< Yoshua 21 >

1 Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
Tad Levitu cilts tēvi piegāja pie priestera Eleazara un pie Jozuas, Nuna dēla, un pie Israēla bērnu cilts tēviem,
2 Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
Un runāja uz tiem Šīlo Kanaāna zemē, sacīdami: Tas Kungs caur Mozu pavēlējis, mums dot pilsētas, kur varam dzīvot, ar ganībām priekš mūsu lopiem.
3 Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
Tad Israēla bērni Levitiem deva no savām daļām pēc Tā Kunga vārda šīs pilsētas un viņu ganības.
4 Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
Un mesli krita Kehāta radiem. Un priestera Ārona bērniem no Levitiem caur mesliem krita trīspadsmit pilsētas no Jūda cilts un no Sīmeana cilts un no Benjamina cilts.
5 Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
Un tiem citiem Kehāta bērniem caur mesliem krita desmit pilsētas no Efraīma cilts radiem un no Dana cilts un no Manasus puscilts.
6 Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
Un Geršona bērniem caur mesliem krita trīspadsmit pilsētas no Īsašara cilts radiem un no Ašera cilts un no Naftalus cilts un no Manasus puscilts Basanā.
7 Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
Merarus bērniem pēc viņu radiem krita divpadsmit pilsētas no Rūbena cilts un no Gada cilts un no Zebulona cilts.
8 Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
Tā Israēla bērni Levitiem deva caur meslošanu šīs pilsētas un viņu ganības, kā Tas Kungs caur Mozu bija pavēlējis.
9 Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
Un no Jūda bērnu cilts un no Sīmeana bērnu cilts tie deva šīs pilsētas, ko pie vārda nosauca,
10 Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
Ka tie piederētu Ārona bērnu bērniem, no Kehāta radiem, no Levja bērniem; jo tie pirmie mesli viņiem krita.
11 Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
Un tie tiem deva Kiriat-Arbu, Enaka tēva pilsētu, tā ir Hebrone Jūda kalnos un viņas apkārtējās ganības.
12 Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
Bet tās pilsētas tīrumu un līdz ar viņas ciemiem tie deva Kālebam, Jefunna dēlam, par dzimtu.
13 Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
Un tie deva priestera Ārona bērniem to glābšanas pilsētu priekš nokāvējiem, Hebroni un viņas ganības, un Libnu un viņas ganības,
14 Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
Un Jatiru un viņas ganības, un Estemou un viņas ganības,
15 Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
Un Holonu un viņas ganības, un Debiru un viņas ganības,
16 Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
Un Aīnu un viņas ganības, un Jūtu un viņas ganības, un BetŠemesu un viņas ganības, - deviņas pilsētas no šīm divām ciltīm.
17 Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
Un no Benjamina cilts: Gibeonu un viņas ganības, Ģebu un viņas ganības,
18 na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
Un Anatotu un viņas ganības, un Almonu un viņas ganības, - četras pilsētas.
19 Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
Pavisam priestera Ārona dēliem bija trīspadsmit pilsētas ar savām ganībām.
20 Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
Bet Kehāta bērnu radiem, tiem Levitiem, tiem citiem Kehāta bērniem krita caur mesliem tās pilsētas no Efraīma cilts.
21 Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
Un tiem deva Šehemi, to glābšanās pilsētu priekš nokāvējiem, un viņas ganības Efraīma kalnos, un Ģezeru un viņas ganības,
22 na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
Un Ķibcaīm un viņas ganības, un Bet-Oronu un viņas ganības, četras pilsētas.
23 Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
Un no Dana cilts: Elteku un viņas ganības, un Ģibetonu un viņas ganības,
24 Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
Un Ajaloni un viņas ganības, Gat-Rimonu un viņas ganības, - četras pilsētas.
25 Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
Un no Manasus puscilts: Taēnaku un viņas ganības, un Gat-Rimonu un viņas ganības, divas pilsētas:
26 Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
Pavisam kopā priekš tiem citiem Kehāta bērnu radiem desmit pilsētas ar savām ganībām.
27 Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
Un Geršona bērniem no Levitu radiem (krita) no Manasus puscilts tā glābšanās pilsēta priekš nokāvējiem, Golana Basanā un viņas ganības un Beēstra un viņas ganības, - divas pilsētas.
28 Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
Un no Īsašara cilts Ķisjone un viņas ganības, un Dobrate un viņas ganības,
29 Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
Jarmute un viņas ganības, Enganim un viņas ganības, - četras pilsētas,
30 Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
Un no Ašera cilts Mizeale un viņas ganības, Abdone un viņas ganības.
31 Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
Elkata un viņas ganības, un Reoba un viņas ganības, - četras pilsētas.
32 Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
Un no Naftalus cilts tā glābšanās pilsēta priekš nokāvējiem Ķedesā Galilejā un viņas ganības, Amot-Dore un viņas ganības, un Kartane un viņas ganības, - trīs pilsētas.
33 Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
Pavisam Geršona bērniem pēc viņu radiem ir trīspadsmit pilsētas ar savām ganībām.
34 Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
Un Merarus bērnu radiem, tiem citiem Levitiem, (krita) no Zebulona cilts Jokneane un viņas ganības, un Karta un viņas ganības,
35 Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
Dimna un viņas ganības, Naālale un viņas ganības, - četras pilsētas.
36 Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
Un no Rūbena cilts Becere un viņas ganības, Jāca un viņas ganības.
37 na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
Ķedemota un viņas ganības, un Mepaāta un viņas ganības, - četras pilsētas.
38 Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
Un no Gada cilts krita tā glābšanās pilsēta priekš nokāvējiem, Rāmote Gileādā un viņas ganības,
39 Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
Un Mahānaīm un viņas ganības, Hešbona un viņas ganības, Jaēzere un viņas ganības, pavisam četras pilsētas.
40 Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
Visas šīs pilsētas piederēja Merarus bērniem pēc viņu radiem, kas arī vēl bija no Levitu radiem, un caur mesliem tiem krita divpadsmit pilsētas.
41 Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
Pavisam Levitu pilsētu Israēla bērnu zemē bija četrdesmit un astoņas ar savām ganībām.
42 Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
Visas šīs pilsētas bija savrup ar savām apkārtējām ganībām; tā bija ar visām šīm pilsētām.
43 Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
Tā Tas Kungs Israēlim deva visu to zemi, ko Viņš bija zvērējis dot viņu tēviem, un tie to uzņēma un tur dzīvoja.
44 Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
Un Tas Kungs tiem deva mieru visapkārt, tā kā Tas Kungs viņu tēviem bija zvērējis, un no visiem viņu ienaidniekiem neviens nepastāvēja viņu priekšā, visus viņu ienaidniekus Tas Kungs deva viņu rokā.
45 Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.
Un neviena vārda netrūka no visiem tiem labiem vārdiem, ko Tas Kungs uz Israēla namu bija runājis, - viss tas notika.

< Yoshua 21 >