< Waamuzi 2 >

1 Malaika wa Bwana akatoka Gilgali, akaenda Bokimu, akasema, “Nimekuleta kutoka Misri, na nimekuleta katika nchi niliyoapa kuwapa baba zako.
And the messenger of Yahweh came up from Gilgal, unto Bochim. And he said—I led you up out of Egypt, and brought you into the land, which I had sworn unto your fathers, And I said, I will not break my covenant with you, to times age-abiding;
2 Nikasema, 'Sitakuvunja kamwe agano langu na wewe. Usifanye agano na wale wanaoishi katika nchi hii. Ziangushe madhabahu zao. Lakini hukusikiliza sauti yangu. Je! ni nini hiki ulichokifanya?
But, ye, must not solemnise a covenant with the inhabitants of this land, Their altars, must ye tear down, —But ye have not hearkened unto my voice, what is this ye have done?
3 Basi sasa nasema, “Sitawafukuza Wakanaani mbele yenu, nao watakuwa miiba kwenu, na miungu yao itakuwa mtego kwa ajili yenu.”
Wherefore also I said, I will not drive them out from before you, —but they shall be your adversaries, and, their gods, shall become unto you a snare.
4 Malaika wa Bwana alipowaambia maneno hayo kwa watu wote wa Israeli, watu wakapiga kelele na kulia.
And it came to pass, when the messenger of Yahweh had spoken these words unto all the sons of Israel, that the people lifted up their voice, and wept.
5 Waliita mahali hapo Bokimu. Hapo wakatoa dhabihu kwa Bwana.
So they called the name of that place, Bochim, and offered sacrifice there, unto Yahweh.
6 Yoshua alipowaruhusu watu waende zao, wana wa Israeli kila mmoja akaenda mahali alipopewa, wakiwa na umiliki wa ardhi yao.
Now, when Joshua had let the people go, the sons of Israel went their way, every man to his inheritance, to take possession of the land.
7 Watu walimtumikia Bwana wakati wa maisha ya Yoshua na wazee walioendelea baada yake, ni wale waliokuwa wameona matendo yote makuu ya Bwana aliyoyafanya kwa Israeli.
And the people served Yahweh all the days of Joshua, —and all the days of the elders who outlived Joshua, who had seen all the great work of Yahweh which he had wrought for Israel.
8 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, alikufa akiwa na umri wa miaka 110.
So then Joshua, the son of Nun, the servant of Yahweh, died, —being a hundred and ten years old.
9 Wakamzika ndani ya mpaka wa nchi aliyopewa huko Timnath Heresi, katika mlima wa Efraimu, kaskazini mwa Mlima Gaash.
And they buried him within the bounds of his inheritance, in Timnath-heres, in the hill country of Ephraim, —on the north of Mount Gaash.
10 Kizazi hicho chote kilikusanyika kwa baba zao. Kizazi kingine kilichofuata baada yao ambao hakikumjua Bwana au kile alichokifanya kwa Israeli.
All that generation also, were gathered unto their fathers, —and there arose another generation, after them, who had not known Yahweh, nor even the work which he had wrought for Israel.
11 Watu wa Israeli walifanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, nao wakawatumikia Mabaali.
So the sons of Israel did the thing that was wicked in the sight of Yahweh, —and served the Baals;
12 Wakaondoka kwa Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewatoa kutoka Misri. Wakaifuata miungu mingine, miungu ya watu waliokuwa karibu nao, nao wakaisujudia. Wakamkasirisha BWANA kwa sababu
and forsook Yahweh, the God of their fathers, who brought them up out of the land of Egypt, and went after other gods, from among the gods of the peoples who were round about them, and bowed themselves down unto them, —and angered Yahweh.
13 waliondoka kwa Bwana na kumwabudu Baal na Maashtoreti.
Yea, they forsook Yahweh, —and did service unto the Baal and unto Ashtaroth.
14 Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawapa washambuliaji walioiba mali zao kutoka kwao. Aliwauza kama watumwa waliofanyika kwa nguvu za maadui zao waliowazunguka, hivyo hawakuweza kujikinga dhidi ya adui zao.
Then kindled the anger of Yahweh upon Israel, and he delivered them into the hand of spoilers, who plundered them, —and he sold them into the hand of their enemies round about, so that they could no longer stand before their enemies.
15 Israeli walipokwenda kupigana, mkono wa Bwana ulikuwa dhidi yao kuwashinda, kama alivyowaapia. Na walikuwa katika shida kali.
Whithersoever they went out, the hand of Yahweh was found to be against them for misfortune, as spake Yahweh, and as sware Yahweh unto them, —and they were distressed exceedingly.
16 Ndipo Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa katika mikono ya wale waliokuwa wakiba mali zao.
And, though Yahweh raised up judges, —who saved them out of the hand of them that plundered them,
17 Hata hivyo hawakuwasikiliza waamuzi wao. Hawakuwa waaminifu kwa Bwana na wakajitoa wenyewe kama makahaba kwa miungu mingine na kuabudu. Waligeuka upesi na kuiacha njia waliyoishi baba zao-wale waliotii amri za Bwana-lakini wao wenyewe hawakufanya hivyo.
yet, even unto their judges, did thy not hearken, for they went unchastely astray after other gods, and bowed themselves down to them, —they turned aside speedily out of the way wherein their fathers who hearkened unto the commandments of Yahweh, walked, they did not so.
18 Bwana aliinua waamuzi kwa ajili yao, Bwana akawasaidia waamuzi na kuwakomboa kutoka kwa mikono ya adui zao siku zote muamuzi aliishi. Bwana aliwahurumia walipougua kwa sababu ya wale waliowadhulumu na kuwasumbua.
And, when Yahweh raised them up judges, then was Yahweh with the judges, and saved them out of the hand of their enemies, all the days of the judge, —for Yahweh was grieved at their outcry, because of them who oppressed them, and ill-treated them.
19 Lakini mwamuzi alipokufa, waligeuka na kufanya mambo ambayo yalikuwa mabaya zaidi kuliko baba zao walivyofanya. Wakaenda kuifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao yote mabaya au njia zao za ukaidi.
But, when the judge was dead, they again broke faith more than their fathers, by going their way after other gods, by serving them, and bowing themselves down to them, —they ceased not from their doings nor from their stubborn way.
20 Hasira ya Bwana iliwaka juu ya Israeli; akasema, Kwa sababu taifa hili limevunja masharti ya agano langu ambalo nililiweka kwa ajili ya baba zao-kwa sababu hawakuisikiliza sauti yangu.
So then the anger of Yahweh kindled upon Israel, and he said—Forasmuch as this nation have transgressed my covenant, which I commanded their fathers, and have not hearkened unto my voice,
21 Tangu sasa sitaliondoa mbele yao taifa lolote aliloliacha Yoshua baada ya kufa.
I also, will no further dispossess a man from before them, —from among the nations which Joshua left remaining, when he died;
22 Nitafanya hivi ili kuwajaribu Israeli, ikiwa watafuata njia ya Bwana au sivyo, kama vile baba zao walivyoifuata.
that I may, by them, put Israel to the proof, —whether they are going to be observant of the way of Yahweh, to walk therein as their fathers observed it, or not.
23 Ndiyo sababu Bwana aliwaacha mataifa hayo, wala hakuwafukuza haraka na kuwatia mikononi mwa Yoshua.
Thus then Yahweh left these nations, not dispossessing them speedily, —neither had he delivered them into the hand of Joshua

< Waamuzi 2 >