< Yoshua 21 >

1 Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
And they approached [the] leaders of [the] fathers of the Levites to Eleazar the priest and to Joshua [the] son of Nun and to [the] leaders of [the] fathers of the tribes of [the] people of Israel.
2 Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
And they spoke to them at Shiloh in [the] land of Canaan saying Yahweh he commanded by [the] hand of Moses to give to us cities to dwell in and pasture lands their for livestock our.
3 Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
And they gave [the] people of Israel to the Levites some of inheritance their to [the] mouth of Yahweh the cities these and pasture lands their.
4 Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
And it came out the lot of [the] clans of the Kohathite[s] and it belonged to [the] descendants of Aaron the priest of the Levites from [the] tribe of Judah and from [the] tribe of the Simeonite[s] and from [the] tribe of Benjamin by the lot cities thir-teen.
5 Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
And [belonged] to [the] descendants of Kohath which remained from [the] clans of [the] tribe of Ephraim and from [the] tribe of Dan and from [the] half of [the] tribe of Manasseh by the lot cities ten.
6 Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
And [belonged] to [the] descendants of Gershon from [the] clans of [the] tribe of Issachar and from [the] tribe of Asher and from [the] tribe of Naphtali and from [the] half of [the] tribe of Manasseh in Bashan by the lot cities thir-teen.
7 Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
[and belonged] to [the] descendants of Merari to clans their from [the] tribe of Reuben and from [the] tribe of Gad and from [the] tribe of Zebulun cities two plus ten.
8 Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
And they gave [the] people of Israel to the Levites the cities these and pasture lands their just as he had commanded Yahweh by [the] hand of Moses by the lot.
9 Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
And they gave from [the] tribe of [the] descendants of Judah and from [the] tribe of [the] descendants of Simeon the cities these which he called them by name.
10 Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
And it belonged to [the] descendants of Aaron one of [the] clans of the Kohathite[s] from [the] descendants of Levi for to them it belonged the lot first.
11 Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
And they gave to them Kiriath Arba [the] father of Anak that [is] Hebron in [the] hill country of Judah and pasture lands its around it.
12 Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
And [the] field[s] of the city and villages its they gave to Caleb [the] son of Jephunneh possession his.
13 Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
And to [the] descendants of - Aaron the priest they gave [the] city of refuge of the killer Hebron and pasture lands its and Libnah and pasture lands its.
14 Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
And Jattir and pasture lands its and Eshtemoa and pasture lands its.
15 Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
And Holon and pasture lands its and Debir and pasture lands its.
16 Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
And Ain and pasture lands its and Juttah and pasture lands its Beth Shemesh and pasture lands its cities nine from with [the] two the tribes these.
17 Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
And from [the] tribe of Benjamin Gibeon and pasture lands its Geba and pasture lands its.
18 na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
Anathoth and pasture lands its and Almon and pasture lands its cities four.
19 Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
All [the] cities of [the] descendants of Aaron the priests [were] thir-teen cities and pasture lands their.
20 Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
And to [the] clans of [the] descendants of Kohath the Levites who remained of [the] descendants of Kohath and it was [the] cities of lot their from [the] tribe of Ephraim.
21 Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
And they gave to them [the] city of refuge of the killer Shechem and pasture lands its in [the] hill country of Ephraim and Gezer and pasture lands its.
22 na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
And Kibzaim and pasture lands its and Beth Horon and pasture lands its cities four.
23 Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
And from [the] tribe of Dan Eltekeh and pasture lands its Gibbethon and pasture lands its.
24 Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
Aijalon and pasture lands its Gath Rimmon and pasture lands its cities four.
25 Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
And from [the] half of [the] tribe of Manasseh Taanach and pasture lands its and Gath Rimmon and pasture lands its cities two.
26 Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
All [the] cities ten and pasture lands their [belonged] to [the] clans of [the] descendants of Kohath which remained.
27 Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
And to [the] descendants of Gershon from [the] clans of the Levites from [the] half of [the] tribe of Manasseh [the] city of refuge of the killer (Golan *QK) in Bashan and pasture lands its and Beeshtarah and pasture lands its cities two.
28 Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
And from [the] tribe of Issachar Kishion and pasture lands its Daberath and pasture lands its.
29 Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
Jarmuth and pasture lands its En Gannim and pasture lands its cities four.
30 Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
And from [the] tribe of Asher Mishal and pasture lands its Abdon and pasture lands its.
31 Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
Helkath and pasture lands its and Rehob and pasture lands its cities four.
32 Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
And from [the] tribe of Naphtali [the] city of - refuge of the killer Kedesh in Galilee and pasture lands its and Hammoth Dor and pasture lands its and Kartan and pasture lands its cities three.
33 Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
All [the] cities of the Gershonite[s] to clans their [were] thir-teen citi[es] and pasture lands their.
34 Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
And to [the] clans of [the] descendants of Merari the Levites which remained from with [the] tribe of Zebulun Jokneam and pasture lands its Kartah and pasture lands its.
35 Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
Dimnah and pasture lands its Nahalal and pasture lands its cities four.
36 Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
(And from [the] tribe of Reuben Bezer and pasture lands its and Jahaz and pasture lands its. *R)
37 na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
(Kedemoth and pasture lands its and Mephaath and pasture lands its cities four. *R)
38 Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
And from [the] tribe of Gad [the] city of refuge of the killer Ramoth in Gilead and pasture lands its and Mahanaim and pasture lands its.
39 Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
Heshbon and pasture lands its Jazer and pasture lands its all [the] cities [were] four.
40 Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
All the cities of [the] descendants of Merari to clans their which remained of [the] clans of the Levites and it was lot their cities two plus ten.
41 Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
All [the] cities of the Levites in [the] midst of [the] possession of [the] people of Israel [were] cities forty and eight and pasture lands their.
42 Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
They were the cities these a city a city and pasture lands its around it thus for all the cities these.
43 Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
And he gave Yahweh to Israel all the land which he had sworn to give to ancestors their and they took possession of it and they dwelt in it.
44 Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
And he gave rest Yahweh to them from round about according to all that he had sworn to ancestors their and not he stood anyone in faces their from all enemies their all enemies their he gave Yahweh in hand their.
45 Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.
Not it fell a word from every word good which he had spoken Yahweh to [the] house of Israel everything it came.

< Yoshua 21 >