< Waamuzi 13 >

1 Watu wa Israeli wakafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, naye akawatia mikononi mwa Wafilisti kwa miaka arobaini.
And the sons of Israel add to do the evil thing in the eyes of Jehovah, and Jehovah giveth them into the hand of the Philistines forty years.
2 Kulikuwa na mtu kutoka Sora, wa jamaa ya Wadani, jina lake Manoa. Mke wake hakuweza kupata mimba na hivyo hakuzaa.
And there is a certain man of Zorah, of the family of the Danite, and his name [is] Manoah, his wife [is] barren, and hath not borne;
3 Malaika wa Bwana akamtokea yule mwanamke akamwambia, Tazame sasa, umeshindwa kupata mimba, wala hujazaa, lakini utakuwa na mimba na utazaa mtoto.
and a messenger of Jehovah appeareth unto the woman, and saith unto her, 'Lo, I pray thee, thou [art] barren, and hast not borne; when thou hast conceived, then thou hast borne a son.
4 Sasa kuwa makini usinywe divai au kileo, wala usile kitu chochote kilicho najisi.
And, now, take heed, I pray thee, and do not drink wine, and strong drink, and do not eat any unclean thing,
5 Angalia, utakuwa na mjamzito na kuzaliwa mtoto mwanaume. Hakuna wembe itakayotumiwa juu ya kichwa chake, kwa kuwa mtoto atakuwa Mnaziri kwa Mungu kutoka tumboni, naye ataanza kuwaokoa Israeli kutoka mkono wa Wafilisti.
for, lo, thou art conceiving and bearing a son, and a razor doth not go up on his head, for a Nazarite to God is the youth from the womb, and he doth begin to save Israel out of the hand of the Philistines.'
6 Kisha mwanamke akaenda kumwambia mumewe, “Mtu wa Mungu alikuja kwangu, na kuonekana kwake kulikuwa kama malaika wa Mungu, wa kutisha sana. Sikumwuliza ametokea wapi, na hakuniambia jina lake.
And the woman cometh and speaketh to her husband, saying, 'A man of God hath come unto me, and his appearance [is] as the appearance of a messenger of God, very fearful, and I have not asked him whence he [is], and his name he hath not declared to me;
7 Akaniambia, 'Tazama! Utakuwa mjamzito, na utazaa mtoto. Basi usinywe divai au kileo, wala usile chakula chochote ambacho sheria inasema kuwa si safi, kwa kuwa mtoto huyo atakuwa Mnaziri kwa Mungu tangu akipokuwa tumboni mwako mpaka siku ya kufa kwake.”
and he saith to me, Lo, thou art pregnant, and bearing a son, and now do not drink wine and strong drink, and do not eat any unclean thing, for a Nazarite to God is the youth from the womb till the day of his death.'
8 Ndipo Manoa akamwomba Bwana, akasema, Ee Bwana, tafadhali mruhusu mtu wa Mungu uliyemtuma arudi kwetu ili atufundishe kile tutakachotendea kwa mtoto atakayezaliwa hivi karibuni.
And Manoah maketh entreaty unto Jehovah, and saith, 'O, my Lord, the man of God whom Thou didst send, let him come in, I pray thee, again unto us, and direct us what we do to the youth who is born.'
9 Mungu akajibu sala ya Manoa, na malaika wa Mungu akamwendea mwanamke tena akiwa ameketi shambani. Lakini Manoa mumewe hakuwa pamoja naye.
And God hearkeneth to the voice of Manoah, and the messenger of God cometh again unto the woman, and she [is] sitting in a field, and Manoah her husband is not with her,
10 Basi mwanamke akakimbia haraka akamwambia mumewe, “Tazama! Yule mtu ameonekana kwangu-aliyekuja kwangu siku ile!”
and the woman hasteth, and runneth, and declareth to her husband, and saith unto him, 'Lo, he hath appeared unto me — the man who came on [that] day unto me.'
11 Manoa akasimama na kumfuata mkewe. Alipofika kwa mtu huyo, akasema, “Je, wewe ndiwe mtu aliyezungumza na mke wangu?'” Mtu huyo akasema, “Ni mimi.”
And Manoah riseth, and goeth after his wife, and cometh unto the man, and saith to him, 'Art thou the man who spake unto the woman?' and he saith, 'I [am].'
