa Aramu. Mkono wa Othnieli alishinda Kushan Rishathaimu.
HERRENS Aand kom over ham, og han blev Dommer i Israel; han drog ud til Kamp, og HERREN gav Kong Kusjan-Risj'atajim af Aram i hans Haand, saa han fik Overtaget over ham.
11 Nchi ilikuwa na amani kwa miaka arobaini. Ndipo Otinieli mwana wa Kenazi akafa.
Og Landet havde Ro i fyrretyve Aar, og Kenizziten Otniel døde.
12 Baada ya hayo, Waisraeli wakafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana; Bwana akampa Egloni mfalme wa Moabu nguvu, kuwashinda Waisraeli.
Men Israeliterne blev ved at gøre, hvad der var ondt i HERRENS Øjne. Da gav HERREN Kong Eglon af Moab Magt over Israel, fordi de gjorde, hvad der var ondt i HERRENS Øjne.
13 Eglon alijiunga na wana wa Amoni na Waamaleki wakaenda na kuwashinda Israeli, na walichukua mji wa Mitende.
Han fik Ammoniterne og Amalekiterne med sig, drog ud og slog Israel og tog Palmestaden.
14 Watu wa Israeli walimtumikia Eglon mfalme wa Moabu kwa miaka kumi na nane.
Og Israeliterne stod under Kong Eglon af Moab i atten Aar.
15 Wana wa Israeli walipomwomba Bwana, Bwana akamwinua mtu aliyewasaidia, Ehudi mwana wa Gera, Mbenjamini, mtu shoto. Wana wa Israeli wakamtuma kwa Egloni, mfalme wa Moabu, kwa malipo yao ya kodi.
Men da Israeliterne raabte til HERREN, lod HERREN en Befrier fremstaa iblandt dem, Benjaminiten Ehud, Geras Søn, som var kejthaandet. Da Israeliterne engang sendte Ehud til Kong Eglon af Moab med Skat,
16 Ehudi akajifanyia upanga uliokuwa na makali kuwili, urefu wa dhiraa moja; aliufunga chini ya nguo zake juu ya mguu wake wa kulia.
lavede han sig et tveægget Sværd, en Gomed langt, og bandt det til sin højre Hofte under Kappen.
17 Akampa Egloni Mfalme wa Moabu malipo ya kodi. (Egloni alikuwa mtu mnene sana.)
Derpaa afleverede han Skatten til Kong Eglon af Moab — Eglon var en meget fed Mand —
18 Baada ya Ehudi kulipa malipo ya kodi, aliondoka na wale waliokuwa wameibeba.
og da han var færdig dermed, ledsagede han Folkene, der havde baaret Skatten, paa Vej,
19 Hata hivyo Ehudi mwenyewe, alipofikia mahali ambapo sanamu za kuchonga zilitengenezwa karibu na Gilgali, akageuka na kurudi, akasema, 'Nina ujumbe wa siri kwako, mfalme wangu.' Eglon akasema, 'Nyamazeni kimya!' Kwa hiyo wote waliomtumikia wakatoka kwenye chumba.
men selv vendte han om ved Pesilim ved Gilgal og sagde: »Konge, jeg har noget at tale med dig om i Hemmelighed!« Men han bød ham tie, til alle de, der stod om ham, var gaaet ud.
20 Ehudi akaja kwake. Mfalme alikuwa amekaa peke yake, peke yake katika chumba cha juu cha baridi. Ehudi akasema, 'Nina ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili yeko.' Mfalme akasimama kutoka katika kiti chake.
