< Waamuzi 21 >

1 Sasa watu wa Israeli walikuwa wameahidi huko Mispa, “Hakuna hata mmoja wetu atakayempa binti yake kuolewa na Mbenyamini.”
Ora tinham jurado os homens de Israel em Mispah, dizendo: Nenhum de nós dará sua filha por mulher aos benjamitas.
2 Ndipo watu wakaenda Betheli, wakakaa huko mbele ya Mungu hata jioni; wakalia kwa sauti kubwa.
Veio pois o povo a bethel, e ali ficaram até à tarde diante de Deus: e levantaram a sua voz, e prantearam com grande pranto,
3 Walipiga kelele, “Kwa nini, Bwana, Mungu wa Israeli, amefanya jambo hili kwa Waisraeli, kwamba moja ya makabila yetu linapotea leo?”
E disseram: Ah! Senhor Deus de Israel, porque sucedeu isto em Israel, que hoje falte uma tribo em Israel?
4 Siku iliyofuata watu waliamka mapema na wakajenga madhabahu huko na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani.
E sucedeu que, no dia seguinte, o povo pela manhã se levantou, e edificou ali um altar; e ofereceram holocaustos e ofertas pacíficas.
5 Watu wa Israeli wakasema, “Ni nani kati ya kabila zote za Israeli hawakuja katika mkutano wa Bwana?” Kwa kuwa walikuwa wamefanya ahadi muhimu juu ya mtu yeyote ambaye hakuja kwa Bwana huko Mispa. Wakasema, “Hakika yeye atauawa.”
E disseram os filhos de Israel: Quem de todas as tribos de Israel não subiu ao ajuntamento ao Senhor? Porque se tinha feito um grande juramento acerca dos que não viessem ao Senhor a Mispah, dizendo: Morrerá certamente.
6 Watu wa Israeli walikuwa na huruma kwa ndugu yao Benyamini. Wakasema, “Leo hii kabila moja limekatiliwa mbali kutoka Israeli.
E arrependeram-se os filhos de Israel acerca de Benjamin, seu irmão, e disseram: Cortada é hoje de Israel uma tribo.
7 Ni nani atakayewapa wale walioachwa wake, kwa kuwa tumeahidi kwa Bwana kwamba hatuwezi kuwaruhusu yeyote kati yao aoe binti zetu?”
Que faremos, acerca de mulheres, com os que ficaram de resto, pois nós temos jurado pelo Senhor que nenhuma de nossas filhas lhes dariamos por mulheres?
8 Wakasema, “Ni nani kati ya kabila za Israeli hawakuja kwa Bwana huko Mispa? Ilionekana kuwa hakuna mtu aliyekuja kwenye mkusanyiko kutoka Jabeshi-Gileadi.
E disseram: há alguma das tribos de Israel que não subisse ao Senhor a Mispah? E eis que ninguém de Jabes de Gilead viera ao arraial, à congregação.
9 Kwa maana watu walipokuwa wamepangwa kwa utaratibu, tazama, hakuna hata mmoja wa wenyeji wa Yabeshi Gileadi.
Porquanto o povo se contou: e eis que nenhum dos moradores de Jabes de Gilead se achou ali.
10 Mkutano huo uliwatuma watu kumi na wawili wa watu wao wenye ujasiri kwa maagizo ya kwenda Jabeshi-gileadi na kuwaangamiza, na kuwaua, hata wanawake na watoto.
Então o ajuntamento enviou lá doze mil homens dos mais valentes, e lhes ordenou, dizendo: Ide, e ao fio da espada feri aos moradores de Jabes de Gilead, e às mulheres e aos meninos.
11 “Fanya hivi unapaswa kuua kila mume na kila mwanamke aliyelala na mwanaume.”
Porém isto é o que haveis de fazer: A todo o macho e a toda a mulher que se houver deitado com um homem totalmente destruireis.
12 Watu wale walikuta watu kati ya hao waliokaa Yabeshi-gileadi, wanawake mia nne ambao hawakulala na mwanaume, wakawapeleka kwenye kambi huko Shilo, huko Kanaani.
E acharam entre os moradores de Jabes de Gilead quatrocentas moças virgens, que não conheceram homem deitando-se com macho: e as trouxeram ao arraial, a Silo, que está na terra de Canaan.
13 Mkutano wote ukatuma ujumbe na kuwaambia watu wa Benyamini waliokuwa kwenye mwamba wa Rimoni kwamba walikuwa wanawapa amani.
Então todo o ajuntamento enviou, e falou aos filhos de Benjamin, que estavam na penha de Rimmon, e lhes proclamou a paz.
