< Yoshua 7 >

1 Lakini watu wa Israeli hawakutenda katika uaminifu kuhusiana na vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu. Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka katika kabila la Yuda, alivitwaa baadhi ya vitu hivyo vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya uharibifu, na hasira ya Yahweh iliwaka juu yawatu wa Israeli.
و بنی‌اسرائیل در آنچه حرام شده بود خیانت ورزیدند، زیرا عخان ابن کرمی ابن زبدی ابن زارح از سبط یهودا، از آنچه حرام شده بود گرفت، و غضب خداوند بر بنی‌اسرائیل افروخته شد.۱
2 Yoshua alituma watu kutoka Yeriko kwenda Ai, mji uliokuwa karibu na Bethi Aveni, mashariki mwa Betheli. Aliwaambia, “Nendeni na mkaipeleleza nchi.” Wale watu walikwea na kuipeleleza Ai.
و یوشع از اریحا تا عای که نزد بیت آون به طرف شرقی بیت ئیل واقع است، مردان فرستاد وایشان را خطاب کرده، گفت: «بروید و زمین راجاسوسی کنید.» پس آن مردان رفته، عای راجاسوسی کردند.۲
3 Waliporudi kwa Yoshua, walimwambia, “Usitume watu wote kwenda Ai. Tuma tu watu elfu mbili au elfu tatu waende kuiteka Ai. Usiwafanye watu wateseke katika vita, kwani ni watu wachache.”
و نزد یوشع برگشته، او راگفتند: «تمامی قوم برنیایند؛ به قدر دو یا سه هزارنفر برآیند و عای را بزنند و تمامی قوم را به آنجازحمت ندهی زیرا که ایشان کم‌اند.»۳
4 Hivyo ni watu wapatao elfu tatu tu kutoka katika jeshi ndio walioenda, lakini watu hawa waliwakimbia watu wa Ai.
پس قریب به سه هزار نفر از قوم به آنجا رفتند و از حضورمردان عای فرار کردند.۴
5 Watu wa Ai waliwaua watu wapatao thelathini na sita, waliwafuata katika lango la mji hadi katika machimbo ya mawe, na waliwauwa walipokuwa wakishuka katika kilima. Na mioyo ya watu ilijawa hofu na ujasiri wao ukawatoka.
و مردان عای از آنها به قدر سی و شش نفر کشتند و از پیش دروازه تاشباریم ایشان را تعاقب نموده، ایشان را در نشیب زدند، و دل قوم گداخته شده، مثل آب گردید.۵
6 Basi Yoshua alizirarua nguo zake. Yeye pamoja na wazewe wa Israeli waliweka mavumbi juu ya vichwa vyao na wakainamisha vichwa vyao hadi katika nchi mbele ya sanduku la Yahweh, na walibaki pale mpaka jioni.
و یوشع و مشایخ اسرائیل جامه خود راچاک زده، پیش تابوت خداوند تا شام رو به زمین افتادند، و خاک به‌سرهای خود پاشیدند.۶
7 Kisha Yoshua akasema, “Oo, Yahweh Bwana, kwanini umewavusha watu hawa ng'ambo ya Yordani? Kutuweka katika mikono ya Waamori ili kutuangamiza? ikiwa kama tulifanya maamuzi tofauti na tungekaa katika upande mwingine wa Yordani!
و یوشع گفت: «آه‌ای خداوند یهوه برای چه این قوم را از اردن عبور دادی تا ما را به‌دست اموریان تسلیم کرده، ما را هلاک کنی، کاش راضی شده بودیم که به آن طرف اردن بمانیم.۷
8 Bwana, niseme nini, baada ya Israeli kuwatega migongo maadui zao?
آه‌ای خداوندچه بگویم بعد از آنکه اسرائیل از حضور دشمنان خود پشت داده‌اند.۸
9 Kwa kuwa Wakaanani na wenyeji wote wa nchi watakaposikia, watatuzunguka na kuwafanya watu wa nchi kulisahau jina letu. Na utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?