Da Ehud kom ind til ham, sad han i sin svale Stue paa Taget, hvor han var alene; og Ehud sagde: »Jeg har et Gudsord til dig!« Da rejste han sig fra sit Sæde,
21 Ehudi akanyoosha mkono wake wa kushoto na akachukua upanga kutoka mguu wake wa kulia, na akautia ndani ya mwili wa mfalme.
men idet han stod op, rakte Ehud sin venstre Haand ud og greb Sværdet ved sin højre Side og stak det i Underlivet paa ham,
22 Na kipini cha upanga kikaingia ndani yake baada ya upanga, nao ukatokea nyuma yake, na mafuta yakashikamana juu ya upanga, kwa kuwa Ehudi hakuutoa upanga nje ya mwili wake.
saa endog Grebet gik i med Klingen; og Fedtet sluttede om Klingen, thi han drog ikke Sværdet ud af Livet paa ham; og Skarnet gik fra ham.
23 Kisha Ehudi akatoka kwenye ukumbi na akafunga milango ya chumba cha juu nyuma yake na akawafungia.
Saa gik Ehud bort gennem Søjlegangen, lukkede Døren til Stuen for ham og laasede den.
24 Baada ya Ehudi kuondoka, watumishi wa mfalme wakaja; wakaona milango ya chumba cha juu imefungwa, kwa hiyo wakafikiri, 'Hakika atakuwa anajitoa mwenyewe katika hali ya baridi ya chumba cha juu.'
Efter at han var gaaet bort, kom Kongens Folk, og da de fandt Døren til Stuen laaset, tænkte de, at han tildækkede sine Fødder i det svale Hammer;
25 Walizidi kuwa na wasiwasi hata walipoanza kuhisi kuwa walikuwa wakipuuza wajibu wao wakati mfalme bado hakufungua milango ya chumba cha juu. Kwa hiyo walichukua ufunguo wakawafungua, tazama bwana wao, ameanguka chini, amekufa.
men da de havde biet, indtil de skammede sig, uden at han aabnede Døren til Stuen, hentede de Nøglen og lukkede op; og se, der laa deres Herre død paa Gulvet.
26 Wakati watumishi wakisubiri, wakijiuliza nini wanapaswa kufanya, Ehudi alikimbia na kupita mahali ambako kulikuwa na sanamu za kuchonga, na hivyo akakimbia kwenda Seira.
Men Ehud slap bort, medens de blev opholdt, og han satte over ved Pesilim og undslap til Se'ira.
27 Alipofika, alipiga tarumbeta katika nchi ya mlima wa Efraimu. Kisha wana wa Israeli wakashuka pamoja naye kutoka milimani, naye akawaongoza.
Saa snart han derpaa naaede Efraims Bjerge, lod han støde i Hornet; og Israeliterne fulgte ham ned fra Bjergene, idet han gik i Spidsen for dem.
28 Akawaambia, Nifuate, kwa kuwa Bwana atawashinda adui zenu, Wamoabu. Wakamfuata, wakakamata vivuko vya Bonde la Yordani, toka kwa Wamoabi, wala hawakuruhusu mtu yeyote kuvuka mto.
Og han sagde til dem: »Følg mig ned, thi HERREN har givet eders Fjender Moabiterne i eders Haand!« Og de fulgte ham ned og fratog Moabiterne Vadestederne over Jordan og lod ikke en eneste komme over.
29 Wakati huo waliwaua watu elfu kumi wa Moabu, na wote walikuwa watu wenye nguvu na wenye uwezo. Hakuna aliyekimbia.
Ved den Lejlighed nedhuggede de omtrent 10 000 Moabiter, lutter stærke og dygtige Mænd, ikke een undslap.
30 Kwa hiyo siku hiyo Moabu ilishindwa na nguvu ya Israeli. Na nchi ilikuwa na amani kwa miaka thelathini.
Saaledes blev Moab den Gang underkuet af Israel; og Landet havde Ro i firsindstyve Aar.
31 Baada ya Ehudi, mwamuzi aliyefuata alikuwa Shamgari mwana wa Anathi ambaye aliwaua Wafilisti 600 kwa konzo la ng'ombe. Pia aliwaokoa Israeli kutoka kwenye hatari.
Efter ham kom Sjamgar, Anats Søn. Han nedhuggede Filisterne, 600 Mand, med en Oksedriverstav; ogsaa han frelste Israel.

< Waamuzi 3 >