14 Wabenyamini walirudi wakati huo na walipewa wanawake wa Yabeshi Gileadi, lakini hapakuwa na wanawake wa kutosha kwa wote.
E ao mesmo tempo voltaram os benjamitas; e deram-lhes as mulheres que haviam guardado com vida, das mulheres de Jabes de Gilead: porém estas ainda lhes não bastaram.
15 Watu waliomboleza kwa kile kilichotokea Benyamini, kwa kuwa Bwana alifanya mgawanyiko kati ya makabila ya Israeli.
Então o povo se arrependeu por causa de Benjamin: porquanto o Senhor tinha feito abertura nas tribos de Israel.
16 Kisha wakuu wa mkutano wakasema, “Tutafanyaje ili Wabenyamini wapate wake, kwa kuwa wanawake wa Benyamini wameuawa?”
E disseram os anciãos do ajuntamento: Que faremos acerca de mulheres para os que ficaram de resto? pois as mulheres são destruídas de Benjamin.
17 Wakasema, 'Lazima kuwe na urithi kwa Wabenyamini waliosalia, ili kabila lisiharibiwe kutoka Israeli.
Disseram mais: A herança dos que ficaram de resto é de Benjamin, e nenhuma tribo de Israel deve ser destruída.
18 Hatuwezi kuwapa wake kutoka kwa binti zetu, kwa kuwa wana wa Israeli walikuwa wametoa ahadi, 'Na alaaniwe mtu atakayempa Benyamini mke.'”
Porém nós não lhes poderemos dar mulheres de nossas filhas, porque os filhos de Israel juraram, dizendo: Maldito aquele que der mulher aos benjamitas.
19 Wakasema, “Mnajua kuwa kuna sikukuu kwa Bwana kila mwaka huko Shilo ( ambayo ni kaskazini ya Betheli, mashariki ya barabara inayopanda kutoka Betheli hadi Shekemu, na kusini mwa Lebona).
Então disseram: Eis que de ano em ano há solenidade do Senhor em Silo, que se celebra para o norte de bethel, da banda do nascente do sol, pelo caminho alto que sobe de bethel a Sichem, e para o sul de Lebona.
20 Wakawaagiza wana wa Benyamini, wakisema, “Nendeni, mjifiche kwa siri, na kusubiri katika mashamba ya mizabibu.
E mandaram aos filhos de Benjamin, dizendo: Ide, e emboscai-vos nas vinhas,
21 Tazama wakati ambapo wasichana kutoka Shilo watatoka kucheza, Tokeni nje ya mizabibu na kila mmoja wenu anapaswa kunyakua mke kutoka kwa wasichana wa Shilo, kisha kurudi kwenye nchi ya Benyamini.
E olhai, e eis ai, saindo as filhas de Silo a dançar em ranchos, saí vós das vinhas, e arrebatai-vos cada um sua mulher das filhas de Silo, e ide-vos à terra de Benjamin.
22 Wakati baba zao au ndugu zao watakapokuja kutupinga, tutawaambia, 'Tupeni neema! Waache wabaki kwa sababu hatukupata wake kwa kila mtu wakati wa vita. Na ninyi hamna hatia juu ya ahadi, kwa sababu hamkuwapa wao binti zenu.'”
E será que, quando seus pais ou seus irmãos vierem a litigar conosco, nós lhes diremos: Por amor de nós, tende compaixão deles, pois nesta guerra não tomamos mulheres para cada um deles: porque não lhas destes vós, para que agora ficasseis culpados?
23 Watu wa Benyamini walifanya hivyo. Walichukua idadi ya wake waliowahitaji kutoka kwa wasichana waliokuwa wakicheza, nao wakawachukua ili wawe wake zao. Wakaenda na kurudi mahali pa urithi wao; wakajenga tena miji, na wakaishi ndani yao.
E os filhos de Benjamin o fizeram assim, e levaram mulheres conforme ao número deles, das que arrebatavam dos ranchos que dançavam: e foram-se, e voltaram à sua herança, e reedificaram as cidades, e habitaram nelas.
24 Kisha watu wa Israeli wakatoka mahali hapo na kwenda nyumbani, kila mmoja kwa kabila lake na ukoo, na kila mmoja kwa urithi wake mwenyewe.
Também os filhos de Israel partiram então dali, cada um para a sua tribo e para a sua geração: e sairam dali, cada um para a sua herança.
25 Siku hizo hapakuwa na mfalme huko Israeli. Kila mtu alifanya yaliyo sawa machoni pake mwenyewe.
Naqueles dias não havia rei em Israel: porém cada um fazia o que parecia reto aos seus olhos.

< Waamuzi 21 >