< Yoshua 23 >

1 Na baada ya siku nyingi, kipindi ambacho Yahweh alikuwa ameipa Israeli pumziko kutoka maadui zao waliowazunguka,
And it cometh to pass, many days after that Jehovah hath given rest to Israel from all their enemies round about, that Joshua is old, entering into days,
2 Joshua alikuwa mzee sana. Yoshua aliwaita Waisraeli wote, na wazee wao, na viongozi, na waamuzi, na kwa maafisa, na kisha akawaambia, “Mimi nimezeeka sana.
and Joshua calleth for all Israel, for its elders, and for its heads, and for its judges, and for its authorities, and saith unto them, 'I have become old; I have entered into days;
3 Mmeshaona kila kitu ambacho Yahweh Mungu wenu ameshafanya kwa mataifa haya yote kwa ajili yenu, kwa kuwa ni Yahweh Mungu wenu ambaye amewapigania ninyi.
and ye — ye have seen all that Jehovah your God hath done to all these nations because of you, for Jehovah your God [is] He who is fighting for you;
4 Tazama! Nimeshawakabidhi kwenu mataifa yaliyosalia ili kuyateka kwa ajili ya kupata urithi ya makabila yenu, sambasamba na mataifa yote ambayo tayari nimeshayaangamiza, tangu Yordani hadi Bahari kuu katika upande wa magharibi.
see, I have caused to fall to you these nations who are left for an inheritance to your tribes, from the Jordan, (and all the nations which I cut off), and the great sea, the going in of the sun.
5 Yahweh Mungu wenu atayaondoa. Atayafukuzia mbali kutoka kwenu. Ataiteka nchi yao, nanyi mtaimiliki nchi yao, kama vile Yahweh Mungu wenu alivyowaahidi ninyi.
'As to Jehovah your God, He doth thrust them from your presence, and hath dispossessed them from before you, and ye have possessed their land, as Jehovah your God hath spoken to you,
6 Hivyo, iweni jasiri, ili kwamba mtunze na kuyafanya yale yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa, msikengeuke upande wa kulia wala upande wa kushoto,
and ye have been very strong to keep and to do the whole that is written in the Book of the Law of Moses, so as not to turn aside from it right or left,
7 basi msichanganyikane na mataifa haya ambayo yamesalia miongoni mwenu, wala msiyataje majina ya miungu yao, wala msiape kwayo, wala msiiabudu, wala msiipigie magoti.
so as not to go in among these nations, these who are left with you; and of the name of their gods ye do not make mention, nor do ye swear, nor do ye serve them, nor do ye bow yourselves to them;
8 Badala yake, mnatakiwa kumshika sana Yahweh Mungu wenu kama vile mlivyofanya siku hii ya leo.
but to Jehovah your God ye do cleave, as ye have done till this day.
9 Kwa kuwa Yahweh ameyafukuzia mbali mbele yenu mataifa makubwa yenye nguvu. Hakuna hata mmoja aliyeweza kusimama mbele yenu hata siku hii ya leo.
And Jehovah is dispossessing from before you nations great and mighty; as for you, none hath stood in your presence till this day;
10 Mtu yeyote mmoja wa kwenu atawafanya watu elfu wakimbie mbali, kwa kuwa Yahweh Mungu wenu, ndiye anayepigania ninyi, kama vile alivyowaahidi.
one man of you doth pursue a thousand, for Jehovah your God [is] He who is fighting for you, as He hath spoken to you;
11 Zingatieni kwa uangalifu ili mmpende Yahweh Mungu wenu.
and ye have been very watchful for yourselves to love Jehovah your God.
12 Lakini kama mkiegeuka na kushikamana na watu walioalia wa mataifa haya waliobaki miongoni mwenu, au kuoana nao, au kama mkishirikiana pamoja nao, na wao pamoja nanyi,
'But — if ye at all turn back and have cleaved to the remnant of these nations, these who are left with you, and intermarried with them, and gone in to them, and they to you,
13 jueni kwa hakika kwamba Yahweh Mungu wenu hatayafukuzia mbali mataifa haya yatoke kati yenu. Badala yake, watakuwa kitanzi na mtego kwenu, viboko migongoni mwenu na miiba machoni mwenu, mpaka pale mtakapoangamia katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
know certainly that Jehovah your God is not continuing to dispossess these nations from before you, and they have been to you for a gin, and for a snare, and for a scourge, in your sides, and for thorns in your eyes, till ye perish from off this good ground which Jehovah your God hath given to you.
14 Na sasa ninaenda katika njia ya dunia yote, na mnajua kwa moyo na roho zenu zote kwamba hakuna hata neno moja ambalo halijatimia kati ya mambo yote mazuri ambayo Yahweh Mungu wenu aliyaahidi juu yenu. Vitu hivi vyote vimetokea kwa ajili yenu. Hakuna hata moja lililoshindikana.
'And lo, I am going, to-day, in the way of all the earth, and ye have known — with all your heart, and with all your soul — that there hath not fallen one thing of all the good things which Jehovah your God hath spoken concerning you; the whole have come to you; there hath not failed of it one thing.
15 Lakini kama kila neno ambalo Yahweh Mungu wenu alilowaahidi limekwisha kutimia, hivyo Yahweh atawaletea juu yenu mabaya yote mpaka pale atakapokuwa amewaangamiza katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
'And it hath been, as there hath come upon you all the good thing which Jehovah your God hath spoken unto you, so doth Jehovah bring upon you the whole of the evil thing, till His destroying you from off this good ground which Jehovah your God hath given to you;
16 Atafanya hivi kama mtalivunja agano la Yahweh Mungu wenu, ambalo aliwaagizeni kulitunza. Kama mtaenda na kuiabudu miungu mingine na kuiinamia, ndipo hasira ya Yahweh itawaka kinyume nanyi, na ninyi mtaangamia upesi katika nchi nzuri ambayo amekwisha kuwapeni ninyi.”
in your transgressing the covenant of Jehovah your God which He commanded you, and ye have gone and served other gods, and bowed yourselves to them, then hath the anger of Jehovah burned against you, and ye have perished hastily from off the good land which He hath given to you.'

< Yoshua 23 >