< Yoshua 4 >

1 Watu wote walipokwisha kuvuka Yordani, Yahweh akamwambia Yoshua,
And it cometh to pass, when all the nation hath completed to pass over the Jordan, that Jehovah speaketh unto Joshua, saying,
2 “Chagueni wenyewe watu waume kumi na wawili, mmoja katika kila kabila.
'Take for you out of the people twelve men, one man — one man out of a tribe;
3 Wape agizo hilo: 'Chukueni mawe kumi na mbili kutoka katikati ya Yordani mahali wanaposimama makuhani katika nchi kavu, na wayalete na kuyaweka chini katika sehemu ambapo mtalala usiku wa leo.
and command ye them, saying, Take up for you from this [place], from the midst of the Jordan, from the established standing-place of the feet of the priests, twelve stones, and ye have removed them over with you, and placed them in the lodging-place in which ye lodge to-night.'
4 Kisha Yoshua akawaita wanaume kumi na wawili ambao aliwachagua kutoka katika makabila ya Israeli, mmoja kutoka kila kabila.
And Joshua calleth unto the twelve men whom he prepared out of the sons of Israel, one man — one man out of a tribe;
5 Yoshua akawaambia, “Nendeni mbele za sanduku la Yahweh Mungu wenu katikati ya Yordani. Kila mmoja wenu achukue jiwe moja mabegani mwake, kulingana na hesabu ya makabila ya watu wa Israeli.
and Joshua saith to them, 'Pass over before the ark of Jehovah your God unto the midst of the Jordan and lift up for you each, one stone on his shoulder, according to the number of the tribes of the sons of Israel,
6 Hii itakuwa ni ishara miongoni mwenu kwa ajili yenu wakati watoto wenu watakapowauliza katika siku zijazo, 'Nini maana ya mawe haya kwenu?'
so that this is a sign in your midst, when your children ask hereafter, saying, What [are] these stones to you?
7 Ndipo mtakapowaambia, 'Maji ya Yordani yalitengwa mbele ya sanduku la Yahweh. Lililpopitishwa katika Yordani, maji ya Yordani yalisimamishwa. Hivyo, mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.'”
that ye have said to them, Because the waters of the Jordan were cut off, at the presence of the ark of the covenant of Jehovah; in its passing over into the Jordan were the waters of the Jordan cut off; and these stones have been for a memorial to the sons of Israel — to the age.'
8 Watu waisraeli walifanya kama Yoshua alivyowaagiza, na walichukua mawe kumi na mbili kutoka katikati ya Yordani, kama Yahweh alivyomwambia Yoshua, walipangwa sawa sawa na hesabu ya makabila ya watu wa Israeli. Waliyachukua mawe mpaka mahali walipolala na wakayaweka chini huko.
And the sons of Israel do so as Joshua commanded, and take up twelve stones out of the midst of the Jordan, as Jehovah hath spoken unto Joshua, according to the number of the tribes of the sons of Israel, and remove them over with them unto the lodging-place, and place them there,
9 Kisha Yoshua akayapanga mawe kumi na mbili katikati ya Yordani, katika sehemu ambapo ilisimama miguu ya makuhani waliolichukua sanduku la agano. Na kumbukumbu hiyo ipo hadi leo.
even the twelve stones hath Joshua raised up out of the midst of the Jordan, the place of the standing of the feet of the priests bearing the ark of the covenant, and they are there unto this day.
10 Makuhani waliolichukua sanduku walisimama katikati ya Yordani mpaka pale kila kitu ambacho Yahweh alimwamuru Yoshua kuwaambia watu kilipokamilika, sawa sawa na yote ambayo Musa alimwagiza Yoshua. Watu walifanya haraka na wakavuka.
And the priests bearing the ark are standing in the midst of the Jordan till the completion of the whole thing which Jehovah commanded Joshua to speak unto the people, according to all that Moses commanded Joshua, and the people haste and pass over.