زیرا چون کنعانیان و تمامی ساکنان زمین این را بشنوند دور ما را خواهندگرفت و نام ما را از این زمین منقطع خواهند کرد، و تو به اسم بزرگ خود چه خواهی کرد؟»۹
10 Yahweh akamwambia Yoshua, “Inuka! kwanini umelala kifudifudi?
خداوند به یوشع گفت: «برخیز چرا تو به این طور به روی خود افتاده‌ای.۱۰
11 Israeli imetenda dhambi. Wamevunja agano langu nililowaagiza. Wameiba baadhi ya vitu vilivyokuwa vimetengwa. Wameiba na kisha pia wakaficha dhambi yao kwa kuweka vitu vile walivyochukua miongoni mwa mali zao wenyewe.
اسرائیل گناه کرده، و از عهدی نیز که به ایشان امر فرمودم تجاوز نموده‌اند و از چیز حرام هم گرفته، دزدیده‌اند، بلکه انکار کرده، آن را در اسباب خودگذاشته‌اند.۱۱
12 Na matokeo yake ni kwamba watu wa Israeli hawataweza kusimama mbele za maadui zao. Walitega migongo yao kwa maadui zao kwasababu wao wenyewe wametengwa kwa ajili ya uharibifu. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka pale mtakapoteketeza vitu vile vilivyotakiwa kuharibiwa, lakini sasa bado viko miongoni mwenu.
از این سبب بنی‌اسرائیل نمی توانندبه حضور دشمنان خود بایستند و از حضوردشمنان خود پشت داده‌اند، زیرا که ملعون شده‌اند، و اگر چیز حرام را از میان خود تباه نسازید، من دیگر با شما نخواهم بود.۱۲
13 Inuka! Waweke watu wakfu kwangu, na uwaambie, 'Jiwekeeni wakfu ninyi wenyewe kesho. Kwa kuwa, Yahweh, Mungu wa Israeli asema hivi, “Kuna vitu vilitengwa ili kuteketezwa ambavyo bado viko miongoni mwenu, Israeli. Hamtaweza kusimama mbele ya maadui zenu mpaka pale mtakapoviondoa miongoni mwenu vitu vyote ambavyo vilitengwa kwa ajili ya kuteketezwa.”
برخیزقوم را تقدیس نما و بگو برای فردا خویشتن راتقدیس نمایید، زیرا یهوه خدای اسرائیل چنین می‌گوید: ای اسرائیل چیزی حرام در میان توست و تا این چیز حرام را از میان خود دور نکنی، پیش روی دشمنان خود نمی توانی‌ایستاد.۱۳
14 Asubuhi, mtajisogeza wenyewe kwa makabila. Kabila lile ambalo Yahweh atalichagua litasogea karibu kwa koo zake. Ukoo ule ambao Yahweh atauchagua lazima usogee karibu kwa nyumba. Nyumba ambayo Yahweh ataichagua lazima isogee karibu kwa mtu mmoja mmoja.
پس بامدادان، شما موافق اسباط خود نزدیک بیایید، وچنین شود که سبطی را که خداوند انتخاب کند به قبیله های خود نزدیک آیند، و قبیله‌ای را که خداوند انتخاب کند به خاندانهای خود نزدیک بیایند، و خاندانی را که خداوند انتخاب کند به مردان خود نزدیک آیند.۱۴
15 Itakuwa hivi mtu yule atakayechaguliwa na aliye navyo vitu hivyo vilivyotengwa kwa ajili ya kuharibiwa, atachomwa moto, yeye na kila kitu alichonacho, kwasababu amelivunja agano la Yahweh na kwasababu amefanya jambo la aibu katika Israeli.'”
و هر‌که آن چیز حرام نزد او یافت شود با هر‌چه دارد به آتش سوخته شود، زیرا که از عهد خداوند تجاوز نموده، قباحتی در میان اسرائیل به عمل آورده است.»۱۵
16 Basi, Yoshua aliamka asubuhi na mapema na aliwaleta Israeli karibu, kabila kwa kabila, na kabila la Yuda lilichaguliwa.
پس یوشع بامدادان بزودی برخاسته، اسرائیل را به اسباط ایشان نزدیک آورد و سبطیهودا گرفته شد.۱۶
17 Yoshua akazisogeza koo za Yuda karibu, na ukoo wa Zera ulichaguliwa. Akausogeza karibu ukoo wa Zera mtu kwa mtu, na Zabdi alichaguliwa.
