< Yoshua 3 >

1 Yoshua aliamka asubuhi na mapema, nao walisafiri kutoka Shitimu. Walifika Yordani, yeye na watu wote wa Israeli, na wakapiga kambi hapo kabla hawajavuka ng'ambo.
And he rose early Joshua in the morning and they set out from Shittim and they came to the Jordan he and all [the] people Israel and they stayed there before they passed over.
2 Baada ya siku tatu, maafisa walienda katika kambi, wakawaagiza watu,
And it was from [the] end of three days and they passed the officers in [the] midst of the camp.
3 “Mtakapoona sanduku la agano la Yahweh Mungu wenu, na makuhani kutoka miongoni mwa Walawi wamelibeba, ni lazima muondoke sehemu hii na kulifuata.
And they commanded the people saying when see you [the] ark of [the] covenant of Yahweh God your and the priests the Levites carrying it and you you will set out from place your and you will go behind it.
4 Lazima kuwe na umbali wa dhiraa elfu moja kati yenu na sanduku. Msilisogelee karibu, ili muweze kuiona njia ya kupitia, kwakuwa hamjawahi kupita njia hii kabla.
Nevertheless - a distance it will be between you (and between it *Qk) about two thousand cubit[s] by measurement may not you draw near to it so that that you may know the way which you will go in it for not you have passed in the way from yesterday three days ago.
5 Yoshua akawaambia watu, “Jitakaseni ninyi wenyewe keso, kwa kuwa Yahweh atafanya maajabu miongoni mwenu.”
And he said Joshua to the people consecrate yourselves for tomorrow he will do Yahweh in midst your wonders.
6 Kisha Yoshua akawaambia makuhani, “Chukueni sanduku la agano, na kulipitisha mbele za watu.” Hivyo, wakalichukua sanduku la agano na wakaenda mbele za watu.
And he said Joshua to the priests saying lift up [the] ark of the covenant and pass over before the people and they lifted up [the] ark of the covenant and they went before the people.
7 Yahweh akamwambia Yoshua, “Siku hii nitakufanya kuwa mtu mkubwa katika macho ya Waisraeli wote. Watajua kuwa kama nilivyokuwa na Musa ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe.
And he said Yahweh to Joshua the day this I will begin to make great you in [the] eyes of all Israel that they will know! that just as I was with Moses I will be with you.
8 Utawaamuru makuhani ambao hulibeba sanduku la agano, 'Mtakapofika katika ukingo wa maji ya Yordani, ni lazima msimame katika Mto Yordani.'”
And you you will command the priests [the] bearers of [the] ark of the covenant saying when come you to [the] edge of [the] waters of the Jordan in the Jordan you will stand still.
9 Kisha Yoshu akawaambia watu wa Israeli, “Njooni hapa na msikilize maneno ya Yahweh Mungu wenu.
And he said Joshua to [the] people of Israel draw near hither and hear [the] words of Yahweh God your.
10 Kwa hili mtajua kwamba Mungu aliye hai yuko miongoni mwenu na kwamba atawaondosha mbele yenu Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagrigashi, Waamori na Wayebusi.
And he said Joshua by this you will know! that God living [is] in midst your and certainly he will dispossess from before you the Canaanite[s] and the Hittite[s] and the Hivite[s] and the Perizzite[s] and the Girgashite[s] and the Amorite[s] and the Jebusite[s].
11 Tazama! Sanduku la agano la Bwana wa nchi yote litavuka mbele yenu katika Yordani.
Here! [the] ark of the covenant [the] lord of all the earth [is] about to pass on before you in the Jordan.
12 Sasa chagueni wanaume kumi na wawili kutoka katika makabila ya Israeli, mmoja katika kila kabila.
And therefore take for yourselves two plus ten man from [the] tribes of Israel a man one a man one to the tribe.
13 Wakati nyayo za miguu ya makuhani walichukualo sanduku la Yahweh, Bwana wa nchi yote, zitakapogusa maji ya Yordani, maji ya Yordani yatatindika, na hata maji yatiririkayo kutoka juu yatakoma kutiririka nayo yatasimama kama chuguu.
And it will be when rest [the] soles of [the] feet of the priests [the] bearers of [the] ark of Yahweh [the] lord of all the earth in [the] waters of the Jordan [the] waters of the Jordan they will be cut off! the waters that are coming down from to above so they may stand a heap one.
14 Hivyo wakati watu walipotoka ili kuvuka Yordani, makuhani waliobeba sanduku la agano waende mbele ya watu.
And it was when set out the people from tents their to pass over the Jordan and the priests [the] bearers of the ark the covenant before the people.
15 Mara tu wale walichukuao sanduku wakiisha kufika Yordani, na miguu ya watu wale waliobeba sanduku itakapotiwa katika ukingo wa maji (maana sasa Yordani hujaa hadi katika kingo zake zote katika kipindi chote cha mavuno),
And just as came [the] bearers of the ark to the Jordan and [the] feet of the priests [the] bearers of the ark they were dipped in [the] edge of the waters and the Jordan it is full over all banks its all [the] days of harvest.
16 maji yote yaliyotiririka kutoka juu yalisimama katika chuguu kimoja. Maji yakakoma kutiririka kutoka katika umbali mrefu. Maji yaliacha kutiririka kutoka Adam, mji ulio karibu na Zarethani, hadi bahari ya Negevu, Bahari ya Chumvi. Na watu walivuka ng'ambo karibu na Yeriko.
And they stood the waters which came down from to above they rose a heap one far away very (from Adam *QK) the city which [is] from [the] side of Zarethan and which went down to [the] sea of the Arabah [the] Sea of Salt they were complete they were cut off and the people they passed over before Jericho.
17 Makuhani waliolibeba sanduku la agano la Yahweh walisimama katika nchi kavu katikati ya Yordani mpaka watu wote wa Israeli walipokwisha kuvuka katika nchi kavu.
And they stood the priests [the] bearers of the ark [the] covenant of Yahweh on the dry ground in [the] middle of the Jordan firmly and all Israel [were] passing over on the dry ground until that they had finished all the nation to pass over the Jordan.

< Yoshua 3 >