11 Wakati watu wote walipokwisha kuvuka, sanduku la Yahweh pamoja na makuhani walivuka mbele za watu.
And it cometh to pass when all the people have completed to pass over, that the ark of Jehovah passeth over, and the priests, in the presence of the people;
12 Kabila la Rubeni, kabila la Gadi, na nusu ya kabila la Manase walipita kama jeshi mbele ya watu wa Israeli, kama ambavyo Musa alivyowaambia.
and the sons of Reuben, and the sons of Gad, and the half of the tribe of Manasseh, pass over, by fifties, before the sons of Israel, as Moses had spoken unto them;
13 Yapata watu watu elfu arobaini walioandaliwa kwa vita walipita mbele za Yahweh, kwa ajili ya vita katika uwanda wa Yeriko.
about forty thousand, armed ones of the host, passed over before Jehovah for battle, unto the plains of Jericho.
14 Katika siku hiyo Yahweh alimfanya Yoshua kuwa mkuu katika macho ya watu wote wa Israeli. Walimheshimu - kama walivyomheshimu Musa - siku zake zote.
On that day hath Jehovah made Joshua great in the eyes of all Israel, and they reverence him, as they reverenced Moses, all days of his life.
15 Kisha Yahweh akamwambia Yoshua,
And Jehovah speaketh unto Joshua, saying,
16 “Waamuru makuhani wanaolibeba sanduku la ushuhuda watoke katika Yordani.”
'Command the priests bearing the ark of the testimony, and they come up out of the Jordan.'
17 Hivyo Yoshua akawaamuru makuhani, '' pandeni mtoke Yordani.”
And Joshua commandeth the priests, saying, 'Come ye up out of the Jordan.'
18 Wakati makuhani wenye kulibeba sanduku la agano la Yahweh walitoka katikati ya Yordani, na nyayo za miguu yao ilikuwa imeinuliwa katika nchi kavu, kisha maji ya Yordani yalirudi katika sehemu zake na kujaa hadi katika kingo zake kama ilivyokuwa siku nne zilizopita.
And it cometh to pass, in the coming up of the priests bearing the ark of the covenant of Jehovah out of the midst of the Jordan — the soles of the feet of the priests have been drawn up into the dry ground — and the waters of the Jordan turn back to their place, and go as heretofore over all its banks.
19 Katika siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, watu walikwea kutoka Yordani. Wakakaa huko Gilgali, mashariki mwa Yeriko.
And the people have come up out of the Jordan on the tenth of the first month, and encamp in Gilgal, in the extremity east of Jericho;
20 Mawe kumi na mawili ambayo yalichukuliwa katika Yordani, Yoshuua aliyasimamisha hapo Gilgali.
and these twelve stones, which they have taken out of the Jordan, hath Joshua raised up in Gilgal.
21 Aliwaambia watu wa Israeli, “wakati watoto wenu watakapowauliza baba zao katika wakai ujao, 'Mawe haya ni ya nini?'
And he speaketh unto the sons of Israel, saying, 'When your sons ask their fathers hereafter, saying, What [are] these stones?
22 Waambieni watoto wenu, 'Hapa ndipo Waisraeli walivuka Yordani katika nchi kavu.
then ye have caused your sons to know, saying, On dry land Israel passed over this Jordan;
23 Yahweh Mungu wenu aliyakausha maji ya Yordani, mpaka hapo Yahweh Mungu wako aliyoyafanya katika bahari ya mianzi, ambayo aliikausha kwa ajili yetu ili tupite juu yakes,
because Jehovah your God dried up the waters of the Jordan at your presence, till your passing over, as Jehovah your God did to the Red Sea which He dried up at our presence till our passing over;
24 ili kwamba watu wote wa nchi wajue kwamba mkono wa Yahweh ni nguvu, na kwamba mtamweshimu Yahweh Mungu wenu milele.''
so that all the people of the land do know the hand of Jehovah that it [is] strong, so that ye have reverenced Jehovah your God all the days.'

< Yoshua 4 >