و قبیله یهودا را نزدیک آوردو قبیله زارحیان گرفته شد. پس قبیله زارحیان رابه مردان ایشان نزدیک آورد و زبدی گرفته شد.۱۷
18 Akaisogeza karibu nyumba ya Zabdi mtu kwa mtu, na Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka kabila la Yuda, alichaguliwa.
و خاندان او را به مردان ایشان نزدیک آورد وعخان بن کرمی ابن زبدی بن زارح از سبط یهوداگرفته شد.۱۸
19 Kisha Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, niambie ukweli mbele za Yahweh, Mungu wa Israel, na ufanye ukiri wako kwake. Tafadhali niambie kile ulichofanya. Usinifiche.”
و یوشع به عخان گفت: «ای پسر من الان یهوه خدای اسرائیل را جلال بده و نزد اواعتراف نما و مرا خبر بده که چه کردی و از مامخفی مدار.»۱۹
20 Akani akamjibu Yoshua, “Kwa kweli nimetenda dhambi mbele Yahweh, Mungu wa Israeli.
عخان در جواب یوشع گفت: «فی الواقع به یهوه خدای اسرائیل گناه کرده، وچنین و چنان به عمل آورده‌ام.۲۰
21 Nilichofanya ni hiki: Nilipoona miongoni mwa nyara mkoti mzuri kutoka Babeli, shekeli mia mbili za fedha, na kipande cha dhahabu chenye uzito wa shekeli hamsini, nilivitamani na nikavichukua. Vimefichwa chini ardhini katikati ya hema langu, na fedha iko chini yake.”
چون در میان غنیمت ردایی فاخر شنعاری و دویست مثقال نقره و یک شمش طلا که وزنش پنجاه مثقال بوددیدم، آنها را طمع‌ورزیده، گرفتم، و اینک درمیان خیمه من در زمین است و نقره زیر آن می‌باشد.»۲۱
22 Yoshua akatuma wajumbe waliokimbia mpaka kwenye hema mahali palipokuwa na vile vitu. Walipoangalia, waliviona vimefichwa katika hema lake, na fedha chini yake.
آنگاه یوشع رسولان فرستاد و به خیمه دویدند، و اینک در خیمه او پنهان بود و نقره زیرآن.۲۲
23 Walivichukua vitu hivyo kutoka katikati ya hema na kuvileta kwa Yoshua na watu wote wa Israeli. Walivimwaga mbele za Yahweh.
و آنها را از میان خیمه گرفته، نزد یوشع وجمیع بنی‌اسرائیل آوردند و آنها را به حضورخداوند نهادند.۲۳
24 Kisha Yoshua na Waisraeli wote pamoja naye, walimchukua Akani mwana wa Zera, na fedha, na koti, na kipande cha dhahabu, wana na binti zake, ng'ombe zake, punda zake, kondoo zake, hema lake, na kila kitu alichokuwa nacho, na wakavileta hata bonde la Akori.
و یوشع و تمامی بنی‌اسرائیل با وی عخان پسر زارح و نقره و ردا و شمش طلا وپسرانش و دخترانش و گاوانش و حمارانش وگوسفندانش و خیمه‌اش و تمامی مایملکش راگرفته، آنها را به وادی عخور بردند.۲۴
25 Kisha Yoshua akasema, “Kwanini umetusumbua? Leo Yahweh atakutesa na wewe.” Waisraeli wote wakampiga kwa mawe. Na wakawachoma wote kwa moto, na wakawapiga mawe.
و یوشع گفت: «برای چه ما را مضطرب ساختی؟ خداوندامروز تو را مضطرب خواهد ساخت.» پس تمامی اسرائیل او را سنگسار کردند و آنها را به آتش سوزانیدند و ایشان را به سنگها سنگسار کردند.۲۵
26 Kisha wakaweka juu yake kichuguu kikubwa cha mawe ambayo yapo hata leo. Yahweh akaachilia mbali hasira yake. Hivyo basi, jina la mahali hapo likawa Akori hata leo.
و توده بزرگ از سنگها بر او برپا داشتند که تا به امروز هست، و خداوند از شدت غضب خودبرگشت، بنابراین اسم آن مکان تا امروز وادی عخور نامیده شده است.۲۶

< Yoshua 7 >