12 Manoa akasema, Sasa maneno yako yatimike. Je! kuna maagizo gani kwa ajili ya mtoto, na kazi yake itakuwa nini? '
And Manoah saith, 'Now let thy words come to pass; what is the custom of the youth — and his work?'
13 Malaika wa Bwana akamwambia Manoa, 'Lazima mkeo afanye kila kitu nilichomwambia.
And the messenger of Jehovah saith unto Manoah, 'Of all that I said unto the woman let her take heed;
14 Asile kitu chochote kinachotokana na mizabibu, wala usimruhusu kunywa divai au kileo; usimruhusu ale chakula chochote ambacho sheria inasema kuwa si safi. Anapaswa kutii kila kitu nilichoamuru afanye.
of anything which cometh out from the wine-vine she doth not eat, and wine and strong drink she doth not drink, and any unclean thing she doth not eat; all that I have commanded her she doth observe.'
15 Manoa akamwambia malaika wa Bwana, Tafadhali keti kwa muda, utupe wakati wa kuandaa mbuzi kwa ajili yako.
And Manoah saith unto the messenger of Jehovah, 'Let us detain thee, we pray thee, and prepare before thee a kid of the goats.'
16 Malaika wa Bwana akamwambia Manowa, Hata kama nitakaa, sitakula chakula chako. Lakini ukitayarisha sadaka ya kuteketezwa, toa kwa Bwana. ' (Manowa hakujua kwamba alikuwa malaika wa Bwana.)
And the messenger of Jehovah saith unto Manoah, 'If thou detain me — I do not eat of thy bread; and if thou prepare a burnt-offering — to Jehovah thou dost offer it;' for Manoah hath not known that He [is] a messenger of Jehovah.
17 Manoa akamwambia malaika wa Bwana, Jina lako ni nani, ili tukuheshimu wakati maneno yako yatakapotimia?
And Manoah saith unto the messenger of Jehovah, 'What [is] thy name? when thy words come to pass, then we have honoured thee.'
18 Malaika wa Bwana akamwambia, Mbona unauliza jina langu? Ni ajabu! '
And the messenger of Jehovah saith to him, 'Why [is] this — thou dost ask for My name? — and it [is] Wonderful.'
19 Manoa akamchukua huyo mbuzi pamoja na sadaka ya nafaka, akatoa sadaka juu ya mwamba kwa Bwana. Alifanya jambo la ajabu wakati Manoah na mke wake walikuwa wakiangalia.
And Manoah taketh the kid of the goats, and the present, and offereth on the rock to Jehovah, and He is doing wonderfully, and Manoah and his wife are looking on,
20 Wakati huo moto ukatoka juu ya madhabahu kwenda mbinguni, malaika wa Bwana akapanda katika moto wa madhabahu. Manoah na mkewe waliona jambo hilo wakainamisha vichwa vyao chini.
and it cometh to pass, in the going up of the flame from off the altar toward the heavens, that the messenger of Jehovah goeth up in the flame of the altar, and Manoah and his wife are looking on, and they fall on their faces to the earth,
21 malaika wa Bwana hakuonekana tena kwa Manoa au mkewe. Manoa akajua kwamba yule ndiye malaika wa Bwana.
and the messenger of Jehovah hath not added again to appear unto Manoah, and unto his wife, then hath Manoah known that He [is] a messenger of Jehovah.
22 Manoa akamwambia mkewe, 'Hakika tutakufa, kwa sababu tumemwona Mungu!'
And Manoah saith unto his wife, 'We certainly die, for we have seen God.'
23 Lakini mkewe akamwambia, Ikiwa Bwana alitaka kutuua, asingepokea sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka tuliyompa. Asingetuonesha mambo haya yote, wala wakati huu asingeweza kuturuhusu tusikie mambo hayo.
And his wife saith to him, 'If Jehovah were desirous to put us to death, He had not received from our hands burnt-offering and present, nor shewed us all these things, nor as [at this] time caused us to hear [anything] like this.'
24 Baadaye mwanamke akamzaa mtoto, akamwita jina lake Samsoni. Mtoto alikua na Bwana akambariki.
And the woman beareth a son, and calleth his name Samson, and the youth groweth, and Jehovah doth bless him,
25 Roho wa Bwana akaanza kumchochea Mahane Dani, kati ya Sora na Eshtaoli.
and the Spirit of Jehovah beginneth to move him in the camp of Dan, between Zorah and Eshtaol.

< Waamuzi 13 >